fbpx

Trakti Namba 03

TRAKTI NAMBA 03

Hukumu na Mavuno

1

Hati miliki 1934, 1942

V.T. Houteff

Haki zote zimehifadhiwa

Trakti hii inasambazwa bila malipo kwa shauku ya kupenda kufikia kila akili inayotafuta ukweli ambayo inataka kuepuka njia inayoongoza kwa uharibifu wa mwili na roho.

TRAKTI NAMBA 03

Toleo la Tatu

Jumuiya ya Wadaudi Waadventista wa Sabato

(Ushirika Huru Unaojumuisha Kanisa)

Mlima Karmeli, Waco, Texas

S.L.P. 23738, Waco, TX 76702

+ 1-254-855-9539

www.gadsda.com

info@gadsda.com

Kimechapishwa Marekani

2

KUKANGANYIKA KWA KUWA MUHIMU

Ingawa ni kazi ya kutia taji wokovu wetu na ya kuanzishwa kwa Ufalme wa Kristo duniani, hata sasa “hukumu ya upelelezi” ni mojawapo wa masomo ya Biblia yaliyofahamika kwa uchache yaliyochafuliwa sana na kuchanganywa ya kizazi hiki. Lingekuwa si la umuhimu kwa wokovu wetu, adui hangeweza kutumia kila jitihada iwezekanavyo kulifunika katika giza. La lazima, hatimaye, ni hitaji lenye bidii ya kuyachunguza Maandiko “kama kuitafuta hazina iliyofichwa,” na kumwomba Mungu kwa uongozi wa Roho Wake ili kuweza kulielewa vyema somo hili muhimu kabisa. Usiofaa, hata hivyo, ni uchunguzi wowote kwa ukweli isipokuwa nia iwe ya kujifunza na kuyatenda mpenzi ya Mungu. Kwa hivyo, “Mtu akipenda kuyatenda mapenzi Yake,” asema Yesu, “atajua habari ya yale mafunzo, kwamba yatoka kwa Mungu.” Yohana 7:17. {TN3: 3.1}

Kwa sababu somo la hukumu limefundishwa kwa mifano na kwa mithali, na kwa kuwa Bwana huelezea kwamba mafundisho Yake kwa mithali ni hivyo ili kwamba wanafunzi Wake tu wataweza kujua siri za ufalme wa mbinguni (Mat. 13:11), pasipo shaka, kwa hivyo,

Hakuna Ila Wafuasi Wake Wanaweza Kuelewa Kweli Yote. {TN3: 3.2}

“Tena ufalme wa mbinguni” Anasema, “umefanana na hazina iliyositirika katika shamba; ambayo mtu alipoiona, aliificha; na kwa furaha yake akaenda akauza alivyo navyo vyote, akalinunua shamba lile. Tena

3

ufalme wa mbinguni umefanana na mfanya biashara, mwenye kutafuta lulu nzuri; naye alipoona lulu moja ya thamani kubwa, alikwenda akauza alivyo navyo vyote, akainunua.” Mat. 13:44-46. {TN3: 3.3}

Katika mithali hizi, Kristo anaweka wazi ukweli wa sasa kama hali ya lazima ya kuanzisha ufalme Wake, na juhudi kuu kama hali ya lazima ya kuingia ndani yake. Kwa hivyo “hakuna,” inatangaza Roho ya Unabii, “ila tu wale ambao wameziimarisha akili kwa kweli za Biblia watasimama katika pambano kuu la mwisho. Kwa kila nafsi utakuja mtihani wa kujihoji, Je, nitamtii Mungu kuliko wanadamu? Saa ya maamuzi imewadia hata sasa. Je! Miguu yetu imesimama kwenye mwamba wa Neno la Mungu lisilobadilika?” — Pambano Kuu, uk. 593, 594. {TN3: 4.1}

Hebu tutoke katika ubumbuazi wa kiburi kwa neema ya Mungu, hata sasa kudhania Yeye anahusika na swala lolote linalotokea maishani mwetu. Yeye amefanya kikamilifu sehemu Yake kuweka ramani kikamilifu njia nyembamba ya kwenda kwa ufalme; sasa hebu tufanye uaminifu wetu kuifuata hadi mwisho wake, kwa furaha ambayo inatungojea huko! Lakini hatutafanya hivyo kamwe isipokuwa kurudi kwenye mipaka ya kale kwa kumwacha Ibilisi, ambaye amewageuza watu wa Mungu kutoka kwa “Njia, na Kweli, na uzima” (Yohana 14:6), hadi kwa njia “ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu, Lakini mwisho wake ni njia za mauti.” Mith. 14:12. {TN3: 4.2}

4

HUKUMU NA MAVUNO KATIKA USHUHUDA, MFANO, SHEREHE NA TARAKIMU

—————————

Katika Nuru ya Shuhuda za Manabii

Kwa sababu baadhi msimamo umedumishwa kwa dhati kwamba ukweli huu wote muhimu hauwezi kuwekwa imara kwa Maandiko pekee, hebu msomaji basi apeane usikivu kwa lile ambalo Biblia inasema {TN3: 5.1}

“Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na mmoja aliye Mzee wa siku ameketi; mavazi Yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa Chake kama sufu safi; kiti Chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu Zake moto uwakao. Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele Yake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele Yake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.” Dan. 7:9, 10. {TN3: 5.2}

Katika maandiko haya yanaeleza kweli nne za kufungamana: (1) viti vya enzi havikuwepo kabla ya ufunguzi wa eneo katika maono; (2) Mzee wa siku alikuja na akaketi wakati viti vilipowekwa; (3) vitabu vilifunguliwa; (4) yote

5

ambayo (viti vya enzi, Mzee wa siku, na vitabu) hufunua taswira ya hukumu. Na maadamu vitabu dhahiri ni kitovu katika picha hiyo, swali kwa kawaida linatokea,

Ni Nini Sababu Ya Vitabu? {TN3: 5.3}

Msingi wa wazo sahihi la hukumu, ni ufahamu sahihi wa asili yake na sababu ya hivyo vitabu. Kuhusu la mwisho Yohana Waufunuo anasema: {TN3: 6.1}

“Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.” Ufu. 20:12. {TN3: 6.2}

Bila shaka, kwa hivyo, vitabu vinayo majina yote na kumbukumbu za wote watakaohukumiwa. Na kwa kawaida majina hayo na rekodi ziliingizwa wakati kila mtu alikuwa akiishi “Macho yako,” anasema mtunga Zaburi, “yaliniona kabla sijakamilika; Chuoni mwako ziliandikwa zote pia, Siku zilizoamriwa kabla hazijawa bado.” Zab. 139:16. “Bwana atahesabu, Awaandikapo mataifa, huyu alizaliwa humo.” Zab. 87:6. {TN3: 6.3}

Hivyo, Uvuvio unaonyesha kwamba matendo ya kila mmoja yamenakiliwa kwa usahihi wa kutisha katika vitabu vya mbinguni, na kwamba hiyo ndiyo sababu ya vitabu vina uhusiano kwa

6

Sababu Ya Hukumu. {TN3: 6.4}

Ya kwamba si kila jina lililoingizwa ndani ya vitabu vya Mwana-Kondoo litahifadhiwa mle, imethibitishwa na hitimisho la huzuni kwa maandiko yafuatayo: {TN3: 7.1}

“Bwana akamwambia Musa, Mtu ye yote aliyenitenda dhambi ndiye Nitakayemfuta katika kitabu Changu.” Kut. 32:33. “Na mtu ye yote akiondoa lo lote katika maneno ya unabii wa kitabu hiki, Mungu atamwondolea sehemu yake katika ule mti wa uzima, na katika ule mji mtakatifu, ambao habari zake zimeandikwa katika kitabu hiki.” Ufu. 22:19. {TN3: 7.2}

Kwa hivyo, vitabu vina majina ya umati mchanganyiko, — wote waliosimama imara katika imani na wakaendelea kwa uvumilivu hadi mwisho, na wale ambao hawakuweza. Alisema Kristo: “Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka.” Mat. 24:13. Ila wale ambao hawatavumilia watapotea. {TN3: 7.3}

“Kadhalika na hawa ndio wapandwao penye miamba, ambao kwamba wakiisha kulisikia lile neno, mara hulipokea kwa furaha; ila hawana mizizi ndani yao, bali hudumu muda mchache; kisha ikitokea dhiki au udhia kwa ajili ya lile neno, mara hujikwaa.” Marko 4:16,17. {TN3: 7.4}

“Ee Bwana, tumaini la Israeli, wote wakuachao watatahayarika. Wao watakaojitenga Nami wataandikwa katika

7

mchanga, kwa sababu wamemwacha Bwana, kisima cha maji yaliyo hai.” Yer. 17:13. {TN3: 7.5}

Hivyo, lazima ije siku ya kutoa hesabu, siku ambayo majina ya wale watakaopatikana hawastahili uzima wa milele yatafutwa kutoka katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo — tendo ambalo jina sahihi la heshima laweza kuwa, “hukumu ya upelelezi.” {TN3: 8.1}

Na sasa ya kwamba “wakati umefika kwa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu…,” “Ushiriki taabu pamoja nami, kama askari mwema wa Kristo Yesu.” (2 Tim. 2:3), kwa maana “ikianza [hukumu] kwetu sisi, mwisho wao wasioitii injili ya Mungu utakuwaje?” 1 Pet. 4:17. {TN3: 8.2}

Kwa sababu, hivyo, katika utimilifu wa wakati, hukumu itaanza katika nyumba ya Mungu, kanisa, kila mmoja anakabiliwa na hitaji la lazima la kujua

Namna Majina Yanavyohifadhiwa Katika Kitabu. {TN3: 8.3}

Mara tunapompokea Kristo kama Mwokozi wetu binafsi kupitia njia ya Neno la Kweli, — kwa wakati huo wa upeo Mungu anatusamehe dhambi zetu, na mikono iliyotiwa doa kwa damu ya Kalvari inaandika majina yetu katika Kitabu cha Uzima cha Mwana-Kondoo. Kisha wakati uo huo kalamu ya malaika huanza katika daftari kubwa ya mbinguni mambo ya maisha au ya mauti kwa uzoefu wetu wa Kikristo tofauti na ya zamani. Hata “nywele za vichwa vyenu zimehesabiwa zote.” Mat. 10:30. Kwa hivyo “Usikiache kinywa chako kuukosesha mwili wako; wala usiseme mbele ya huyo

8

malaika ya kwamba umepitiliwa; kwani Mungu akukasirikie sauti yako, na kuiharibu kazi ya mikono yako.” Mhu. 5:6. Kwa maana katika hukumu ya upelelezi vitabu vinafunguliwa na matendo yaliyofanywa katika mwili yanawekwa wazi kwa kutoa hesabu ya mwisho mbele ya Mzee wa siku. Wote ambao wamesimama imara hadi mwisho hapo dhambi zao zitaondolewa kutoka kwa vitabu na majina yao kuhifadhiwa ndani yake; ilhali wote ambao si washindi kisha milele dhambi zao zitahifadhiwa katika vitabu na majina yao kuondolewa humo. {TN3: 8.4}

Siku zote mtihani mkubwa zaidi wa mwanadamu, na mmoja ambao umewahi kuhusika karibu na uamuzi wa haraka, umekuwa katika kukunjua kwa gombo — katika kupatwa kwa ujumbe uliopita na mpya, — ukweli wa sasa. Katika kila tukio la namna hii kila mmoja ilimpasa kuamua: Je, Nitautii ukweli mpya na usiokuwa maarufu na kutembea katika nuru yake, kujiunga na wale wanaodharauliwa karibu na kila kiongozi wa kidini katika nchi? au je, Nitajiruhusu kuzuiliwa na uamuzi na ushauri wa ukasisi katika kanisa langu? {TN3: 9.1}

Wakati hukumu inaanza na vitabu kufunuliwa na kesi za kila kizazi zikipita mfululizo katika mapitio mbele ya jopo la mwamuzi, baadhi ya vizazi vinapatwa karibu jumla ya majina yanaondolewa badala ya dhambi. Wakati kizazi cha ujio wa kwanza wa Kristo kinapopimwa kwa mizani ya patakatifu, taifa lote litapatikana kuwa pungufu na majina yao yatafutwa kutoka kitabuni. Na hivyo kwa kiwango kinachotofautiana imekuwa hivyo katika utangulizi wa

9

kila ujumbe katika kila kizazi. “Vipindi tofauti katika historia ya kanisa kila kimoja kimetiwa alama na ustawi wa ukweli fulani maalum, kulingana na mahitaji ya watu wa Mungu kwa wakati huo. Kila ukweli mpya umefanyiza njia yake dhidi ya chuki na upinzani; wale waliobarikiwa na nuru yake walijaribiwa na kuteswa.” — Pambano Kuu, uk. 609. {TN3: 9.2}

Kwa hivyo, “wakati ujumbe unakuja kwa jina la Bwana kwa watu Wake, hakuna mtu anayeweza kujiruhusu kutofanya uchunguzi wa madai yake.” — Shuhuda kwa Kazi za Shule ya Sabato, uk. 65. Weka mbali chuki zote, maoni ya kibinafsi, na dhana za watu ambao hawabebi alama ya Uvuvio, na ambao husema maana yake kwa matendo yao: “Mimi ni tajiri, nimejitajirisha, wala sina haja ya kitu” (ukweli au manabii). Ufu. 3:17. {TN3: 10.1}

Biblia inaweza kufafanuliwa kwa usahihi tu na Roho Ambaye aliiandikisha. Yeye “atawaongoza awatie kwenye kweli yote; kwa maana hatanena kwa shauri Lake Mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayanena, na mambo yajayo atawapasha habari yake” ili mweze “kuthibitishwa katika ukweli wa sasa.” Na “Na kila mtu .… anayemkufuru Roho Mtakatifu [anayenena maovu dhidi ya ujumbe], hatasamehewa” kwa maana ndio njia ya pekee ambayo tunaweza kuokolewa (Yohana 16:13, 2 Pet. 1:12; Luka 12:10). {TN3: 10.2}

Vivyo hivyo, hatari kubwa ya watu haijawahi kuwa wao kusikiliza kosa

10

ila zaidi kukataa kwao ukweli wa sasa. “Iwapo ujumbe unakuja,” asema Bwana, “usiouelewa,vumilia ili uweze kusikiza sababu ambazo mjumbe anaweza kutoa, … basi wasilisha sababu zako thabiti, kwa maana msimamo wako hautatikiswa kwa kukutana na makosa.” — Shuhuda kwa Kazi za Shule ya Sabato, uk. 65, 66. “Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke.” 1 Kor. 10:12. {TN3: 10.3}

Wazi wazi, kwa hivyo, mwenendo wowote unaomwongoza mtu asiufanye uchunguzi wazi wa ujumbe wowote unaodai kwamba ni ukweli wa ziada, lazima bila kuepuka ajiletee uharibifu kwa nafsi yake. Ambapo kwa upande mwingine yeye anayeupokea ukweli lakini ashindwe kuishi na kuutangaza kwa uaminifu, hivyo hujiletea uharibifu pia — ambao Ezekieli huonya dhidi yake: “Tena mtu mwenye haki aiachapo haki yake, na kutenda uovu, Nami nikiweka kikwazo [ujumbe] mbele yake, atakufa; kwa sababu hukumwonya, atakufa katika uovu wake, wala matendo yake ya haki aliyoyatenda hayatakumbukwa; lakini damu yake nitaitaka mkononi mwako. Bali ukimwonya mwenye haki, kwamba yule mwenye haki asitende dhambi, tena ikiwa yeye hatendi dhambi, hakika ataishi, kwa sababu alikubali kuonywa; nawe umejiokoa roho yako.” Ezek. 3:20, 21. Lakini waovu “Na wafutwe katika chuo cha uhai, Wala pamoja na wenye haki wasiandikwe.” Zab. 69:28. {TN3: 11.1}

11

Hivi msingi imara, msimamo ambao umetangulia juu ya hukumu ya upelelezi unafanya misimamo yote ya upinzani

Hitimisho Zisizo Na Msingi. {TN3: 12.1}

Kwa sababu ya imani yao ya uongo kwamba kiti cha enzi cha Mungu kimekuwa siku zote ndani ya patakatifu na kwamba baada ya Kristo kupaa juu aliketi hapo kwa mkono wa kulia wa Baba Yake, watu wamejitahidi kuweka kila thibitisho linalowezekana kwamba Kristo aliingia “ndani ya pazia” mara baada ya kuwaacha wanafunzi Wake. Lakini kama juhudi hizo zote, ingawa zimekuwa na nia nzuri katika maslahi ya ukweli, zimetolewa na akili zisizovuviwa, si na Roho wa Kweli, ila kwa wazo lililoshikiliwa, basi lazima tumuombe Bwana Msaidizi aliyeahidiwa kwa bidii kutuongoza katika kweli yote, na kutuokoa kutoka kwa kiburi na kwa upofu wa kupuuza mambo na kubuni maamuzi kwa kusoma bila kwenda kwa undani. {TN3: 12.2}

“Nasi tuna lile neno la unabii lililo imara zaidi, ambalo, mkiliangalia, kama taa ing’aayo mahali penye giza, mwafanya vyema, mpaka kutakapopambazuka, na nyota ya asubuhi kuzuka mioyoni mwenu. Mkijua neno hili kwanza, ya kwamba hakuna unabii katika maandiko upatao kufasiriwa kama apendavyo mtu fulani tu. Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu.” 2 Pet. 1:19-21. {TN3: 12.2}

12

Msomaji mwenye hekima, kwa hivyo, tangu sasa ataacha kuzipatia nafasi nadharia na makisio ya kibinadamu ambayo humjaribu kabisa kuufanya mwili kuwa kinga yake. Badala yake ataangalia kwa uangalifu unabii wa Biblia na kwa ufafanusi uliovuviwa na atajifunza kutoka kwayo kwamba patakatifu ni

Chumba cha Muda cha Kiti cha Enzi cha Mungu. {TN3: 13.1}

Kwa sababu viumbe wa dunia, wenyewe hawajawahi kwenda mbinguni, kwa asili wao ni wageni kwa uhalisi wa mbinguni (1 Kor. 2:9), basi ili Mungu aufanye ukweli wa mbinguni waujue, lazima Aufunue kwa njia ya uhalisi wa duniani ambao wanajua. Hivyo kupitia kwa kazi ya hekalu la duniani huonekana kazi ya hekalu la mbinguni (Ebr. 9:1-9). Hakika, hekalu la juu likiwa ni mfano wa la duniani huduma za la kwanza kwa hivyo ni dhahiri kwa uhalisi katika huduma za la pili. Na ukweli kwamba hekalu la duniani lilichaguliwa kama mahali pa kuungama na kwa ajili ya msamaha wa dhambi, linaonyesha kwamba chumba cha kiti cha enzi katika hekalu la mbinguni ni cha muda tu. Kutoka humo, wakati dhambi ingalipo, Bwana huiendeleza kazi ya kuondoa kwa ulimwengu dhambi na wadhambi. Na nuru hii kwa zamu inaonyesha wazi kwamba kabla ya dhambi kuja katika ulimwengu hapangefaa kuwapo hekalu mbinguni. {TN3: 13.2}

“Nikaona,” akapaaza sauti kusema Waufunuo karibu 96 B.K., kuhusu kuonyeshwa kiti cha enzi katika patakatifu, “na tazama,

13

mlango ukafunguka mbinguni, na sauti ile ya kwanza niliyoisikia kama sauti ya baragumu ikinena nami, ikisema, Panda hata huku, Nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako upesi. {TN3: 13.3}

“Na mara nalikuwa katika Roho; na tazama, kiti cha enzi kimewekwa mbinguni na Mmoja ameketi juu ya kile kiti; na Yeye aliyeketi alionekana mithili ya jiwe la yaspi na akiki, na upinde wa mvua ulikizunguka kile kiti cha enzi, ukionekana mithili ya zumaridi. Na viti ishirini na vinne vilikizunguka kile kiti cha enzi, na juu ya vile viti naliona wazee ishirini na wanne, wameketi, wamevikwa mavazi meupe; na juu ya vichwa vyao walikuwa na taji za dhahabu. Na katika kile kiti cha enzi kunatoka umeme na sauti na ngurumo. Na taa saba za moto zikiwaka mbele ya kile kiti cha enzi, ndizo Roho saba za Mungu. Na mbele ya kile kiti cha enzi kulikuwa na mfano wa bahari ya kioo, kama bilauri; na katikati ya kile kiti cha enzi, na pande zote za kile kiti, walikuwako wenye uhai wanne, wamejaa macho mbele na nyuma.” {TN3: 14.1}

“Nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale wenye uhai wanne, na katikati ya wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, alikuwa kana kwamba amechinjwa, mwenye pembe saba na macho saba, ambazo ni Roho saba za Mungu zilizotumwa katika dunia yote…. Nikaona nikasikia sauti ya malaika wengi pande zote za kile kiti cha enzi, na za wale wenye uhai, na za wale wazee, na hesabu yao ilikuwa elfu kumi mara elfu kumi

14

na elfu mara elfu.” Ufu. 4: 1-6; 5:6,11. {TN3: 14.2}

Hapa inaletwa kwa mtazamo mandhari mara mbili. Kwa upande mmoja, mbele ya kiti cha enzi ni “taa saba zinazowaka” na “Mwana-Kondoo kana kwamba amechinjwa,” kuonyesha kwamba kiti cha enzi “kiliwekwa” huko kutumika wakati wa uangalizi. Nuru kutoka kwenye kinara cha taa inawakilisha nuru ya ukweli katika kanisa wakati damu ya Mwana-Kondoo inafanya upatanisho kwa ajili ya viumbe wakosefu. Kwa upande mwingine, juu ya kiti cha enzi anakaa Mzee wa siku, Hakimu, akizungukwa na jopo la wazee ishirini na wanne pamoja na mashahidi wa malaika, “elfu kumi mara elfu kumi, na elfu mara elfu”, pamoja na wenye uhai wanne (ambao, wakiwa “wamekombolewa” “kutoka kwa kila kabila, na lugha, na jamaa, na taifa” — Ufu. 5:8, 9, — kwa hivyo ni mfano wa watakatifu, — wote ambao dhambi zao zitafutwa kutoka kwa vitabu vya kumbukumbu, — kama vile wanyama wa Danieli 7 ni mfano wa falme zote ambazo zitaangamia katika dhambi zao), pamoja na Mwana-Kondoo, Wakili wetu, katikati. Yote haya yanaonyesha kazi shirikishi ya upatanisho na ya hakimu. {TN3: 15.1}

Sasa hadi hapa, tunaona kwamba wakati Yohana katika maono aliuona mlango — pazia — ilipokuwa ikifunguliwa hadi katika Patakatifu Mno pa hekalu la mbinguni, aliruhusiwa kutazama ndani, na kwamba mambo aliyoyaona, yangalitukia “hapo baadaye” kutoka kwa wakati wake; kuonyesha kwa hivyo kwamba wakati wa maono yake (karibu 96 B.K.) Patakatifu

15

Mno palikuwa pamefungwa. Kuongeza kwa hili, tutaona sasa kutoka kwa unabii wa Danieli kwamba kiti cha enzi cha hukumu kiliwekwa katika Patakatifu Mno pa hekalu la mbinguni baada ya “pembe ndogo” ya Danieli 7 kuinuka. {TN3: 15.2}

“Nikaziangalia sana pembe zake,” asema mwonaji, “na tazama, pembe nyingine ikazuka kati yao, nayo ilikuwa ndogo, ambayo mbele yake pembe tatu katika zile za kwanza zikang’olewa kabisa; na tazama, katika pembe hiyo mlikuwa na macho kama macho ya mwanadamu, na kinywa kilichokuwa kikinena maneno makuu. Nikatazama hata viti vya enzi vikawekwa, na Mmoja aliye Mzee wa siku ameketi; mavazi Yake yalikuwa meupe kama theluji, na nywele za kichwa Chake kama sufu safi; kiti Chake cha enzi kilikuwa miali ya moto, na gurudumu Zake moto uwakao. Mto kama wa moto ukatoka ukapita mbele Yake; maelfu elfu wakamtumikia, na elfu kumi mara elfu kumi wakasimama mbele Yake; hukumu ikawekwa, na vitabu vikafunuliwa.” Dan. 7:8-10. {TN3: 16.1}

Aya hizi hufichua kwamba baada ya hukumu kuwekwa, na vitabu vikafunuliwa,” “Mwana wa adamu,” Kristo, wakati huo “aliletwa” kwa nafasi mahali, si “kwa mkono wa kulia wa Mungu,” “Mzee wa siku, “ ila “karibu mbele” Yake (Dan. 7:8-10, 13). {TN3: 16.2}

Yote maono ya Yohana na Danieli yanafichua kwamba kiti cha enzi katika hekalu hakikuwapo tangu mwanzo wa uumbaji wa Mungu; au tangu siku za Musa; au bado kuanzia saa ambayo Kristo alipaa

16

juu; au hata kutoka siku za Rumi ya kipagani; kwamba, kwa kweli, hakikuwa “kimewekwa” mpaka baada ya kuanguka kwa Rumi ya kipagani, wakati “pembe ndogo” ya mnyama dubwana alipoinuka — katika siku za Rumi ya Upapa (Dan. 7:7-12, 21, 22). Kwingineko wala si katika hekalu, kwa hivyo, ni

Chumba cha Kiti cha Enzi cha Mungu cha Milele. {TN3: 16.3}

Kwa sababu kiti cha enzi cha hekalu hakikuwapo katika siku za kanisa la Kikristo la kwanza, kwa hivyo kiti cha enzi ambacho Stefano alimwona Kristo “mkono wa kulia wa Mungu” (Mdo. 7:56) hakikuwa katika hekalu, ambapo ipo “bahari ya kioo,” bali badala yake katika Paradiso, ambapo hutoka “mto wa maji ya uzima,” na kila upande ambapo kuna “mti wa uzima.” Ufu. 22:1, 2. Kwa hivyo, dhahiri sana, kiti cha enzi ambacho Stefano aliona ni “kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo,” kiti cha enzi cha kudumu na cha milele. Kuzunguka kiti hiki cha enzi cha utukufu hakuna wanyama, wala mashahidi, wala jopo, na mbele yake “hakuna taa,” na hakuna damu ya kutolewa dhabihu. Kwa ufupi, kinasimama, si katika hekalu lenye mizigo ya dhambi, ila katika Paradiso. Ni kiti cha Mwenye enzi cha utawala, ambacho Mungu hutawala milele viumbe Vyake visivyokufa wala kutenda dhambi! {TN3: 17.1}

Kwa kiti hiki cha enzi, basi, ambacho ni cha kutoka milele hata milele, Kristo alipaa na hapo akaketi kwa mkono wa kulia wa Baba Yake hadi wakati ulipofika ambapo, katika kutimiza unabii wa Danieli na ufunuo wa Yohana, wakati fulani baada ya utawala

17

wa pembe ndogo kuinuka, Yeye na Baba Yake walihamia kwenye kiti cha enzi cha hekalu. Juu ya cha mwisho Yeye haketi kama mfalme upande wa kulia wa Mungu; ila mbele Yake Yeye husimama kama mwana-kondoo wa dhabihu (Ufu. 5:6), na kama mwombezi (Dan. 7:13) akisihi kwa ajili ya wanadamu wadhambi. Hivyo, kazi Yake ya upatanisho ilianzia

Mwanzo Katika Patakatifu, Kisha Katika Patakatifu Mno. {TN3: 17.2}

Katika hekalu la duniani, kuhani mkuu (mfano wa Kristo) alihudumu kwanza katika patakatifu wakati wote kwa mwaka, kisha kwa siku ya Upatanisho, siku ya kilitakasa hekalu na kuwahukumu watu, alihudumu Patakatifu Mno kwa siku moja tu. Huduma hii mara mbili ina maana kwamba katika hekalu la mbinguni, Kuhani Mkuu, Kristo, lazima kwa sharti kwanza ahudumu katika patakatifu hadi siku ya uakisi ya Upatanisho, na katika siku hiyo, lazima ahudumu katika Patakatifu Mno, mbele ya kiti cha enzi. Hivi huduma za duniani, pia, zinakataa wazo kwamba Kristo aliingia Patakatifu Mno pa hekalu la mbinguni mara baada ya kupaa Kwake. {TN3: 18.1}

Wazi kabisa, basi, mfumo wa sherehe unaonyesha kwamba tangu wakati Kristo “alipoketi mkono wa kuume wa Mungu.” (Marko 16:19), ambapo kuna “mto wa maji ya uzima” hadi, wakati ambapo Yeye na Baba walihamia kwenye kiti cha enzi katika hekalu, ambapo “bahari ya kioo” ipo (Dan. 7: 9, 10; Ufu. 4.6), Yeye

18

alihudumu kwa ajili yetu kama kuhani mkuu katika “mahali patakatifu” (Ebr. 9:12); na wakati uo huo, kwa ushirika na Baba, juu ya kiti cha enzi cha utawala cha milele (“kiti cha enzi cha Mungu na cha Mwana-Kondoo”), Alitawala ulimwengu usiokuwa na dhambi. {TN3: 18.2}

Kutoka kwa kweli zilizotangulia, wazi na moja moja, hitimisho la pekee la kuthibitika la kuandikwa ni kwamba Kristo, mara baada ya kupaa Kwake, badala ya kuingia ndani ya pazia katika hekalu, aliketi mkono wa kuume wa Baba Yake, katika Paradiso na kutoka huko aliifanya kazi Yake katika patakatifu pa hekalu. {TN3: 19.1}

Dhahiri ilioje, tayari, nuru ya ukweli hatimaye inang’aa kwenye somo hili muhimu la wokovu ambalo kwa muda mrefu limefunikwa katika ukungu mnene wa dhana na makisio ya watu! Imara lililoje thibitisho la mwisho la Roho ya Unabii la kuthibitisha tena msimamo wake kwenye mada: “kwamba swali la patakatifu linasimama kwa haki na ukweli, sawa sawa kama tulivyofanya kwa miaka mingi.” — Watendakazi wa Injili, uk. 303. {TN3: 19.2}

“Basi msiutupe ujasiri wenu, kwa maana una thawabu kuu. Maana mnahitaji saburi, ili kwamba mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu mpate ile ahadi. Kwa kuwa bado kitambo kidogo sana, Yeye ajaye atakuja, wala hatakawia.” Ebr. 10:35-37. {TN3: 19.3}

“Basi, katika hayo tunayosema, neno lililo kuu ndilo hili: Tunaye

19

kuhani mkuu wa namna hii, Aliyeketi mkono wa kuume wa kiti cha enzi cha Ukuu mbinguni, mhudumu wa patakatifu, na wa ile hema ya kweli, ambayo Bwana aliiweka wala si mwanadamu.” Ebr. 8:1 {TN3: 19.4}

“Kwa sababu Kristo hakuingia katika patakatifu palipofanyika kwa mikono, ndio mfano wa patakatifu halisi; bali Aliingia mbinguni hasa, aonekane sasa usoni pa Mungu kwa ajili yetu.” Ebr. 9:24. Kwa kweli, “mara moja tu, katika utimilifu wa nyakati, amefunuliwa, azitangue dhambi kwa dhabihu ya nafsi yake. Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu.” (Ebr. 9:26, 27) — kutakaswa kwa patakatifu (Dan. 8:14). {TN3: 20.1}

Wazi wazi, kwa hivyo, hukumu itaanza na patakatifu kutakaswa, si kabla, lakini baada ya kutimizwa kwa kipindi cha wale walioteuliwa kufa. Kuhukumu kunavyopatana na rekodi zilizopatikana katika vitabu vya mbinguni, majina, kwa hivyo, ya wale wanaopatikana hawastahili, bila kujivika “vazi la harusi,” wanaondolewa kwenye vitabu. Hivi ndivyo patakatifu panatakaswa. Akizungumza kuhusu kuanza kwa kazi hii ya kuhukumu na kutakasa, malaika akamwambia Danieli: “Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa.” Dan. 8:14. {TN3: 20.2}

Ya kwamba kutakaswa, kwa hivyo kunatukia penye kikomo cha siku 2,300 na ni hivyo, kama ambavyo tumekwisha ona, hukumu,

20

ambayo inafanyika “katika mwisho wa dunia” (Ebr. 9:26), vile vile kikomo cha hizo siku, na kuanza kwa kazi ya upatanisho na ya uhakimu ya Kristo ni, kwa mamlaka ya Uvuvio Wenyewe, wakati mwafaka ulioteuliwa hadi mwisho wa Dunia. Hivyo, kwa kuondoa shaka, siku 2,300 hazikukoma katika siku za Antiochus Epiphanes, kama wengine wanavyofundisha. Msimamo huu haukubaliki juu ya mada hiyo, pamoja na maoni mengine yasiyoweza kutegemewa juu yake, kwa hivyo yanafanya kuwa lazima, ili kubainisha haswa tarehe ya kutakasa, kwanza

Kuondoa Mchafuko Kuhusu Siku 2,300. {TN3: 20.3}

Wale walio katika upinzani kwa fundisho kwamba siku 2,300 hupata kikomo chake katika mwisho wa dunia, wako, kati yao, kwa ubishi wa ukakawana juu ya lini siku, wanadhani, zinakoma, kama vile walivyo kwa ukweli wa umati wa mafundisho mengine. Dhahiri kabisa hata hivyo ni ukweli kwamba hakuna hata mmoja wao ana ukweli juu ya hiyo mada. Na bado licha ya unyeti wa ukweli huu, wanashindwa kuona kwamba roho ambayo imewaongoza katika hali yao ya sasa ya mfarakano, tofauti ya mafundisho, kubishana, na mchafuko, usiokuwa na kifani katika historia, hawezi kuwa Roho wa Kweli, Ambaye pekee yake anaweza kuwaongoza katika ukweli wa unabii wa siku 2,300. Kwa hivyo wanaendelea kutia giza himaya ya Ukristo kwa yale wanayodhani na kutangaza kwamba ni nuru juu yake. {TN3: 21.1}

Katika juhudi za kuunga msimamo wao,

21

huleta Septuagint, Vulgate, na Tafsiri ya Kiingereza Iliyosahihishwa. Hizi katika utaratibu uliotajwa kwa namna mbalimbali hutoa hesabu katika Danieli 8:14 kama 2,400, 2,200, na 2,300 “jioni asubuhi.” Tofauti hii peke yake ni ushahidi kamili kwamba fasiri hizo si matokeo sahihi, halisi ya kuifasiri hiyo aya; lakini badala yake ni mazao ya maelezo ya fasiri zake, zinazoletwa na mawazo yaliyozalishwa kitheolojia kwenye hiyo mada. {TN3: 21.2}

Hata hivyo, hata fasiri hizi jinsi zilivyo, zinatoa mapendezi dhaifu ya aina hii kutosha kwa nadharia zinazoshikiliwa kinyume na mafundisho ya kwamba siku 2,300 zinakoma katika mwisho wa dunia, kama kuwashurutisha wana nadharia kusoma Danieli 8:14 neno “dhabihu” ili kubadilisha “jioni asubuhi” awamu ya maandiko kusoma “kafara za jioni asubuhi.” Kisha, kwa misingi kwamba kulikuwa na dhabihu mbili kwa siku, wanagawanya idadi yazo kwa nusu. Na idadi hiyo kuwa 2,400, 2,200, au 2,300, kulingana na tafsiri ambayo wanatumia, hupata siku 1,200, 1,100, 1,150 kwa mtiririko! Hii kuongezea na mkato, wao kisha kwa ujasiri hutoa ushahidi wa nadharia yao! ingawa hakuna kuepuka maana safi kama kioo ya “jioni asubuhi” inapotazamwa katika nuru ya Mwanzo 1:5 ambayo, jinsi kila mwanafunzi wa Biblia anavyojua vyema, inaweza kumaanisha tu kipindi cha masaa 24 (usiku na mchana), na ambayo hayahusiani na ile dhabihu. {TN3: 22.1}

22

Wazi kabisa, kwa hivyo, tarakimu 2,400 na 2,200 na kutia katika Maandiko neno “dhabihu,” ni matokeo matupu ya ufasiri wa uongo wa unabii wa Danieli. Tofauti kati ya takwimu hizo mbili ni kwa sababu ya tofauti katika tarehe zinazohitajika ili kufanikisha mawazo tofauti kwa andiko. Akifunua wazi tamaa na hatima ya wale waliohusika na jaribio hilo tupu la kuweka utimilifu wa unabii, Bwana alimwambia Danieli: “wenye jeuri miongoni mwa watu wako watajiinua ili kuyathibitisha maono; lakini wataanguka.” Dan. 11:14. {TN3: 23.1}

Ingawa juhudi za wanyang’anyi hawa wa watu wa Mungu kuyafanya maono kufaa mawazo yao zimehukumiwa kushindwa, bado katika ujasiri wao wa kujitegemea kwa upofu wanajitahidi wawezavyo kuyaweka imara, hata kwenda umbali kwa juhudi za kuyafanya maandishi ya Josephus kunena kama historia takatifu ili kuunga mkono nadharia yao. {TN3: 23.2}

“Na hakika ilitimia hivyo,” asema mwandishi wa historia wa Kiyahudi, katika kifungu ambacho kwa kawaida wao hukitumia, “kwamba taifa letu liliteswa chini ya Antiochus Epiphanes, kulingana na maono ya Danieli na kile alichoandika miaka mingi kabla ya kutukia.” — Zamani za Kale, Kitabu 12, Sura ya 5. {TN3: 23.3}

Ijapokuwa Josephus hagusi kwa kusema au kuandika idadi ya siku zilizotajwa katika Danieli 8:14, bado kwa sababu yeye huyahushisha yale maono kwa kazi ya Antiochus Epiphanes,

23

kwa matokeo wao humchukua kama nabii aliyevuviwa kuyafasiri Maandiko! Akiwa mwana historia tu, na si nabii, yeye kwa hivyo, kwa kuandika historia ya Wayahudi, alifanya tu matumizi ya historia kwa hali ya kufanana aliyoiona kati ya unabii wa Danieli na kazi ya Antiochus. Na hivyo ilikuwa vizuri ndani ya jimbo lake kama mwana historia. Lakini kwamba hakuwa na karama ya unabii huwazuia watu wa Mungu kuyapokea matumizi yake ya Maandiko kama mamlaka na ya kutegemewa. {TN3: 23.4}

Kutokana na aina hii ya kupinda , kupotosha, kueleza kwa namna ya akili za binadamu, na kuondoa maana ya ukweli rahisi, msomaji mwadilifu ataona umbali ambao wanadamu wanakwenda ili kukwepa ukweli uliofunuliwa ambao hawapendi, na kukumbatia nadharia za kibinafsi kulingana na kupenda kwao. Hakika ni kweli msemo, “mpe mwanadamu nadharia na mambo yatakuja kwa wingi pamoja!” {TN3: 24.1}

Kwa kuuondoa ukungu wa makosa sasa, njia yetu ni safi kwendelea kuhakiki

Ni Lini Siku 2,300 Zinaanzia Na Kukoma. {TN3: 24.2}

Kutoka Danieli 7 ilionekana kuwa kiti cha enzi cha hukumu au cha kutakasa hakingewekwa hadi wakati fulani baada ya utawala wa pembe ndogo kuja kuwapo, ilhali kutoka Ebr. 9:24-27 ilionekana kingewekwa wakati fulani kabla ya “mwisho wa dunia.” Sasa ili kumulika kwa mtazamo kikamilifu nuru juu ya ukweli ambao tayari umeletwa, ni lazima twende kwa Danieli 8 na 11, kwa maelezo ya unabii wa ile mada– siku 2300. {TN3: 24.3}

24

Dan. 8:11, 12

“Naam, ikajitukuza hata juu yake aliye Mkuu wa jeshi hilo, ikamwondolea sadaka ya kuteketezwa ya daima, na mahali pa patakatifu Pake pakaangushwa chini. Na jeshi likatolewa kwake pamoja na sadaka ya kuteketezwa ya daima, kwa sababu ya makosa; nayo ikaiangusha kweli hata chini; ikatenda ilivyopenda, na kufanikiwa.” {TN3: 25.1}

Dan. 11:31

“Na wenye silaha watasimama upande wake, nao watapatia unajisi mahali patakatifu, ndiyo ngome, nao wataondoa sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, nao watalisimamisha chukizo la uharibifu.” {TN3: 25.2}

Kutoka kwa ulinganifu huu wa Danieli 8:11, 12, na Danieli 11:31, msomaji ataona kwamba maandiko yote yananena juu ya utawala mmoja. Na Kristo, akitabiri ishara za mwisho wa dunia, jinsi Alivyotazama mbele ya mkondo wa wakati, alitangaza: “Basi hapo [wafuasi Wake watakaokuwa wanaishi wakati ambao utawala wa pembe ulikuwa ukifanya kazi dhidi ya Mungu, ukweli Wake, na watu Wake] mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu), ndipo walio katika Uyahudi na wakimbilie milimani.” Mat. 24:15, 16. Maneno haya dhahiri ya Kristo Mwenyewe, huweka kazi ya utawala huu kwa wakati ujao kutoka wakati Wake. {TN3: 25.3}

Hapa Kristo anasema waziwazi kwamba wakati Wake chukizo la uharibifu halikuwa limesimama “mahali patakatifu,” ila kwamba

25

wakati fulani katika kipindi cha Kikristo utaonekana kusimama hapo. Tena zaidi, malaika alimwagiza Danieli kwamba mwanzoni mwa wakati wa mwisho itakuwa ile njozi (Dan. 8:13, 17). Kweli hizi mbili zinasheheni ushahidi unaotakasa kwamba kipindi cha siku 2300 hakingekoma mpaka, baada ya wakati wa Kristo, ya kila siku itupwe nje na machukizo kuanzishwa: maana matukio haya mawili yalipaswa kutimia ndani ya siku 2300. {TN3: 25.4}

Utawala huu wa uharibifu ulikuwa, kulingana na Danieli, utie unajisi kwa uasi patakatifu pa duniani, au kanisa. Hili lingetimizwa kwa kuiangusha Kweli chini, kwa kuondoa ya kila siku, na kwa kuingiza mahali patakatifu “chukizo la uharibifu,” yote ambayo yangekuwa, akasema malaika, “hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa.” {TN3: 26.1}

Kutoka kwa ushahidi mzito ambao umekusanywa hapa, lipo dhihirisho la hitimisho moja linalowezekana: kutia unajisi patakatifu, kukoma kwa siku 2300, na kutakaswa kwa patakatifu hakungeweza kutimia kabla ya wakati wa Kristo. {TN3: 26.2}

Kukabiliana na mwisho unaovuma wa hitimisho hili la mara tatu, sauti nyingi ambazo zinasisitiza kuzuilia ndani ya kipindi cha Agano la Kale matukio yanayofungamana na siku 2300, zinapaswa sasa kunyamaza kabisa na milele. Lakini kama

26

haziwezi, basi Mungu, pekee, anajua lile zitatangaza ijayo! {TN3: 26.3}

Hamwezi kumudu, ndugu zangu, sasa kwamba nuru imekuja, kuruhusu iponyoke kutoka kwenu fursa ya kuachana na nadharia za watu ambazo hapa ndani zimedunishwa na “Roho wa Kweli,” na kwa kuiweka miguu yenu imara juu ya msingi thabiti ambao umewekwa hapa mahali pake kwa ushuhuda wa Yesu Kristo. {TN3: 27.1}

Juu ya mwamba huu imara jengo la ukweli sasa linajengwa, kama msomaji ameweza kuona, litahimili dhoruba kali zaidi ya zote “pepo” na “mvua.” Kwa hivyo hebu, tukiendelea kuisimamisha miundo msingi yake bora, kwa kutumia maridhawa, bila hofu hata kidogo kwa dhoruba inayokuja (ambayo itabomoa na kufagilia mbali kila kitu kinachosimama kwa msingi wa mchanga), nyenzo zinazopeanwa bure: {TN3: 27.2}

Ili kutakasa patakatifu pa duniani, chukizo ambalo utawala katili ambao hapa unajadiliwa, ulileta ndani, lazima kwa sharti litupwe nje, halafu “ukweli,” pia “ ya kila siku,” ambayo utawala huo ulikanyagia chini na kutupa nje, lazima irejeshwe. Dhahiri kabisa, kwa hivyo, hakuna hata nafasi ya shaka ni jinsi gani ambayo patakatifu palitiwa unajisi au jinsi ambavyo ni lazima patakaswe. {TN3: 27.3}

Sura ya nane ya kitabu cha Danieli ina mfano halisi wa kinabii wa wanyama wawili (kondoo dume na beberu), kuhusiana nao

27

malaika alielezea: “Yule kondoo dume uliyemwona, mwenye pembe mbili, hizo ndizo wafalme wa Umedi na Uajemi. Na yule beberu, mwenye manyoya mengi, ni mfalme wa Uyunani; na ile pembe kubwa iliyo kati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.” Dan. 8:20, 21. {TN3: 27.4}

“… Na yule beberu akajitukuza sana; na alipokuwa na nguvu, pembe ile kubwa ilivunjika; na badala yake zikazuka pembe nne mashuhuri zilizoelekea pepo nne za mbinguni. Na katika moja ya pembe hizo ilitokea pembe ndogo, iliyokua sana, upande wa kusini, na upande wa magharibi, na upande wa nchi ya uzuri.” Dan. 8:8, 9. “na ile pembe kubwa iliyo kati ya macho yake ni mfalme wa kwanza.” — Alexander. “Tena katika habari ya pembe ile iliyovunjika, ambayo badala yake zilisimama pembe nne, falme nne zitasimama kutoka katika taifa lile, lakini si kwa nguvu kama zake.” — si katika uwezo wa Alexander; yaani, si “kwa uzao wake.” Dan. 8:21, 22; 11: 4. {TN3: 28.1}

“Na wakati wa mwisho wa ufalme wao, wakosao [Wayahudi] watakapotimia, mfalme mwenye uso mkali, afahamuye mafumbo, atasimama. Na nguvu zake zitakuwa nyingi mno, lakini si kwa uwezo wake mwenyewe [kwa “wenye silaha watasimama upande wake,” (Dan. 11:31) naye ataharibu kiasi cha kustaajabisha watu, na kufanikiwa, na kutenda apendavyo; naye atawaangamiza hao walio hodari na watu watakatifu. “ Dan. 8:23, 24. {TN3: 28.2}

Kwa hivyo basi, Danieli 8:22-24 ni sawa na Danieli 7:25: “Naye atanena

28

maneno kinyume chake Aliye juu, naye atawadhoofisha watakatifu wake Aliye Juu; naye ataazimu kubadili majira na sheria; nao watatiwa mikononi mwake kwa wakati, na nyakati mbili, na nusu wakati.” {TN3: 28.3}

[Picha ya Kondoo Dume na Beberu]

29

Danieli alipata maono akiwa Babeli, kaskazini mashariki ya “nchi ya uzuri” — Palestina. Kutoka Babeli ile pembe kubwa sana ilienda kwanza “kusini,” ijayo “mashariki,” kisha kaskazini ili kufanya mzunguko kuelekea magharibi — “kuelekea nchi ya uzuri.” Hivyo ilienda katika maelekeo yote manne, kuashiria kwamba ulikuwa utawala wa ulimwengu. Zaidi ya hayo, pia “shaba” ya sanamu kubwa ya Danieli 2, ambayo Danieli anaeleza “itakuwa na mamlaka juu ya dunia yote,” inawakilisha Uyunani. Hata hivyo, pembe ya kwanza ya mbuzi wala pembe zake nne zilizofuata hazikutawala dunia yote, basi kutimiza unabii wa ufalme wa shaba, pembe yake kubwa sana lazima iwe ambayo “itamiliki juu ya dunia yote.” Dan. 2:39. {TN3: 30.1}

Ijapokuwa mnyama wa nne wa Danieli 7 anaonyesha kwamba utawala huu wa uharibifu umetoka Rumi, kutumia mfano wa beberu unarejea nyuma zaidi ili kuonyesha kwamba utawala huu wa ulimwengu asili yake ulitoka katika mojawapo wa majimbo yaliyogawanyika ya Uyunani (Dan. 11:5), na baadaye kujivika vazi la Ukristo — dini ya “mungu ambaye baba zake hawakumjua.” Dan. 11:38. {TN3: 30.2}

Hatua kwa hatua akijitanguliza kwa mapambo ya patakatifu, kabla ya muda mrefu alijitukuza dhidi ya Mfalme (Kristo) wa jeshi (Wakristo). Na kwa kumpuuza “mungu wa baba zake,” kwa nje akawa Mkristo, lakini ni kwa gharama gani kwa Ukristo! — Si tu “ya kila siku” “iliondolewa,” bali pia “mahali pa

30

patakatifu Pake pakaangushwa chini.” Kwa maneno mengine, “aliangusha chini” mahali pa Bwana na hapo akaweka pake mwenyewe — akajiinua hadi kwa nafasi ya Kristo. {TN3: 30.3}

Neno “dhabihu” likiwa limewekwa kuhusiana na neno “ya kila siku,” ni bayana si sehemu ya maandiko hayo. Maadamu, hata hivyo, lugha ya Kiingereza haina neno halisi sawa na neno la Kiebrania “ya kila siku,” ambalo linafasiriwa kwa njia mbalimbali “ya mfululizo,” “daima,” “milele,” na kwa kuwa hakuna maneno kati ya haya ni visawe, ila hubeba sifa za kibinafsi , vile vile ni muhimu kuyachukua yote kama neno moja, ili kuufikia ukweli halisi. Kwa mtazamo, kwa hivyo, wa ukweli huu, pia ukweli kwamba fundisho la Sabato ndilo fundisho la Biblia la pekee katika enzi ya Kikristo ambalo laweza kutajwa kama “ya kila siku” (linalohusu ibada kwa heshima ya siku), pamoja na “mfululizo,” “daima,” na “milele,” — tangu zamani za kale hadi milele, — ni hapa dhahiri kwamba fasiri hizi zote haziwezi kutumika kwa fundisho lingine lolote kuliko Sabato — siku ya kupumzika ya milele. Na katika thibitisho la Mungu la umilele wake, huendelea kuvuma kwa karne nyingi kutoka Sinai kwa maneno yasiyotanguka: {TN3: 31.1}

“Kwa ajili ya hayo wana wa Israeli wataishika Sabato, kuiangalia sana hiyo Sabato katika vizazi vyao vyote, ni agano la milele. Ni ishara kati ya Mimi na wana wa Israeli milele; kwani kwa siku sita Bwana alifanya mbingu na nchi,

31

akastarehe kwa siku ya saba na kupumzika.” Kut. 31:16, 17. {TN3: 31.2}

Kwa hivyo ile pembe kuondoa “ya kila siku,” halikuwa lolote isipokuwa kuondoa katika kanisa la Kikristo Sabato ya Bwana na kuweka mahali pake ibada ya Jumapili, sabato ya kipagani, — “chukizo la uharibifu,” — uteuzi uliohuzunisha uwepo wa Mungu kuondoka kanisani. {TN3: 32.1}

Kondoo dume na beberu walionyeshwa kwa Danieli katika maono “mwaka wa tatu wa kumiliki kwake mfalme Belshaza.” Dan. 8:1. Danieli “naliyastajabia yale maono, ila hakuna aliyeyafahamu.” Dan. 8:27. Wakati, zaidi ya hayo, ulikuwa umepita, na Yerusalemu ulikuwa bado ni magofu. Kisha baadaye katika “mwaka wa kwanza wa Dario,” ambaye “alitawazwa kuwa mfalme juu ya milki ya Wakaldayo” (Danieli 9:1), Daniel alionyeshwa “kwa kuvisoma vitabu, nalifahamu hesabu ya miaka, ambayo neno la Bwana lilimjia Yeremia nabii, ya kuutimiza ukiwa wa Yerusalemu, yaani, miaka sabini.” Dan. 9:2. Yerusalemu, hata hivyo, ulikuwa bado magofu, ingawa wakati wa kutekwa kwa watu kulingana na unabii ulikuwa umetimia na maono bado “hakuna [hasha] aliyefahamu,” kama inavyoonekana wazi kutoka kwa sala ya Danieli: {TN3: 32.2}

“… Nikamwelekezea Bwana Mungu uso wangu, ili kutaka kwa maombi, na dua, pamoja na kufunga, na kuvaa nguo za magunia na majivu. Nikamwomba Bwana, Mungu wangu …. Ee Bwana

32

sawasawa na haki Yako yote, nakusihi, hasira Yako na ghadhabu Yako zigeuzwe na kuuacha mji Wako Yerusalemu, mlima Wako mtakatifu; maana kwa sababu ya dhambi zetu, na maovu ya baba zetu, Yerusalemu na watu Wako wamepata kulaumiwa na watu wote wanaotuzunguka. Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso Wako juu ya patakatifu Pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana….. {TN3: 32.3}

“Naam, nilipokuwa nikinena katika kuomba, mtu yule, Gabrieli, niliyemwona katika njozi hapo kwanza [katika sura ya nane], akirushwa upesi, alinigusa panapo wakati wa dhabihu ya jioni…. akasema,… Muda wa majuma sabini umeamriwa juu ya watu wako, na juu ya mji wako mtakatifu, ili kukomesha makosa, na kuishiliza dhambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya uovu, na kuleta haki ya milele, na kutia muhuri maono na unabii, na kumtia mafuta Yeye aliye mtakatifu. {TN3: 33.1}

“Basi ujue na kufahamu, ya kuwa tangu kuwekwa amri ya kutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu hata zamani zake Masihi aliye Mkuu; kutakuwa na majuma saba; na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu. Na baada ya yale majuma sitini na mawili, Masihi atakatiliwa mbali, Naye atakuwa hana kitu; na watu wa mkuu atakayekuja watauangamiza mji, na patakatifu; na mwisho wake utakuwa

33

pamoja na gharika, na hata mwisho ule vita vitakuwapo; ukiwa umekwisha kukusudiwa. Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo Ataikomesha sadaka na dhabihu; na mahali pake litasimama chukizo la uharibifu; na hivyo, hata ukomo, na ghadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu.” Danieli 9:3-27. {TN3: 33.2}

Malaika aligawanya wiki sabini katika vipindi vitatu: “majuma saba, na majuma sitini na mbili,” na “juma moja.” Na ingawa kwa maneno yake kwa Danieli, yaliyonukuliwa hapo juu, alifafanua wakati uliotabiriwa, lakini bado Danieli hakuelewa kikamilifu hayo maono. Kama alivyofanya hakika, hata hivyo, kuelewa ufafanuzi wa malaika wa “kondoo dume” na “beberu” ‘kuwa mfano wa “Uajemi” na “Uyunani” mtawalia, kazi ya ile “pembe kubwa sana” ndio kwa hivyo ambayo hakuelewa. Na hivyo ilikuwa kwamba baadaye “katika siku hizo,” alikuwa tena “akiomboleza;” wakati huu, “majuma matatu kamili.” Kwa hivyo anasema: {TN3: 34.1}

Nikaona “mtu aliyevikwa nguo za kitani, viuno vyake vimefungwa dhahabu safi ya Ufazi.… Ndipo akaniambia,… Sasa nimekuja kukufahamisha mambo yatakayowapata watu wako katika siku za mwisho; maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.” “kwa maana maono haya ni ya wakati wa mwisho.” Dan. 10:5, 12, 14; 8:17. {TN3: 34.2}

34

Kwamba sura ya 11 na ya 12 ziko na maelezo ya maono yaliyoahidiwa na malaika katika sura ya 10, yanaweza kutambuliwa kwa urahisi si tu kutoka kwa uendelevu wa hotuba ya malaika lakini pia kutokana na ukweli kwamba sura hizi ni maelezo ya maono katika sura ya nane. Kwa urahisi wa msomaji, tunanukuu aya mbili za mwisho za sura ya 10, na sehemu ya maelezo ya malaika yaliyoandikwa katika sura ya 11: {TN3: 35.1}

“Ndipo akasema, Je! Unajua sababu hata nikakujia? Na sasa nitarudi ili nipigane na mkuu wa Uajemi; nami nitakapotoka huku, tazama, mkuu wa Uyunani atakuja. Lakini nitakuambia yaliyoandikwa katika maandiko ya kweli; wala hapana anisaidiaye juu ya hao ila huyo Mikaeli, Mkuu wenu.” {TN3: 35.2}

“Tena mimi, katika mwaka wa kwanza wa Dario, Mmedi, mimi nalisimama nimthibitishe na kumtia nguvu. Nami sasa nitakuonyesha yaliyo kweli. Tazama, watasimama wafalme watatu katika Uajemi; naye mfalme wa nne atakuwa tajiri kuliko hao wote; naye atakapopata nguvu kwa utajiri wake, atawachochea wote juu ya ufalme wa Uyunani. Na mfalme hodari atasimama, atakayetawala kwa mamlaka kubwa, na kutenda apendavyo. Naye atakaposimama, ufalme wake utavunjika, na kugawanyika katika pepo nne za mbinguni; lakini hautakuwa wa uzao wake, wala hautakuwa kama mamlaka yake ambayo alitawala kwayo;

35

kwa maana ufalme wake utang’olewa, hata kwa ajili ya wengine zaidi ya hao.” Dan 10:20, 21; 11:1-4. {TN3: 35.3}

Ni dhahiri kwamba katika sura hii malaika anaelezea kwa undani “maono” ambayo yalionyeshwa kwa Danieli katika sura ya nane, na ya kwamba Danieli 8:11, 12 ni sambamba kwa wakati na Danieli 11:31. Ulinganifu wa maandiko yote, kama yanavyopatikana kwa ukurasa wa 25, unaweka wazi kwamba sura ya kumi na moja ni maelezo hasa ya utawala ambao unaonyeshwa na ile pembe kubwa zaidi ya sura ya nane. {TN3: 36.1}

Pia inaonyesha wazi kwamba patakatifu paliponenwa katika Danieli 8:11 hapawezi kuwa kingine chochote isipokuwa hekalu la Mungu: maana kwa upande mmoja, jengo la kipagani haliwezi kamwe kuwa na nguvu au kwa upande mwingine kutiwa unajisi wakati halijawahi kuwa safi. Na, zaidi ya hayo, Biblia kamwe haijawahi kuliita patakatifu. {TN3: 36.2}

Na, mwisho, ukweli ule kwamba hekalu huko Yerusalemu halikutiwa unajisi wala kutakaswa kwa namna ilivyoelezwa na malaika, ila liliachwa ukiwa na hatimaye kuharibiwa (Dan. 9:26), unaweka ushahidi wa kugongomea kwamba hakuna kutiwa unajisi au utakaso uliofanyika katika enzi ya Agano la Kale. {TN3: 36.3}

Hitimisho hili imara limefanywa maradufu haraka kwa sababu ya wema wa kauli ya Kristo (ukurasa wa 25), iliyoweka kazi ya utawala wa uharibifu katika kipindi cha Kikristo. {TN3: 36.4}

36

[Picha ya Siku 2,300]

Hakuna wakati mwingine isipokuwa “siku elfu mbili na mia tatu” (Dan. 8:14) na “majuma sabini” (Dan. 9:24),

37

ambao kauli hii inaweza kutumika, “wakati uliowekwa rasmi ulikuwa mrefu.” Dan. 10:1. Lakini kuona kwamba kipindi cha zamani kilikuwa muda mrefu sana kwa ajili ya kurejesha na kulitakasa hekalu huko Yerusalemu, na ya kwamba kipindi cha mwisho kilikuwa kirefu sana kwa ajili ya kuujenga tena mji (kwa maana miaka sabini iliyotajwa na Yeremia tayari ilikuwa imetimizwa), Danieli kwa haraka alimlilia Bwana kwa ajili ya ufahamu. {TN3: 37.1}

“Ndipo,” anasema, akiendelea , “nikamsikia mtakatifu mmoja akinena, na mtakatifu mwingine akamwuliza huyo aliyenena, Haya maono katika habari ya sadaka ya kuteketezwa ya daima, na lile kosa lifanyalo ukiwa, yataendelea hata lini, kukanyagisha patakatifu na jeshi? Akamwambia, Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa.” Dan. 8:13, 14. {TN3: 38.1}

Akielezea katika usemi wa kisasa, jibu la malaika kwa swali la Danieli litakuwa kwamba siku 2300 zitatakiwa kwa ajili ya “mahali pa patakatifu na jeshi kukanyagishwa chini.” pia kwa ya kila siku kuangushwa chini na kwa chukizo la uharibifu kusimamishwa, na ya kwamba baadaye patakatifu patatakaswa. {TN3: 38.2}

Katika nuru hii inaonekana kwamba kipindi cha siku 2300 lazima kimalizike baada ya “kila siku” kuondolewa na “chukizo la uharibifu” kusimamishwa. Hivyo kuondoa ya “kila siku “ na kuingiza “chukizo la

38

uharibifu” kwa uasi wa uharibifu, “patakatifu pa mahali pake pakaangushwa chini.” {TN3: 38.3}

Kulikanyagia chini jeshi ni kuwachinja Wakristo ambao hawakuabudu kulingana na maagizo ya utawala wa ile pembe. Kukanyagia chini patakatifu, kanisa, kuliruhusu kuanzishwa kwa ukuhani wa kidunia kuchukua nafasi ya Kristo, Ambaye anahudumu ndani ya hekalu la mbinguni. {TN3: 39.1}

Na vile pembe kubwa ya yule beberu ni mfano wa Rumi (chuma — Dan. 2:40) dunia katika awamu zake tatu, — ya kipagani, ya kipapa, na ya uprotestanti, — pia jinsi katika kipindi chake cha pili, ilikanyagia ukweli na “jeshi” chini ya mguu na kulitia unajisi hekalu kwa kuleta ndani machukizo wakati “ikatenda ilivyopenda, na kufanikiwa.” (Dan. 8:12), kipindi cha siku 2300, vile vile, hutambaa hadi baada ya kuanguka kwa Rumi ya Upapa na kufika katika kipindi cha Uprotestanti. {TN3: 39.2}

Zaidi ya hayo, amri ya kuujenga upya Yerusalemu ilitolewa katika 457 K.K. (Ezra 7:21-27), hatua ya mwanzo wa majira ya wiki sabini huthibitisha kwamba ni moja na ile ya siku 2300. {TN3: 39.3}

Na kuzuilia ukasisi wa Kristo ndani ya kipindi hiki, malaika akasema: “Naye [Kristo] atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na kwa nusu ya juma hiyo Ataikomesha sadaka na dhabihu.” Dan. 9:27. {TN3 39.4}

39

Kwa sababu kulithibitisha agano na watu wengi (Wayahudi) kulitimizwa katika miaka saba tangu mwanzo wa ukasisi wa Kristo, wakati wa ubatizo Wake, hadi wakati ambapo Petro aliagizwa kupeleka Injili kwa watu wa Mataifa (Mdo. 10:28; soma sura yote), na tangu katikati ya kipindi hiki Kristo alisulubiwa, “juma” linathibitishwa kuwa miaka saba halisi, na inaonyesha kwamba kipindi cha siku 2300 lazima kihesabiwe kwa kanuni ya Ezekieli 4, kuhesabu siku kuwa mwaka, hivyo: {TN3: 40.1}

“… tangu kuwekwa amri [iliyopatikana katika Ezra 7:21-27] ya kuutengeneza na kuujenga upya Yerusalemu [mwanzo wa siku 2300], hata zamani zake Masihi aliye Mkuu [kwa Kristo wakati wa ubatizo Wake], kutakuwa na majuma saba [miaka 49], na katika majuma sitini na mawili utajengwa tena pamoja na njia kuu zake na handaki, naam, katika nyakati za taabu. [miaka 434],” jumla ya miaka 483, pamoja na majuma saba ya kwanza au miaka arobaini na tisa, kwa ajili ya kuujenga upya mji huo. {TN3: 40.1}

Kisha baada ya “majuma saba” pamoja na “majuma sabini na mbili [Masihi] atakataliwa mbali,… na watu wa mkuu [Warumi] atakayekuja watauangamiza mji na patakatifu [ulitimizwa na Tito mwaka wa 70 B.K.]; na mwisho wake utakuwa na gharika, na mwisho wa vita uharibifu umekusudiwa. Na Yeye [Kristo] atalithibitisha agano na watu wengi kwa juma moja [miaka saba, kuanzia ubatizo Wake]:

40

na katikati ya juma [katikati ya miaka saba] Atasababisha kafara na sadaka kukoma [kwa kafara ya Nafsi Yake na kwa uhamisho wake hadi katika hekalu la mbinguni: Kafara Yake ikichukua kafara ya duniani , na hivyo hekalu la mbinguni linachukua nafasi ya hekalu la duniani, pamoja na Kristo Mwenyewe akiwa ni kuhani mkuu], na kwa kuenea kwa machukizo Yeye atalifanya [hekalu la Yerusalemu] ukiwa [uwepo Wake kuondolewa kabisa], hata mpaka utimilifu, na gadhabu iliyokusudiwa imemwagwa juu yake mwenye kuharibu.” Dan. 9:25-27. {TN3: 40.2}

Salio la siku 2300, au miaka, linafikia wakati wa kupatakasa patakatifu. (Tazama kielelezo katika ukurasa wa 37.) {TN3: 41.1}

Kuhesabu umbele miaka 2300 kutoka Oktoba 457 K.K., kikomo ni Oktoba 1844 B.K. Na jinsi malaika alisema, “Hata nyakati za jioni na asubuhi elfu mbili na mia tatu; ndipo patakatifu patakapotakaswa,” utakaso lazima ulianzia hapo 1844, hasa mwaka ambao kwa mara ya kwanza katika historia, ujumbe wa malaika wa kwanza ulitangazwa: “Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu Yake imekuja.” (Ufu. 14:7, Dan. 7:9, 10) — wakati ambapo Jaji Mkuu na mahakama ya mbinguni wanakaa katika hukumu kutenga wabaya kutoka kwa wazuri; yaani, kuondoa katika Kitabu cha Uzima majina ya

41

wale ambao wameingia huduma ya Kristo lakini hawakuvumilia hadi mwisho. {TN3: 41.2}

Kwa sababu ukweli huu wa kutisha, ulivyofunuliwa hapa, unapata pacha wake katika mfano wa Kristo wa ngano na magugu, mifano hiyo lazima kwa hivyo ifundishe ya upelelezi

Hukumu Miongoni mwa Walio Hai. {TN3: 42.1}

“Viacheni vyote vikue,” amri ya Kristo, kuhusiana na kuchangamana kwa ngano na magugu, “hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno Nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani Mwangu.” Mat. 13:30. {TN3: 42.2}

Hapa Bwana anafundisha kwa mfano kuwa wakati wa upelelezi utakuja, na ya kwamba hatimaye malaika watawaondoa wadhambi kutoka “katika kusanyiko la wenye haki.” Zab. 1:5 {TN3: 42.3}

“Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna; hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa. Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki.” Mat. 13:47- 49. {TN3: 42.4}

Katika mifano hii yote miwili, Kristo anavumisha onyo la kimbele kwamba hukumu

42

ya upelelezi itafanyika katika wakati unaoitwa “mavuno,” ambao ni mwisho wa dunia — wakati ambapo siku 2300 zitakapokoma, jinsi malaika alivyotangaza: “Fahamu, Ee mwanadamu, kwa maana maono haya ni ya wakati wa mwisho.” Dan. 8:17. “… yafunike maono hayo; maana ni ya wakati ujao baada ya siku nyingi.” Dan. 8:26. “… maana maono hayo ni ya siku nyingi bado.” Dan. 10:14. {TN3: 42.5}

Akionyesha moja kwa moja hadi wakati ambapo hukumu ya upelelezi itafanyika miongoni mwa walio hai, Malaki analinganisha mifano yote katika unabii wake: {TN3: 43.1}

“Angalieni, namtuma mjumbe Wangu, naye ataitengeneza njia mbele Yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu Lake ghafla; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi. Lakini ni nani atakayestahimili siku ya kuja Kwake? Au ni nani atakayesimama atakapoonekana Yeye? Kwa maana Yeye ni mfano wa moto wa mtu asafishaye fedha, ni mfano wa sabuni ya mtu afuaye nguo; Naye ataketi kama asafishaye fedha na kuitakasa, Naye atawatakasa wana wa Lawi, atawasafisha kama dhahabu na fedha; nao watamtolea Bwana dhabihu katika haki.” Mal. 3:1- 3. {TN3: 43.2}

Kwa sababu utakaso unaotajwa katika mifano na katika unabii wa Malaki haujawahi kutukia, hukumu ya upelelezi ya walio hai ni dhahiri, basi, bado ni wa baadaye. Kazi hii ya upelelezi kwa hivyo ni ya tukio la kazi ya kutenganisha katika hekalu la duniani (kanisa), jinsi inavyoletwa kwa mtazamo pia katika Ezekieli 9: {TN3: 43.3}

43

“Kisha akalia kwa sauti kuu masikioni mwangu, akisema, waamuru wale wanaousimamia mji wakaribie, kila mmoja na awe na kitu chake cha kuangamiza mkononi mwake. Na tazama, watu sita wakaja, wakitokea kwa njia ya lango la juu, lielekealo upande wa kaskazini, kila mmoja ana kitu chake cha kufisha mkononi mwake; na mtu mmoja kati yao amevaa bafta, naye ana kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. Wakaingia, wakasimama karibu na madhabahu ya shaba. Na huo utukufu wa Bwana wa Israeli ulikuwa umepanda juu kutoka kwa kerubi, ambaye ulikuwa juu yake, mpaka kizingiti cha nyumba; akamwita mtu yule aliyekuwa amevaa bafta, mwenye kidau cha wino cha mwandishi kiunoni. Bwana akamwambia, Pita kati ya mji, kati ya Yerusalemu, ukatie alama katika vipaji vya nyuso vya watu wanaougua na kulia kwa sababu ya machukizo yote yanayofanyika kati yake.” {TN3: 44.1}

“Na hao wengine aliwaambia, nami nalisikia, Piteni kati ya mji nyuma yake, mkapige; jicho lenu lisiachilie, wala msione huruma; Waueni kabisa, mzee, na kijana, na msichana, na watoto wachanga, na wanawake; lakini msimkaribie mtu ye yote mwenye hiyo alama; tena anzeni katika patakatifu Pangu. Basi, wakaanza kwa wazee waliokuwa mbele ya nyumba.”Ezek. 9:2-6. {TN3: 44.2}

Hapa watu wanaonyeshwa kwamba katika hali ya mchanganyiko (magugu na ngano pamoja), na wakati ulio mbele yao ambapo kwa upande mmoja wale ambao wameugua na kulia dhidi ya machukizo kati yao watapokea alama ya ukombozi, ilhali kwa upande mwingine wale ambao

44

hawajaugua na kulia wataachwa bila alama, kuangamia (katika dhambi zao) chini ya vyombo vya kufisha vya malaika. {TN3: 44.3}

Kutoka kwa utengo huu — ule wa ndani ya kanisa — wanatokea malimbuko. {TN3: 45.1}

Kisha unafuata utengo kutoka kati ya mataifa, jinsi inavyoonekana katika mfano wa Mathayo 25, kwa kinabii kuelezea ujio wa Kristo, ingawa si ule unaotazamwa katika 1 Thes. 4:16, 17, maana kwa wakati wa ujio wa mwisho, “nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani” ilhali kwa wakati wa awali, “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu Wake, na malaika watakatifu wote pamoja Naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu Wake [kanisa la ufalme, ambalo hadi wakati huo linajumuisha tu malimbuko] {TN3: 45.2}

“Na mataifa yote watakusanyika mbele Yake; Naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; Yeye atawaweka kondoo mkono Wake wa kuume, na mbuzi mkono Wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono Wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba Yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu…. Kisha atawaambia na wale walio mkono Wake wa kushoto, Ondokeni Kwangu, mliolaaniwa, mwende

45

katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake.” Mat. 25:31-34, 41. {TN3: 45.3}

Kutoka kwa utengo huu — ule wa ndani ya mataifa — wanatokea mavuno ya pili. {TN3: 46.1}

Malaika ambao wanakizunguka kiti cha enzi katika hekalu la mbinguni wakati wa hukumu ya Danieli 7:9, 10 na Ufunuo 5:11, jinsi mifano inavyoelezea, watashuka pamoja na “Mwana wa Adamu” wakati Anakuja “kwa hekalu Lake” (kanisa Lake) kutenganisha kwa hukumu “waovu kutoka kati ya wenye haki,” na atawasafisha kama dhahabu na fedha “Lakini ni nani atakayestahimili siku ya kuja Kwake…. nao watamtolea Bwana dhabihu katika haki.” Mal. 3:2, 3. {TN3: 46.2}

Katika onyesho la mchoro kwamba Atakuja kwa dunia pamoja na malaika Zake wote kutekeleza hukumu kwa walio hai, Bwana alijifunua Mwenyewe kinabii kwa Ezekieli akiletwa kama aliyeketi juu ya kiti cha enzi kwa dunia na viumbe hai wanne mara tu kabla ya mchinjo wa wanafiki ndani ya kanisa kutukia. Na kama vile kila kiumbe hai kina uso wa simba, uso wa ndama, uso wa mwanadamu, na uso wa tai (Ezek. 1:10), — nembo sawa na ya mahakama kama walivyo wanyama ambao wako mbele ya kiti cha enzi katika hekalu la mbinguni (Ufu. 4:7) wakati wa hukumu ya walio kufa, — na wakati wanashuka kwa dunia, wao hivyo kimfano wanaonyesha kwamba kazi ya kiti cha enzi ya upatanisho-ya hukumu ambayo inaitisha kikao

46

na kutawala hukumu ya walio kufa inapanuliwa hadi duniani. {TN3: 46.3}

Upanuzi huu, hadi hapa jinsi tumeweza kujua sasa, lazima utukie kwa ufunguzi wa muhuri wa saba (Ufu. 8:1), maana kwa wakati huo sauti za mbinguni, ambazo zilifungua hukumu ya walio kufa, zinanyamaza katika hekalu la mbinguni na kuanza, baada ya ukimya wa nusu saa, kuvuma duniani. Kwa maneno mengine, kama vile mbinguni kwa wakati wa ufunguzi wa hukumu ya wafu, kulikuwa na “umeme na sauti na ngurumo” (Ufu. 4:5), vivyo hivyo duniani wakati wa ufunguzi wa “hukumu ya walio hai,” “kuna kukawa radi na sauti na umeme na tetemeko la nchi.” Ufu. 8:5. {TN3: 47.1}

Kwa hukumu ya walio kufa, hata hivyo, kazi ya utengo hutukia vitabuni katika hekalu la mbinguni; ilhali kwa hukumu ya walio hai, utengo hutukia kati ya watu kanisani na kati ya majina yao ndani ya vitabu katika hekalu la mbinguni, hivyo kuonyesha kwamba hekalu zote mbili zitatakaswa mwishowe. {TN3: 47.2}

Bila shaka, kwa hivyo, ujio wa Bwana kwa Hekalu Lake (Mal. 3:1-3), kuja Kwake pamoja na malaika Zake wote (Mat. 25), na kuja Kwake akiwa ameketi kwa kiti cha enzi juu ya viumbe hai (Ezek. 1), — wote tatu unawakilisha tukio lile lile jinsi ambavyo limeonyeshwa, — kutukia mwanzoni mwa hukumu ya walio hai: wakati ambapo shughuli za mahakama za hekalu la mbinguni

47

zinapanuliwa hadi kwa patakatifu pa duniani — kanisa. {TN3: 47.3}

“Kisha nikaona, na tazama, wingu jeupe,” akapaaza sauti Yohana Waufunuo akiwazia ujio ule ule ulioelezwa Malaki, Mathayona Ezekieli, “na juu ya wingu hilo ameketi Mmoja, mfano wa Mwanadamu, mwenye taji ya dhahabu juu ya kichwa Chake, na katika mkono Wake mundu mkali. Na malaika mwingine akatoka katika hekalu, akimlilia kwa sauti kuu Yeye aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu, Tia mundu Wako, ukavune; kwa kuwa saa ya kuvuna imekuja; kwa kuwa mavuno ya nchi yamekomaa. Na Yeye aliyeketi juu ya wingu akautupa mundu Wake juu ya nchi, nchi ikavunwa.” Ufu. 14:14-16. {TN3: 48.1}

Ujio huu wa Mwana wa Adamu ni wazi, kwa hivyo, si kwa wakati ule waliofufuliwa na watakatifu walio hai wananyakuliwa pamoja kukutana Naye angani: maana aya za 17-20, zinazofuata zile ambazo zimenukuliwa katika aya ya hapo juu, hufunua kwamba baada ya Yeye kuja na kuvuna nchi, “malaika mwingine…mwenye mundu mkali” alikuja na kuvuna mavuno ya pili kabla ya ghadhabu ya Mungu — mapigo saba ya mwisho (Ufu. 15:1) — kumwagwa kwa waovu. {TN3: 48.2}

Hivyo tena na kwa mara ya nne inaonekana kwamba upo ujio mara mbili tofauti wa Mwana wa adamu: mmoja wa “kuwatenga waovu kutoka kati ya wenye haki” kanisani (Mat. 13:49), na kisha hala hala kuwaita wenye haki kutoka miongoni mwa waovu

48

Babeli (Ufu. 18:4); ule mwingine kuwapeleka watakatifu, waliofufuliwa na walio hai, hadi kwa majumba ambayo Yeye amewaandalia (1 The. 4:16; Yoh. 14:1-3). {TN3: 48.3}

Wakati wa ujio wa kwanza wa Mwana wa Adamu, jiwe lililoipiga sanamu kubwa lilichongwa bila mikono (bila msaada wa mwanadamu, na Bwana Mwenyewe) kwa sababu, jinsi Bwana husema, “Nikatazama, wala hakuna wa kusaidia; Nikashangaa kwa kuwa hakuna mwenye kutegemeza; Basi, mkono Wangu Mwenyewe uliniletea wokovu, Ghadhabu Yangu ndio iliyonitegemeza. Nikazikanyaga kabila za watu kwa hasira Yangu, Nikawalevya kwa ghadhabu Yangu, Nami nikaimwaga damu yao chini.” Isa. 63:5, 6. {TN3: 49.1}

Kazi hii ya utengo, au utakaso, ilioletwa kwa mtazamo katika mfano wa Mathayo 13:30 na tena katika ule wa Mathayo 13:47-49, pia katika unabii wa Malaki 3:1-3 na unabii wa Ezekieli 9, kama vile katika Ufunuo 14, inahusu moja kwa moja siku ya hukumu kwa walio hai; lakini kupatakasa patakatifu mwishoni mwa siku 2300 kwa mujibu wa Danieli 8:14 na Danieli 7:9, 10 kunahusu moja kwa moja

Hukumu Kati ya Wafu. {TN3: 49.2}

Ingawa kupatakasa patakatifu, jinsi tayari tumeona kutoka kwa unabii wa Danieli kungetukia baada ya 1844 B.K., lakini kwa vile wenye haki walio hai bado wamechangamana na wadhambi kanisani, na jinsi Danieli alimwona Mzee

49

wa siku aliketi katika hukumu, si kuwachinja wale waliokuwa na “alama,” ila kuhukumu kutoka kwa “vitabu” ambavyo “vilikuwa vimefunuliwa,” ni dhahiri maono yake ya hukumu inahusiana na wafu. {TN3: 49.3}

Kuhusu utakaso wa kanisa kwa dunia, ni lazima kwanza kutafanikishwa kwa kulitupa nje chukizo, pili kurejesha ukweli, na tatu kuyaondoa magugu. Lakini kuhusu kulitakasa hekalu mbinguni, sasa kunafanikishwa kwa kuondoa katika Kitabu cha Uzima majina ya wale wanaopatikana hawastahili; kisha kuyaweka katika kitabu chenye majina ya wale watakaokuja katika ufufuo wa waovu baada ya miaka elfu (Ufu. 20: 5); hivyo kuacha katika Kitabu cha Uzima majina ya wale tu ambao wamepata ushindi kwa dhambi, na ambao hivyo wanasubiri kuja katika ufufuo wa wenye haki (Ufu. 20:6). Yohana, basi, “Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunuliwa; na kitabu kingine kikafunuliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao.” Ufu. 20:12. {TN3: 50.1}

Zaidi ya sababu ambazo tayari zimetolewa, bado zipo

Sababu Zaidi Kwa Hukumu Zote Mbili. {TN3: 50.2}

Kwa sababu utakaso wa hekalu la mbinguni ni kazi ya kuvitakasa vitabu kwa

50

kufuta kutoka kwavyo majina ya wote waliokengeuka na magugu, na kama kwa “wakati wa taabu, mfano wake haukuwapo tangu lilipoanza kuwapo taifa hata wakati uo huo,” wale tu “watakaookolewa” ni wale ambao majina yao yatapatikana yameandikwa katika kile kitabu, utakaso wa vitabu, kwa hivyo, unaonekana wazi unafanyika kabla ya ufufuo, na kabla ya wakati wa taabu mfano wake haukuwapo. Hivyo wafu wasiokuwa waaminifu wataachwa katika makaburi yao wakati wa ufufuo wa kwanza, na walio hai wasiokuwa waaminifu wataachwa bila kuokolewa kutoka kwa taabu inayokuja. Lakini majina yao yangeruhusiwa kusalia katika vitabu, basi kwa mujibu wa kumbu kumbu aidha waovu waliokufa wangepaswa kufufuliwa pamoja na watakatifu, na waovu walio hai kuokolewa pamoja na watakatifu walio hai au vinginevyo wote watakatifu waliokufa na watakatifu walio hai watapaswa kuachwa pamoja nao — badala zote mbili ambazo, bila shaka, haiwezekani; hivyo tena kufanya wa lazima utengo tofauti kabisa, kama ulivyo katika mfano katika wakati wa Yoshua: {TN3: 50.3}

“Kitu kilichowekwa wakfu,” akasema Bwana, “kiko katikati yako, Ee Israeli; huwezi kusimama mbele ya adui zako, hata mtakapokiondoa kile mlicho nacho kilichowekwa wakfu….Kisha Yoshua, na Israeli wote pamoja naye, wakamtwaa Akani….na vitu vyote alivyokuwa navyo….Ndipo Israeli wote wakampiga kwa mawe.” Yos. 7:13, 24, 25. {TN3: 51.1}

Kutoka kwa ushahidi huu imara kuthibitisha utakaso wa kanisa duniani

51

na vitabu vikiwa mbinguni, hutokeza mnara wa ukweli usioweza kupenywa kwamba walio hai ambao, wanaendelea kwa uaminifu hadi mwisho, wanahifadhi majina yao katika Kitabu cha Uzima, wakati huu wa utengo, watapata alama ya Mungu, au muhuri, wa ukombozi, ilhali wale ambao hawataweza wataachwa bila muhuri, kuangamia katika dhambi zao. Na, vivyo hivyo, wafu ambao majina yao yamehifadhiwa baada ya hukumu, katika kitabu cha wafu, watatokea katika ufufuo wa kwanza (Ufu. 20:6), wakati wale ambao hawakuwa waaminifu katika maisha wanasubiri hadi baada ya miaka elfu, kutokea pamoja na waovu wote katika ufufuo wa pili (Ufu. 20:5). {TN3: 51.2}

Hivyo wakati ni muhimu katika kongamano la wafu kuwatenga waovu kutoka kwa watakatifu sasa wanaosubiri asubuhi ya ufufuo, ni muhimu tu katika kongamano la walio hai kuwatenga waovu kutoka kwa watakatifu sasa wakijiandaa kwa ukombozi kutoka kwa taabu inayokuja, na kungojea ujio wa pili wa Kristo — Kuja Kwake akionekana kuwaamsha watakatifu waliolala na kuwapeleka juu wote na walio hai. {TN3: 52.1}

Kwa hivyo ipo mitengo miwili, mmoja kati ya watakatifu waliolala na mwingine kati ya watakatifu walio hai, wafu wanaochaguliwa kwa ufufuo na walio hai kwa kuhamishwa bila kufa. {TN3: 52.2}

Wale, kwa upande mwingine, ambao majina yao yatafutwa kutoka vitabuni ni wale ambao watakuwa wameshindwa kujivika “vazi la

52

harusi.” Mat. 22:11 Kwa amri ya Bwana (Mat. 22:13), watatupwa nje, wala kamwe hawatakuwa kati ya wageni wa harusi. {TN3: 52.3}

Utakaso huu wa Kitabu cha Uzima unaonekana zaidi kuwa ni muhimu ili kuwawezesha malaika kuwachagua kwa usahihi watakatifu, kwa maana wakati Mwana wa adamu anapokuja pamoja na malaika Zake wote, atawatuma nao “watawakusanya wateule wake [waliofufuliwa] toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.” (Mat. 24:31), na kuwapeleka kujiunga na walio hai. {TN3: 53.1}

Nuru thabiti sasa inaangaza kutoka kwa unabii ambao hapa ndani umetazamwa katika uwiano wake unaohusiana, unaonyesha kwamba hekalu la mbinguni na lile la duniani yalitiwa unajisi, si kwa ushindi wa kisiasa na kijeshi wa tawala za wapagani, ila bali kwa, kwanza, na baadhi ya waongofu wake ‘hawakuvumilia hata mwisho (Mat. 10:22); pili na Shetani kuleta magugu watu walipolala (Mat. 13:25); na tatu, na pembe kubwa sana kutupa nje “ya kila siku,” ikikanyagia chini ukweli, na kuleta ndani chukizo la uharibifu: hivyo kuyahusisha yote mahekalu la duniani na la mbinguni. {TN3: 53.2}

Ufunuo huu wa kushangaza unaonyesha wazi kwamba utakaso kwa mujibu wa Danieli 8:14 ni kwanza kwa hekalu la mbinguni, na pili kwa hekalu kwa dunia. {TN3: 53.3}

53

Muhimu jinsi ilivyo, yeyote atakayeshindwa kufanya utafiti wa bidii na makini wa asili na maana ya kazi hii kuu ya Mungu kuwapeleleza wageni ambao wamekuja ndani kwa ajili ya harusi wao ni wa kutojali tu matarajio ya uzima wa milele — “wokovu mkuu sana.” Kwa maana hukumu ya mtu inapokuwa inangoja, na hujui ukweli wake, hatakuwa amejiandaa na kutoweza kusimama wakati kesi yake inapelelezwa. Kwa somo hili la umuhimu wote “Kwa hivyo imetupasa kuyaangalia zaidi hayo yaliyosikiwa tusije tukayakosa.” Ebr. 2:1. Na katika kufanya hili, lazima tuijongee hukumu

Katika Nuru Ya Mifano. {TN3: 54.1}

Mpanzi, mbegu, shamba, msimu wa kutayarisha na kukuza, na msimu wa mavuno lazima yakadiriwe pamoja kwa ukamilifu kuonyesha ufalme wa kiroho; vinginevyo uwakilishi unaweza tu kuongoza katika kosa badala ya ndani ya ukweli. {TN3: 54.2}

Misimu minne ya mwaka yote inahitajika kukamilisha mchakato wa kupanda, kukuza, na kuvuna mazao ya mwaka, na Vuli ikiwa mwanzo wa mwaka wa kilimo (kama vile mwisho wa msimu wa majira ya hari ni “sikukuu ya kukusanya ndani, ambayo ikatika mwisho wa mwaka, utakapokuwa umekusanya hayo uliyoyataabikia shambani. — Kut. 23:16), mfano huu kwa hivyo huonyesha kwa miezi kumi na miwili ya mwaka kipindi cha historia ya injili, katika kufungwa kwake ambapo ufalme wa Kristo utaanzishwa, na mwanzo wake ni

54

Wakati wa kupanda Mbegu. {TN3: 54.3}

Kwa kuwa kipindi cha historia ya kanisa kimeonyeshwa na hiki kipindi cha mavuno cha miezi

[Chati: Mavuno, Mathayo 13]

55

kumi na mbili, basi lazima tutafute wakati wa mwanzo wake — wakati wa kupanda mbegu, na wakati wa kufunga kwake — wakati wa mavuno. {TN3: 55.1}

“Azipandaye zile mbegu njema,” asema Kristo, “ni Mwana wa Adamu,” na adui aliyepanda magugu ni “Ibilisi.” Mat. 13:37, 39. {TN3: 56.1}

“Mwana wa Adamu,” Yeye “aliyepanda mbegu njema,” ni kweli si mwingine isipokuwa Kristo. Lakini kama hangeweza kuitwa “Mwana wa adamu” kabla ya kuzaliwa na mwanamke, Yeye kwa hivyo hangeweza kuwa amepanda “mbegu njema” ya mavuno ya kiroho hadi baada ya kuzaliwa Kwake Bethlehemu, Yudea. {TN3: 56.2}

Kwa sababu ukasisi Wake — Kwake kupanda ile “mbegu njema,” ukweli — ulianza mara baada ya kubatizwa Kwake (Mat. 4:17), kwa hivyo kuweka mwanzo wa kipindi cha mavuno ya kimfano, lazima tuhakiki tarehe ambayo Yeye alibatizwa. {TN3: 56.3}

“Na baada ya yale majuma sitini na mawili,” alitabiri Danieli, kuhusu ukasisi wa Kristo na kifo Chake, “Masihi atakatiliwa mbali, Naye atakuwa hana kitu…. Naye atafanya agano thabiti na watu wengi kwa muda wa juma moja; na katikati ya juma hilo Yeye ataikomesha sadaka na dhabihu.” Dan. 9:26, 27. {TN3: 56.4}

Kwamba huu ni muda wa kinabii, umehesabiwa kwa kanuni ya mwaka-siku ya Ezekieli 4:6, unaonekana kutoka kwa ukweli kwamba kulikuwa na miaka saba

56

tangu wakati Kristo alipobatizwa hadi wakati mitume waliruhusiwa kuipeleka Injili kwa Mataifa. Katika kipindi hiki, Kristo alithibitisha au alitimiza agano. “Katikati ya juma,” au mwishoni mwa miaka mitatu na nusu moja, Alipaswa kusulubiwa, na hivyo kusababisha kafara ya patakatifu pa duniani kukoma. {TN3: 56.5}

Ukweli ukiwa umewekwa (tazama mchoro kwa uk. 55) kwamba miaka mitatu na nusu moja ya ukasisi wa Kristo ilikoma siku ya 16 ya mwezi wa kwanza kisha kuhesabu miaka mitatu na nusu moja (fuata mchoro kwa uk. 55), tunaona kwamba ubatizo Wake ulifanyika siku ya 16 ya mwezi wa saba uliokuwa katika juma la Vibanda, na sikukuu ambayo ilikuwa mwisho wa mwaka wa kilimo, kufunga mavuno (Law. 23:39). {TN3: 57.1}

Kwa hivyo tunaona kwamba mfano huu u katika uwiano amini kwa maumbile, na ya kwamba “Mwana wa adamu” alianza kupanda mbegu ya kiroho kwa wakati sahihi — katika mwisho wa ya zamani na katika mwanzo wa mavuno ya mwaka mpya — kwa usahihi msimu sahihi wa mwaka. Upanzi wa mbegu ulianza na ubatizo wa Kristo na mavuno yanapokuja kwenye “mwisho wa dunia,” kipindi cha mfano huo ni dhahiri kinakumbatia kipindi chote cha injili — tangu mwanzo wa ukasisi wa Kristo hadi kufungwa kwa muda wa rehema. Kati ya hivyo viwili ni

57

Wakati wa Ngano kukua. {TN3: 57.2}

Miaka mitatu na nusu moja tangu mwanzo wa huduma ya Kristo hadi kusulubishwa Kwake kuwa ni wakati wa kupanda, na wakati wa mavuno kuwa mwisho wa dunia, basi kipindi cha kuingilia kati ni wakati wa kukuza na kukomaza ngano, pia ni

Wakati wa kupanda Magugu. {TN3: 58.1}

Katika kumaliza kupanda mbegu njema, “Mwana wa adamu…. aliiacha nyumba Yake, na kuwapa watumwa Wake mamlaka, na kwa kila mtu kazi yake, naye akamwamuru bawabu akeshe.” Marko 13:34. Lakini Yeye alipokuwa amesafiri, “watu walilala,” jinsi watu wamezoea kufanya wakati mwajiri wao yu mbali. Hivyo, wakati fulani baada ya Kristo kupaa juu “akaja adui akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake.” Mat. 13:25. Lakini watumwa Wake, wakiwa wamelala, hawakujua! Ni picha ya kusikitisha inayoshangaza! Walinzi wa Zayuni wamelala hasa juu ya kuta zake, wakati adui anapita juu yao pasipo kuonekana na kutopingwa! O ni hatia ya kuogofya ilioje ya uzembe mkubwa wa jukumu lililo kwa walinzi tangu siku za mitume! {TN3: 58.2}

Kuwashutumu leo wale wanaohusika na huku kushindwa kulilinda kanisa dhidi ya kuwaorodhesha kwa ushirika haraka yeyote anayekiri kuwa na nia na kuonyesha ari ya ushirika, ingawa mtu huyo hana msingi katika ukweli wala hazai “matunda yapasayo toba,”

58

Roho ya Unabii inatangaza: “Kazi nyingi ya haraka hufanyika kuongeza majina kwenye kitabu cha kanisa. Mapungufu makubwa huonekana katika tabia za baadhi ya wanaojiunga na kanisa. Wale ambao huwaorodhesha husema, Tutawaingiza kwanza kanisani, na baadaye kuwarekebisha. Lakini hili ni kosa. Kazi ile ya kwanza kufanywa ni ya matengenezo…. Msiruhusu wajiunge na watu wa Mungu katika mahusiano ya kanisa hadi wameshuhudia kwa uamuzi kwamba Roho wa Mungu anafanya kazi kwa mioyo yao. Wengi ambao majina yao yamesajiliwa kwenye vitabu vya kanisa si Wakristo.” — Mapitio na Kutangaza, Mei 21, 1901. {TN3: 58.3}

Ni ushahidi gani imara zaidi unaohitajika ili kushawishi nafsi moja kwamba walinzi wamepoteza macho ya kiroho ambayo Yohana Mbatizaji na mitume walikuwa nayo? Yenye kusikitisha kweli ni mashtaka makali: “Wahubiri wanaolala wanahubiri kwa watu wanaolala.” — Shuhuda, Gombo la 2, uk. 337.{TN3: 59.1}

Kutambua “alipowaona wengi miongoni mwa Mafarisayo na Masadukayo wakiujia ubatizo wake,” kwamba baadaye wangemsulubisha Bwana wake Yohana akawaambia, “Enyi wazao wa nyoka, ni nani aliyewaonya ninyi kuikimbia hasira itakayokuja? Basi zaeni matunda yapasayo toba.” Mat. 3:7, 8. Hivyo aliifunua na kuizuia hatua ya shetani kuleta ndani magugu kwa wakati huo. Kwa maana yeye alijua vyema kwamba iwapo magugu yangaliingia na kisha ajaribu kuyang’oa, angeng’oa ngano pamoja nayo. {TN3: 59.1}

59

Na kisha wakati wa mitume, Petro, kama mlinzi mwaminifu wa kanisa, akigundua jaribio la shetani tena kuja na mbegu yake mbaya, akamwambia mwenye hatia: “Anania, kwa nini Shetani amekujaza moyo wako kumwambia uongo Roho Mtakatifu, na kuzuia kwa siri sehemu ya thamani ya kiwanja?… Anania aliposikia maneno haya akaanguka, akafa. Hofu nyingi ikawapata watu wote walioyasikia haya…. Hata muda wa saa tatu baadaye mkewe akaingia.” Petro akamwambia, “Mlikiuza kiwanja kwa thamani hiyo?” Naye akasema, “Naam, kwa thamani hiyo.… Mara akaanguka miguuni pake akafa.” Mdo. 5:3, 5, 7, 8, 10. {TN3: 60.1}

Ukweli kwamba ushirika, pia, umeshindwa kugundua shetani akipanda mbegu yake kati yao, mara mbili inathibitisha hati ya mashtaka: “Wahubiri wanaolala, wanahubiri kwa watu wanaolala” (Shuhuda, Gombo la 2, uk. 337), na inathibitisha kwamba kanisa lote, ukasisi na walei, wamelala fofofo, katika kuyatimiza maneno ya Kristo: “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi,…. Watano wao walikuwa wapumbavu, na watano wenye busara…. Lakini… bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.” Mat. 25:1-5. {TN3: 60.2}

Uovu wa kumruhusu shetani kwa uhuru kupanda magugu kati ya ngano, umekuwepo katika kanisa la Kikristo tangu kulala kwa mitume, na matokeo yake ni kwamba wakati wowote

60

Bwana ametuma ujumbe kwa watu Wake, magugu miongoni mwao mara moja (kwa maelekezo ya viongozi) huinua mikono yao na kupiga kura kumtupa nje yeyote anayemsikiliza mjumbe na kutii ujumbe. Hivyo mara kwa mara kuuza urithi wao kwa thamani duni ya mchuzi wa ndengu, watu wanaodai kuwa ni wa Mungu wamepoteza, na bado kanisa halijajifunza kamwe somo la kusikitisha! {TN3: 60.3}

“Enyi nyumba ya Israeli,” anaonya Bwana, “katika machukizo yenu yote, na iwatoshe, kuwa mmewaingiza wageni, ambao mioyo yao haikutahiriwa, wala miili yao haikutahiriwa, wawe ndani ya patakatifu Pangu, wapatie unajisi, naam, nyumba Yangu, mtoapo sadaka ya chakula Changu, mafuta na damu; nao wameyavunja maagano Yangu, juu ya machukizo yenu yote.” Ezek. 44:6, 7. {TN3: 61.1}

Lakini daima kwa waaminifu, kama vile magugu yamewatupa nje ya makanisa yao, hakikisho la Bwana lenye faraja limekuwa: “Heri ninyi watu watakapowachukia, na kuwatenga, na kuwashutumu, na kulitupa nje jina lenu kama neno ovu, kwa ajili ya Mwana wa Adamu. Furahini siku ile na kuruka-ruka, kwa kuwa, tazama, thawabu yenu ni kubwa mbinguni, maana, baba zao waliwatenda manabii vivyo hivyo.” Luka 6:22, 23. {TN3: 61.2}

Kwa sababu kipindi tangu kulala kwa mitume kimekuwa wakati wa ngano na magugu kukua, na kama , isitoshe, kanisa la Laodekia ni la mwisho kwa sehemu saba za kanisa la Kikristo ambamo ngano na magugu yamechangamana lazima tujifunze jibu la swali:

61

Lipi Ndilo Kanisa la Laodekia? {TN3: 61.3}

Jumuiya ya Ukristo kuwa msitu halisi kwa idadi ya dini zake, madhehebu, na vidhehebu, hivyo tu kwa neno la Mungu anayejua yote tunaweza kulitambua Kanisa la Laodekia. {TN3: 62.1}

Majina ya “makanisa saba” (huwakilisha sehemu zinazofuatana za kanisa la Kikristo, ambazo Laodekia ni la mwisho) si “majina tu.” Chukua kama mfano maarufu jina la ya sita, “Filadelfia.” Maana Yake, “upendo wa undugu,” kuwa kasoro ya hali ya kiroho ya ushirika wowote wa kanisa katika enzi yote ya Ukristo, inafaa kabisa, hata hivyo, hali ya upendo kwa kawaida na ya umoja kwa la ya sita — kanisa la Miller. {TN3: 62.2}

Wakati utangazwaji wa siku 2300 za Danieli 8:14 ulivuma kwa makanisa Kabla ya 1844, waliwanyima kwa jeuri washiriki wao haki ya uhuru wa kidini, kwa kuwakataza hata kuhudhuria mahubiri ya Miller, na kwa kuwatupa nje wale walioupokea ujumbe huo. Kisha baada ya 1844 makundi yale yale ya kidini yalipinga kutangazwa kwa Ujumbe wa Malaika Watatu (Ufu. 14:6-11), tena yakichukua hatua zile zile za udikteta dhidi ya ndugu zao walio na nia huru. Kanisa la Miller kwa hatua yake tofauti na hayo makundi mengine, lilisema, “Kila mtu na athibitike katika akili zake mwenyewe.” (Rum. 14:5), na tusiingie kati ya Mungu na watu Wake kwa kubuni

62

sheria za kidini au kuzuia maoezi uhuru ya dhamiri ya mtu yeyote.” {TN3: 62.3}

Ukiwa ni mfano mmoja unaoangaza wa kanisa ambalo halina hatia yoyote ya kuwazuia au kujaribu kuzuia kwa namna yoyote washiriki wake katika zoezi la haki yao ya msingi kuchunguza na kupokea wenyewe chochote dhamiri yao itawahimiza kuchunguza na kupokea, hilo [kanisa] tu halikuchangia lolote kwa hali mbaya sana inayoitisha andiko: “Lisikilizeni neno la Bwana, ninyi mtetemekao kwa sababu ya neno Lake; Ndugu zenu wawachukiao ninyi, waliowatupa kwa ajili ya jina Langu, wamesema, Na atukuzwe Bwana, tupate kuiona furaha yenu; lakini watatahayarika.” (Isa. 66: 5) katika

Utengo Wa Magugu Kutoka Kati Ya Ngano. {TN3: 63.1}

Mwisho wa kipindi ambacho ngano mechangamana na magugu ni wakati wa kazi ya kufunga kwa kanisa la Laodekia (la mwisho kwa makanisa saba). Kazi hii imetambuliwa na mwasisi wa kanisa kama kutia alama katika Ezekieli 9, kuwatia muhuri Waisraeli wa kiroho, watu 144,000. (Angalia Shuhuda kwa Wachungaji, uk. 445 na Shuhuda, Gombo la 3, uk. 266; Gombo la 5, uk. 211.) Na utambulisho huu unahakikishwa kikamilifu kwa ukweli, jinsi ulivyoonekana humu, kwamba unabii wa Ezekieli ni utengo wa matabaka mawili — wale ambao “wanaugua na kulia dhidi ya machukizo yote yanayofanyika kati yake” (kanisa) na wale ambao

63

hawafanyi hivyo. Na kwa sababu wa awali wanaokolewa ilhali wa mwisho wanaanguka chini ya silaha za kufisha za malaika, unaonekana wazi utengo kamili wa magugu kutoka kati ya ngano katika

Wakati wa Mavuno. {TN3: 63.2}

Ingawa maana ya kweli na wakati wa mavuno imekanganywa sana na wachache na kuwachanganya wengi, uchunguzi wa karibu wa Neno utatatua huo mkanganyo kwa namna rahisi kama ulivyotatua wakati wa kupanda mbegu na kipindi cha ngano na magugu. {TN3: 64.1}

Kwa jicho Lake likipenyeza ukungu wa vizazi vingi, Kristo aliona kimbele utepetevu wa walinzi Wake na uovu ambao ungeota katika kanisa Lake. Hata hivyo, baada ya kuulizwa na watumwa Wake, “hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? …. Basi, wataka twende tukayakusanye? Akasema, La; msije mkakusanya magugu, na kuzing’oa ngano pamoja nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na katika wakati wa mavuno Mimi nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani Mwangu.” Mat. 13:27-30. {TN3: 64.2}

Mavuno humaanisha “tokeo la juhudi,” la kufanya kazi, “kuyakusanya mazao” — kuvuna matokeo ya kazi na kuyajaza maghala kwa nafaka. Hivyo badala ya kazi ya mwaka

64

kuwa inakwisha mwanzoni mwa mavuno, kazi nzito zaidi ya mwaka huanza wakati huo. Na ingawa wakati wa mavuno ni mfupi zaidi kuliko vipindi vyote vya mwaka wa mavuno, kazi ya kuvuna haifanyiki kwa nukta; huchukua muda. Mavuno hayakusanywi kwa kugeuza shamba hadi ndani ya ghala; la, hilo litakuwa rundiko la ujumla badala ya mavuno. Kwanza mundu unawekwa kwenye nafaka, na ijayo nafaka hufungwa miganda, kisha kupura, hatimaye huwekwa ghalani; na baada ya hayo makapi na magugu kuharibiwa. Kazi hii inapokamilika wakati wa vuli, huonyesha kwamba mavuno ni msimu wa nyakati baada ya “wakati wa hari umepita,” na unafuatwa na kipindi gumba cha masika. {TN3: 64.3}

Ni lazima iwe kwa mavuno ya kiroho ambayo vinginevyo hayangeweza kuonyeshwa kwa ya asili. Usiangalie kwa wepesi hekima ya Mungu: mifano Yake ni mikamilifu. {TN3: 65.1}

Angalia, sasa, ni kwa uhalisi gani amini kwa mavuno ya asili Bwana amesimulia kweli za mavuno ya kiroho: “Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno,” Yeye anasema: “na wakati wa mavuno Mimi nitawaambia wavunao, Yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani Mwangu.” Mat. 13:30. {TN3: 65.2}

Katika maneno haya ya kimfano Kristo ameufanya utaratibu wa kiroho wa kuvuna

65

kufanana na wa asili. Mmoja usingalikuwa sawa sawa na mwingine, Yeye angebainisha utofauti. Kwa hivyo, unaonywa kwa upole, usiruhusu mawazo ya ubatili yaingie ndani ya akili, ila usimame kidete kwa Maandiko, kwa sababu yamejaa maana kamili ya thamani isiyowekewa mipaka — hakika, ni, maisha yako. {TN3: 65.3}

Kama neno “mpaka” humaanisha “hadi,” magugu kwa hivyo yatakusanywa nje, si kabla au baada ya mavuno, lakini mwanzoni mwake. Na “wakati wa mavuno” kuwa “mwisho wa muda wa rehema” (Mafunzo ya Kristo kwa Mifano, uk. 72), basi mavuno yenyewe lazima yanatangulia kufungwa kwa mlango wa rehema — msimu gumba wa kipupwe. Kwa hivyo, magugu yanatengwa kutoka kati ya ngano kabla, si baada ya, mwisho wa muda wa rehema. {TN3: 66.1}

Ngano, “wana wa ufalme” (Mat. 13:38), wanakusanywa ghalani, ufalme; magugu, “wana wa yule mwovu” (aya ya 38) — wanaodai tu, wale ambao si watendaji wa Neno, na ambao walipewa ushirika “watu walipolala “ — “jinsi magugu yakusanywavyo na kuchomwa motoni” (Mat. 13:40), baada ya ngano kufungwa miganda. Lakini

Ni Nani Wavunaji? {TN3: 66.2}

“Na wale wavunao ni malaika.” ambao “watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki.” Mat. 13:39, 49. Malaika hawa si ambao “watakuja pamoja”

66

na Kristo wakati wa ujio Wake wa pili, ila wale Yeye “atatuma.” Wao ni kama malaika watatu wa Ufunuo 14:6 -11. Hakika, malaika wa tatu “ataichagua ngano kutoka kati ya magugu na kutia muhuri, au kuifunga, ngano kwa ajili ya ghala la mbinguni.” — Maandishi ya Awali, uk. 118. Kwa hivyo malaika, wavunaji, ambao Kristo anatuma, ni pamoja na yule anayetia muhuri, au kufunga, na wale wanaofuata ili kuangamiza (Ezek. 9:2, 5, 6), kwanza kanisani, kisha duniani. Hivi ndivyo

Utengo Katika Sehemu Mbili. {TN3: 66.3}

Ile amri, “kKusanya kutoka katika ufalme Wake vitu vyote vinavyochukiza, na hao watendao maasi,” haimaanishi kuwakusanya watakatifu Wake kutoka duniani kuingia mbinguni; wala haina maana ya kuwaangamiza waovu kutoka kwa dunia; maana wa awali watakusanywa, si moja kwa moja hadi mbinguni, lakini kwanza hadi ndani ya “ghala,” ufalme kwa dunia; na wa mwisho hawataangamizwa mara moja “katika wakati wa mavuno,” lakini kwanza watakusanywa katika matita, na kisha kuangamizwa, jinsi inavyoelezwa zaidi katika mfano wa juya: {TN3: 67.1}

“Tena ufalme wa mbinguni umefanana na juya, lililotupwa baharini, likakusanya samaki wa kila namna; hata lilipojaa, walilivuta pwani; wakaketi, wakakusanya walio wema vyomboni, bali walio wabaya wakawatupa.” Mat. 13:47, 48. {TN3: 67.2}

67

Mfano huu pia huonyesha utengo wa waovu kutoka kati ya watu wa Mungu kanisani (“juya”), hii ikiwa ni sehemu ya kwanza ya kazi ya utengo, mwanzo wa mavuno. Sehemu andamo inafuata katika dunia, hivyo dunia inapoangazwa kwa utukufu wa malaika wa “Kilio Kikuu,” na pia “sauti nyingine kutoka mbinguni,” ikisema: “Tokeni kwake, enyi watu Wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” Ufu. 18:4. {TN3: 68.1}

Kumbuka kwamba katika sehemu ya kwanza ya utengo ndani ya kanisa, waovu wanaondolewa mbali kutoka kati ya watakatifu, ilhali katika wa pili, ule wa Babeli, watakatifu wanaitwa kutoka kati ya waovu. {TN3: 68.2}

Kwa sababu shamba ni “ulimwengu” (Mat. 13:38), ule mfano wa ngano na magugu ni lazima hushughulisha sehemu zote za mavuno. Kama, kutofautisha, “juya” hukokota ndani “samaki,” waongofu waliofanyizwa na kanisa la injili, mfano wa juya kwa hivyo eneo lake ni utengo katika kanisa. Pamoja hutofautisha

Uhusiano wa Malimbuko kwa Mavuno Ya Pili. {TN3: 68.3}

Isaya pia alipewa mtazamo wa mavuno maradufu. “Kwa maana Bwana atateta na wote wenye mwili, kwa moto na kwa upanga Wake; nao watakaouawa na Bwana watakuwa wengi. Watu wale wajitakasao,

68

na kujisafisha katika bustani, nyuma yake aliye katikati; wakila nyama ya nguruwe, na machukizo, na panya; watakoma pamoja, asema Bwana.” Isa. 66:16, 17. {TN3: 68.4}

Wale waliouawa na Bwana, katika andiko hili ni wale wanaodai kuwa katika imani, wanaosema tu utakaso na kusafishwa, ila hufanya hivyo kwa sifa za haki yao, — ya “wao wenyewe,” — si kwa wema wa haki ya Kristo. Hutembea, yaani, katika njia zao wenyewe, si katika utiifu kwa ukweli. Wakiwa wamejifunika mavazi haya bandia ya utakaso na kusafishwa, wanajifanya kama wana-matengenezo, ila wakati wote wanajiingiza katika machukizo ya wapagani; wakifanya hivyo kwa siri — “nyuma ya mti mmoja,” au, jinsi pambizo husema, humfuata anayeongoza “mmoja baada ya mwingine.” Na chakula (nyama ya nguruwe, panya, na machukizo, — chochote kinachoweza kuwa popote pale Wakristo hawa wa kipagani wanaweza kuwa, — vyakula vinavyoliwa mtawalia tu katika sehemu fulani za dunia, kati ya vikundi tofauti na jamaa) ambavyo hufurahia kuridhisha tamaa zao, huonyesha kwamba matokeo ya maangamizi kati ya hawa waliojitakasa nafsi na waliojisafisha nafsi ni ndani ya kanisa duniani kote. {TN3: 69.1}

Kwamba maangamizi hayakuwa kati ya Mataifa, ambao hawakuujua ukweli wa Mungu na uwezo Wake mkuu huonyeshwa wazi kwa maneno ya Bwana: “Nami nitaweka ishara kati yao, Nami nitawatuma hao waliookoka kwa mataifa, Tarshishi, na Puli, na Ludi, wavutao upinde, kwa Tubali na

69

Yavani [nchi za Mataifa leo zinavyoitwa kwa majina yazo ya kale], visiwa vilivyo mbali; watu ambao hawajahabari Yangu, wala hawajauona utukufu Wangu; nao watahubiri utukufu Wangu kati ya mataifa.” Isa. 66:19. {TN3: 69.2}

Kwa sababu hawa waliokoka (malimbuko, watu 144,000 watumwa wa Mungu — Ufu. 7:3) “watawaleta ndugu zenu wote” (mavuno ya pili umati mkubwa — Ufu. 7:9) “kuwa sadaka…kutoka katika mataifa yote” (Isa. 66:20, sehemu ya kwanza), huu ukusanywaji ndani mkubwa kwa hivyo lazima, ni kufunga kazi ya injili — sehemu ya pili ya mavuno. {TN3: 70.1}

Na kwa sababu, isitoshe, hawa waliokoka watawaleta ndugu zao wote mpaka “mlima Wangu mtakatifu Yerusalemu, asema Bwana;” “katika chombo safi hadi ndani ya nyumba ya Bwana.” (Isa. 66:20, sehemu ya mwisho), ukweli ni wazi kabisa kwamba kuangamizwa kwa waovu kunaleta utakaso wa kanisa. Kile “chombo safi” kwa hivyo ni kanisa lililotakaswa, linalojumuisha wale waliokoka malimbuko, watu 144,000 — ambao, huru kutoka kwa waovu (magugu) basi wakati huo, kama “watumwa wa Mungu wetu,” watawaleta ndani mavuno ya pili, umati mkubwa ambao hakuna mtu anayeweza kuuhesabu, kutoka katika mataifa yote. {TN3: 70.2}

Sehemu ya pili ya utengo ikiwa hivi imekamilika, muda wa Rehema unafungwa. Halafu kutoka kwa waovu yatasikika maombolezo ya kutisha kwa maangamizo: “Mavuno yamepita, wakati wa hari umekwisha, wala sisi hatujaokoka.” Yer. 8:20. {TN3: 70.3}

70

Huu uliwa ni uzoefu wa kutisha wa magugu huko Babeli, katika sehemu ya pili ya mavuno, lazima uwe, kama mfano, sawa na uliotangulia kwa magugu katika kanisa la Laodekia, katika sehemu ya kwanza ya mavuno, usambamba ambao unaonyesha kwa kumalizia kwamba

Kanisa Si Babeli. {TN3: 71.1}

Sababu ya kwamba kanisa si “Babeli” kimfano ni kwamba linaitwa Yerusalemu (Ezek. 9:4,8), na kutoka kati ya wema ndani yake, waovu (magugu) wanaangamizwa, wanaondolewa nje na wale watu sita wenye silaha za kufisha (Ezek. 9:6-9), na kisha baadaye wema (ngano) wanakusanywa ndani ya “ghala;” ilhali kutoka kwa waovu huko Babeli, wenye haki (“watu Wangu”) wanaitwa watoke na kukusanywa ghalani, na kisha waovu waliosalia wanaangamizwa na malaika saba wakiyamimina mapigo saba ya mwisho. {TN3: 71.2}

Hivyo katika sehemu ya kwanza ya mavuno, utengo katika kanisa, waovu wanaangamizwa na watu sita wenye silaha za kuchinja, kabla wale wema kuondolewa; na katika sehemu ya pili, utengo kati ya makanisa ya Babeli, waovu wanaangamizwa na malaika saba kwa mapigo saba ya mwisho, baada ya wema kuondolewa. Kwa hivyo ipo mitengo miwili na mavuno mawili: ule wa awali unatoa malimbuko, watu 144,000, ambao hawajatiwa unajisi na wanawake (Ufu. 14:4). Yaani, wao ndio ambao ujumbe wa kutiwa muhuri unawapata

71

katika kanisa la Mungu, si katika makanisa ya wapagani. Na ule wa pili unatoa mavuno ya pili, umati mkubwa kutoka kwa mataifa yote, baadhi yao pia huenda hawajatiwa unajisi na wanawake — makanisa ya wapagani. {TN3: 71.3}

Tukiwa kufikia hatua hii tumeichambua hukumu, mavuno, katika nuru ya shuhuda za manabii na mifano ya Kristo, sasa tutaichunguza

KATIKA NURU YA HUDUMA ZA SHEREHE. {TN3: 72.1}

Kama vile Roho ya Unabii hutangaza kwamba “mfumo wote wa mifano na nembo ulikuwa unabii ulioshindiliwa wa injili, utoaji ambao ulikuwa umefungiwa ahadi za ukombozi” (Matendo ya Mitume, uk. 14), hivyo mpango wa wokovu umefunuliwa si tu katika shuhuda za manabii na katika mifano ya Kristo lakini pia katika mifano na nembo za hekalu la duniani. Katika kuongezea hili, uzoefu wa watu katika kipindi cha mfano “Basi mambo hayo yaliwapata wao,” tunaambiwa, “kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani.” 1 Kor. 10:11. Kwa hivyo kwa busara tumefungwa kuanzia mwanzo hasa ili kuyaangalia maagizo ya Mungu kwa Musa: {TN3: 72.2}

“Siku ya kumi ya mwezi huu wa saba ni siku ya upatanisho:…. fanya upatanisho kwa ajili yenu mbele ya

72

Bwana, Mungu wenu. Kwa kuwa mtu awaye yote asiyeitesa nafsi yake siku iyo hiyo, itakatiliwa mbali na watu Wake.” “Fanya upatanisho kwa ajili ya wana wa Israeli….mara moja kila mwaka.” Law. 23:27-29 ; 16:34. {TN3: 72.3}

Wakati mtu mmoja “amekataliwa mbali na watu Wake” kwa sababu ya dhambi, jina lake lazima pia “lifutwe katika kitabu cha walio hai.” Zab. 69:28. Kwa hivyo, siku ya upatanisho ilikuwa siku ya hukumu, jinsi hata sasa inavyojulikana na Wayahudi, na kwa kidokezi hicho ilianzishwa kama mfano wa siku kuu ya upatanisho ya uakisi (hukumu ya upelelezi) — siku ambayo Bwana atayafuta kutoka katika kitabu Chake majina ya wadhambi wote, na “kukatwa kabisa” kutoka kwa kongamano la watu Wake wote ambao majina yao hayatakuwa katika kile kitabu. {TN3: 73.1}

Mintarafu siku ya upatanisho ya mfano, amri ya Bwana kupitia kwa Musa ilikuwa: “Katika siku hiyo kuhani atafanya upatanisho kwa ajili yenu, ili kuwatakasa; ili muwe safi kutoka kwa dhambi zenu zote mbele ya Bwana…. Naye atafanya upatanisho kwa ajili ya hekalu takatifu, naye atafanya upatanisho kwa ajili ya hema ya kukutania, na kwa ajili ya madhabahu.” Law. 16:30, 33. {TN3: 73.2}

Ikiwa ni siku ya upatanisho kwa mfano kwa wote wafu na walio hai, huduma hii ya hekalu la duniani kwa hivyo huonyesha siku ya upatanisho katika uakisi wake kutakaswa kwa hekalu mbinguni kutoka

73

kwa majina yasiyostahili katika vitabu, na kutakaswa kwa kanisa duniani kutoka kwa washiriki wake ambao hawajaongoka na wasiokuwa imara, — hivyo kuleta wakati wa vitabu safi, kanisa safi, na watu wasafi. {TN3: 73.3}

Akitazama mbele kwa siku hii ya utakaso, Zekaria hutabiri: “Katika siku hiyo katika njuga za farasi yataandikwa maneno haya, WATAKATIFU KWA BWANA; navyo vyombo vilivyomo ndani ya nyumba ya Bwana vitakuwa kama mabakuli yaliyoko mbele ya madhabahu. Naam, kila chombo katika Yerusalemu, na katika Yuda, kitakuwa kitakatifu kwa Bwana wa majeshi:… na katika siku hiyo hatakuwamo tena Mkanaani ndani ya nyumba ya Bwana wa majeshi.” Zek. 14:20, 21. {TN3: 74.1}

Kulitabiri tukio lilo hilo, nabii Isaya anatangaza: “Na Mataifa wataiona haki yako, na wafalme wote watauona utukufu wako; nawe utaitwa jina jipya, litakalotajwa na kinywa cha Bwana. Nawe utakuwa taji ya uzuri katika mkono wa Bwana, na kilemba cha kifalme mkononi mwa Mungu wako. Hutaitwa tena Aliyeachwa; …. utaitwa Hefziba …. Watu watakatifu.” Isa. 62:2-4, 12. {TN3: 74.2}

“Bali ninyi…mmwachao Bwana, na kusahau mlima Wangu mtakatifu,….nanyi mtaliacha jina lenu kuwa laana kwa wateule Wangu. Na Bwana MUNGU atakuua; na atawaita watumwa Wake kwa jina lingine.” Isa. 65:11, 15. {TN3: 74.3}

“Na watu wasiofahamu wataangamia.” Hos. 4:14. “Wengi watajitakasa,

74

na kujifanya weupe, na kusafika; bali wabaya watatenda mabaya; wala hataelewa mtu mbaya awaye yote; bali wao walio na hekima ndio watakaoelewa.” Dan. 12:10. {TN3: 74.4}

Wale ambao maono yao ni safi kwa ukweli wa mavuno jinsi unavyofundishwa katika shuhuda za manabii na katika mifano watakuwa na maono safi zaidi tunapochambua maana ya

Mganda wa Kutikiswa, Mikate ya Kutikiswa, Na Sikukuu Ya Vibanda. {TN3: 75.1}

Kuonyesha wokovu wetu kwa ukamilifu, hafla za mavuno za mfumo wa sherehe lazima zithibitishe shuhuda zote za manabii na mifano kuhusu mavuno, kwa maana zote zimefunganishwa kabisa kwa pamoja. Sherehe za mavuno ya malimbuko na ya pili ya nafaka basi lazima zifunue ukweli kuhusu mavuno ya malimbuko na ya pili ya wanadamu. Katika Sheria ya Walawi tunasoma: {TN3: 75.2}

“Mtauleta mganda wa malimbuko ya mavuno yenu kwa kuhani; naye atautikisa mganda mbele ya Bwana ili kwamba ukubaliwe kwa ajili yenu; siku ya pili baada ya Sabato kuhani atautikisa… Nanyi msile mkate, wala bisi, wala masuke machanga, hata siku iyo hiyo, hata mtakapokuwa mmekwisha kuleta sadaka ya Mungu wenu:… Nanyi mtajihesabia tangu siku ya pili baada ya Sabato, tangu siku hiyo mliyouleta mganda wa sadaka ya kutikiswa; zitatimia Sabato saba;

75

hata siku ya pili ya hiyo Sabato ya saba mtahesabu siku hamsini; nanyi mtamsongezea Bwana sadaka ya unga mpya. Mtatoa katika makao yenu mikate miwili ya kutikiswa, itakuwa ya sehemu za kumi mbili za efa; itakuwa ya unga mwembamba, itaokwa na chachu, hiyo ni malimbuko kwa Bwana… Pia katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, hapo mtakapokuwa mmekwisha kuyachuma mavuno ya nchi, mtaweka sikukuu ya Bwana muda wa siku saba; siku ya kwanza itakuwa sabato, na siku ya nane itakuwa sabato.” Law. 23:10,11, 14-17, 39. {TN3: 75.3}

Hapa tunaona ziliamriwa maadhimisho ya sherehe tatu za mavuno: (1) sherehe ya mganda wa kutikiswa, mwanzoni mwa mavuno ya malimbuko; (2) sherehe ya mikate ya kutikiswa, mwishoni mwa mavuno ya malimbuko; na (3) sikukuu ya vibanda mwishoni mwa mavuno ya pili. Zikiwa mfano, mavuno haya mawili ya nafaka na sakramenti zake tatu halisi, kwa hivyo zinatabiri mavuno mawili ya nafsi na sherehe tatu za kiroho, ya kwanza ambayo ni

Malimbuko Na Mganda wa Kutikiswa Na Mikate ya Kutikiswa. {TN3: 76.1}

Ukiwa ni vikonyo vilivyokatwa vya nafaka, mganda wa kutikiswa uliashiria mazao yatakayovunwa. Na kama vile mganda ulipaswa kutolewa kabla ya mundu kuwekwa kwenye nafaka na kukusanywa kuwa miganda, ilitabiri umbele kwa mavuno ya kiroho ya malimbuko yatakayokusanywa. {TN3: 76.2}

76

[Picha ya Mavuno ya Sherehe]

Kwa Pentekoste siku hamsini baada ya mganda halisi ulitolewa, Waisraeli wote wangetoa “sadaka ya unga mpya kwa Bwana….

77

[mikate miwili ya kutikiswa “iliyookwa na chachu”] malimbuko kwa Bwana.” Law. 23:16, 17. {TN3: 77.1}

Mganda wa kutikiswa na mikate ya kutikiswa ilikuwa ni sadaka za shukrani kwa ajili ya malimbuko. Moja ilitolewa wakfu mwanzoni mwa mavuno; ile nyingine wakati wa kukamilika kwa mavuno. Tofauti kwa mganda wa kutikiswa wa vikonyo vilivyokatwa vya nafaka, ulitangulia mavuno ya kukusanywa baada ya mganda wa kutikiswa kutolewa, mikate ya kutikiswa, ikiwa bidhaa iliyo tayari, iliashiria mavuno yaliyokusanywa awali. (Msomaji ambaye ataweza kuelewa vizuri zaidi maana ya maadhimisho ya sherehe hizi tatu zote muhimu kwa wokovu wetu, ataufuata mchoro kwa ukurasa wa 77, tunapoendelea.) {TN3: 78.1}

Itaonekana kwamba ile amri kuhusu kuadhimisha Sabato ya siku ya saba, vile vile na ile inayohusu kuadhimisha za kila mwaka sikukuu za sherehe, zimeandikwa katika sura ya ishirini na tatu ya Mambo ya Walawi, aya ya 3. Uangalifu, kwa hivyo, ni lazima utekelezwe kutouchanganya ukweli mmoja na mwingine. {TN3: 78.2}

Mganda wa kutikiswa ulipaswa kutolewa “siku ya pili baada ya Sabato” — yaani, siku ya kwanza ya juma, ambayo sasa kwa kawaida huitwa Jumapili. Sadaka hii ingetolewa, si kwa siku maalum ya mwezi, ila badala yake kwa siku maalum ya juma, kabla ya mundu kuwekwa kwa nafaka na kukusanywa kuwa miganda (Law. 23:11, 14). Ikija kwa wakati sahihi, katika msimu wa malimbuko, juma la

78

Pasaka lilikuwa kipindi ambacho ndani yake mganda wa kutikiswa kwa kawaida ulitolewa mbele ya Bwana, ibada yake ikionyesha kinabii

Kristo, Akisi Wa Mganda Wa Kutikiswa. {TN3: 78.3}

Kwa zaidi ya miaka elfu, kutikiswa kwa mganda kila mwaka kulionyesha umbele kwa tukio lake la uakisi, kufufuka kwa Kristo. Na jinsi Kristo alivyofufuka siku ile ile ambayo mganda wa kutikiswa ulipaswa kutolewa, siku “baada ya Sabato,” mtu yeyote asidai eti umoja wa upatano wa matukio hayo mawili siku hiyo kama ulinganifu wa bahati nasibu au kwa sababu yoyote isipokuwa ubunifu wa Mungu. “Yeye alikuwa akisi wa mganda wa kutikiswa,” yatangaza Roho ya Unabii, “na ufufuo Wake ulitukia kwa siku ile ile mganda wa kutikiswa ulipaswa kutolewa mbele ya Bwana.” — Tumaini la Vizazi Vyote, uk. 785. {TN3: 79.1}

Hivyo, Kristo, malimbuko, na wale ambao pamoja Naye katika ufufuo Wake walitoka kaburini, walifufuliwa kwa uzima wa milele, walikuwa mganda wa kutikiswa akisi wa wafu. Na kwa sababu mganda wa kutikiswa wa nafaka ulionyesha umbele kukusanywa ndani malimbuko ya kondeni, vivyo hivyo wale waliofufuka na Kristo, kuwa malimbuko ya wafu, walionyesha umbele kukusanywa malimbuko ya Injili — wanafunzi 120. Lakini wale waliofufuka na Kristo walipaa pamoja Naye kama nyara za ushindi Wake juu ya kifo na kaburi, wao hivyo basi wakawa mfano hai, na hivyo

79

Mganda wa Kutikiswa wa Walio Hai. {TN3: 79.2}

Kama vile Kristo alivyofufuka siku ile ile mganda wa kutikiswa ulipaswa kutolewa, vivyo hivyo Roho Mtakatifu aliwashukia wanafunzi 120 siku ile ile mikate ya kutikiswa ilipaswa kutolewa mbele ya Bwana. Pentekoste ya mitume ilikuwa basi mfano-pacha wa Pentekoste ya sherehe (siku ile mikate ya kutikiswa ilitolewa). Na kwa sababu mganda wa kutikiswa ulikuwa ni mfano wa Kristo na wa wale waliofufuka pamoja Naye kama wa kwanza wa malimbuko ya wafu, kwa hivyo mikate ya kutikiswa ilikuwa ni mfano wa wanafunzi 120 waliojazwa Roho ambao walikuwa kikamilisho kamili cha malimbuko ya wafu, na ambao walikusanywa ndani baada ya ufufuo. {TN3: 80.1}

Kutoka kwa kweli hizi inaweza kuonekana wazi zaidi kwamba wale ambao Kristo Alienda nao walikuwa mganda hai wa kutikiswa na wa pekee ambao umewahi kutolewa katika hekalu la mbinguni; na ya kwamba wakiwa wale waliofufuliwa kutoka kwa wafu, wao ni malimbuko ya wafu, ilhali wakiwa hai milele mbele ya Baba, wao ni mganda hai wa kutikiswa wa walio hai wa malimbuko ya walio hai, watu 144,000 watumwa wa Mungu, ambao kwa mfuatano wanatangulia

Mavuno ya Pili Na Sikukuu Ya Vibanda. {TN3: 80.2}

Wanafunzi 120 kwa siku ya Pentekoste wakiwa malimbuko ya wafu ya injili, hufuata kwamba umati mkubwa ulioongezeka kwa kanisa kila siku baada ya hapo, kwa kawaida walikuwa mavuno ya pili ya wafu ya injili. {TN3: 80.3}

80

“Pia katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba,” inaendelea rekodi ya Walawi ya maagizo ya Bwana mintarafu ya ibada za mavuno, “hapo mtakapokuwa mmekwisha kuyachuma mavuno ya nchi, mtaweka sikukuu ya Bwana muda wa siku saba:… Nanyi siku ya kwanza mtajipatia matawi ya miti mizuri, na makuti ya mitende, na matawi ya miti minene, na mierebi ya vijitoni; nanyi mtafurahi mbele ya Bwana, Mungu wenu, muda wa siku saba… Mtakaa katika vibanda muda wa siku saba; wazalia wote wa Israeli watakaa katika vibanda.” Law. 23:39, 40, 42. {TN3: 81.1}

Kwa sababu mganda wa kutikiswa na mikate ya kutikiswa ni ya mfano, basi pia Sikukuu ya Vibanda lazima iwe ya mfano. Vinginevyo sherehe haingaliadhimishwa kama sehemu ya ibada ya mavuno. Na ilivyo katika mfano sikukuu ilipaswa kusherehekewa mwishoni mwa kukusanya mavuno ya mwaka, basi vivyo hivyo katika uakisi ni lazima iadhimishwe mwishoni mwa kukusanya mavuno ya dunia, ambayo yanakaribia kutimizwa kwake. Hivyo wakati uliotumiwa kuzalisha na kutoa mganda wa kutikiswa na mikate ya kutikiswa, pia katika kuadhimisha Siku kuu ya Vibanda, ni uwakilishi wa wakati wote wa mavuno ya kiroho ya walio hai na wafu. {TN3: 81.2}

Kutoa ukweli huu Roho ya Unabii inasema: {TN3: 81.3}

“Siku kuu ya Vibanda haikuwa tu ya ukumbusho, bali ya mfano… Ilisherehekewa

81

kwa ukusanywaji wa mavuno ya nchi, na ilionyesha mbele kwa siku kuu ya kukusanya ya mwisho, wakati Bwana wa mavuno atawatuma wavunaji Wake kuyakusanya magugu pamoja katika matita kwa moto, na kuikusanya ngano ndani ya ghala Lake. Kwa wakati huo, waovu wote wataangamizwa.” — Wazee wa Imani na Manabii, uk. 541. {TN3: 81.4}

Waziwazi, kwa hivyo, kwa sababu malimbuko na mavuno ya pili ya mavuno halisi na ibada zake za huduma yalikuwa kivuli cha mavuno ya kiroho ya malimbuko na mavuno ya pili, yatafikia kilele kwa Siku kuu ya Vibanda ya uakisi. {TN3: 82.1}

“Naliona watakatifu,” asema mtumwa wa Bwana akiifafanua sherehe hii, “wakihama mijini na vijijini, na wakiungana pamoja katika makundi, na kuishi katika maeneo ya faragha zaidi. Malaika waliwapa chakula na maji, ilhali waovu walikuwa wanateseka kwa njaa na kiu.” — Maandishi ya Awali, uk. 282. {TN3: 82.2}

Kwa hivyo Israeli ya kale kukaa katika vibanda ni mfano wa Israeli mamboleo hatimaye kukaa kwenye misitu. Isivyoweza kukanushwa, kwa hivyo, mavuno ya Mathayo 13 hutangulia kufungwa kwa muda wa rehema, na ni wakati wa kuyakusanya malimbuko na mavuno ya pili — watu 144,000 na “umati mkubwa,” — watakatifu wote ambao watahamishwa bila kufa. {TN3: 82.3}

Kwa sababu nuru inayokazia hatua hii hufichua wazi kwamba Pentekoste baada ya ufufuo

82

ilikuwa ya kuwakusanya wale ambao wangekufa, lazima, vivyo hivyo, iwepo Pentekoste kwa ajili ya kuwakusanya wale ambao watahamishwa bila kufa. Na kwa ishara hiyo ya busara, mganda wa kutikiswa na mikate ya kutikiswa lazima iwe na matumizi maradufu, kila moja kwa wafu na kwa walio hai, kwa pamoja ikijumuisha mazao yote ya mavuno ya uakisi. {TN3: 82.4}

Pentekoste ya Mitume kwa kutoa uwezo wa kuyakusanya mavuno ya pili hadi mwanzoni mwa hukumu ya wale ambao sasa wamelala, iliashiria umbele Pentekoste ya mwisho ambayo bado ni ya baadaye, na ambayo italeta uwezo wa kuyakusanya mavuno ya pili ya walio hai, wale ambao hawatakufa kamwe. Kwa maneno mengine, wale waliokufa kabla ya Pentekoste ya mwisho watahukumiwa kwa nuru ya ukweli unaoakisi kupitia nguvu ya Pentekoste ya mitume. {TN3: 83.1}

(Kutoka kwa ubatizo Wake hadi kupaa Kwake, Kristo alifundisha ng’ambo ukweli ambao ungewaandaa wale ambao wangeupokea, kuufundisha. Kisha katika siku ya Pentekoste, Aliwapa Roho Wake kuutangaza kwa nguvu.) {TN3: 83.2}

Mintarafu ya hukumu, mavuno, mtumwa wa Bwana anatangaza: {TN3: 83.3}

“Kisha nalimwona malaika wa tatu. Akasema malaika aliyeandamana nami, ‘Ya kutisha ni kazi yake. Utume wake ni wa kuogofya. Yeye ndiye malaika atakayeichagua ngano kutoka kwa magugu, na

83

kutia muhuri, au kufunga, ngano kwa ghala la mbinguni.” — Maandishi ya Awali, uk. 118. {TN3: 83.4}

“Basi sasa msiwe watu wenye kudharau, vifungo vyenu visije vikakazwa; maana nimesikia kutoka kwa Bwana, Bwana wa majeshi, habari ya hukumu itakayotimizwa, nayo imekusudiwa, itakayoipata dunia yote pia. Tegeni masikio, sikieni sauti Yangu, sikilizeni mkasikie neno Langu.” Isa. 28:22, 23. {TN3: 84.1}

Na sasa ya kwamba kila mmoja ambaye kwa uaminifu hutafuta kusikia na kutii sauti ya Ukweli anaweza kuwa na ufahamu wa kutosha wa kudaka vipengele kadhaa vya somo la hukumu, mavuno, vinaletwa hapa ndani ya lengo liliojumuishwa: {TN3: 84.2}

Msomaji atakumbuka kwamba wale waliofufuka na Kristo siku ya kumi na nane ya mwezi wa kwanza (fuata mchoro kwa ukurasa wa 55), walifanywa kutoweza kufa na kupokelewa mbinguni kama mganda wa uakisi, wakionyesha umbele kukusanywa kwa mavuno ambayo hayatakufa kamwe. Ufufuo wao kutoka kwa wafu uliashiria mwanzo wa mavuno ya malimbuko ya wanafunzi 120 ambao wangekufa na kufufuliwa. Ukweli kwamba wafuasi wa Kristo hawakuwa na umoja kabla ya huo ufufuo, ni ushuhuda mzuri sana kwamba malimbuko (watu 120) ya wale wanaolala hawakukomaa (kuwa waongofu kamili) mpaka baada ya ufufuo. {TN3: 84.3}

Siku 40 za uwepo wa Kristo kwa dunia baada ya kufufuka Kwake zilikuwa

84

wakati ambao malimbuko walikusanywa, maana baada ya kupaa Kwake Wakristo walijifungia kwenye chumba cha juu na hawakuondoka kuhubiri ukweli kufikia siku ya Pentekoste. Wale 120 ambao walipokea nguvu ya Roho kwa siku ile ile mikate ya kutikiswa ilitolewa, walikuwa kwa hivyo mikate ya kutikiswa ya uakisi, ikiashiria kukamilika kwa mavuno ya malimbuko. Mtawalia yakaja mavuno ya pili ya wafu, katika kipindi ambacho magugu yalichangamana na ngano. {TN3: 84.4}

Ajabu hakika ni njia ambayo Mungu ameufanya mpango wa wokovu na kuufunua hatua kwa hatua kadri inavyohitajika. Wakati katika 1844 hukumu ya upelelezi ya wafu na kuanza kuyakusanya malimbuko ya walio hai, Yeye hakuwaacha watu Wake gizani kuhusu matukio haya. Njozi ya kwanza ambayo Dada White alipokea mwaka wa 1844 ilikuwa ya watu 144,000 malimbuko, “watumwa wa Mungu wetu,” ambao hawataonja kifo kamwe. (Tazama Maandishi ya Awali, uk. 13-15.) {TN3: 85.1}

Kama vile Kristo na wale ambao Yeye aliwafufua na kwenda pamoja Naye wakawa mganda wa mfano pacha, wakiashiria kimbele kukusanywa kwa malimbuko (watu 120) ya wale watakaofufuliwa, hivyo pia wakati Yeye aliingia kwa huduma Yake ya ukuhani katika patakatifu pa hekalu la mbinguni, na kujiwasilisha Mwenyewe na nyara Zake mbele ya Baba Yake, wakawa mganda wa uakisi, na kuashiria kimbele kukusanywa

85

malimbuko ya wale watakahamishwa bila kufa (watu 144,000 watakatifu walio hai). Katika nuru ya usambamba huu, hali ya kiroho ya watu 120 kabla ya Pentekoste ya mitume inaonekana wazi kuonyesha hali ya kiroho ya watu 144,000 kabla ya Pentekoste ya baadaye. {TN3: 85.2}

Siku 40 (Mdo. 1:3, 9) kutoka kwa ufufuo hadi kupaa vivyo hivyo ni mfano wa kipindi kutoka 1844 hadi kutimilika kwa kutia alama na kuchinja kama ilivyoandikwa katika Ezekieli 9 na Ufunuo 7:3-8; 14:1-5 mtawalia, na katika Shuhuda kwa Wachungaji, uk. 445, Shuhuda, Gombo la 3, uk. 266, pia Maandishi ya Awali, uk. 270-273. {TN3: 86.1}

Baada ya malimbuko kutiwa muhuri na magugu kuondolewa kati yao, wakiwa wakati huo wametengwa na mvuto wa dunia, jinsi walivyokuwa watu 120 siku ya Pentekoste, watapokea kumwahwa kwa “Roho Mtakatifu” kwa kipimo kikubwa zaidi, kadiri ongezeko la uovu hudai mwito zaidi wa uamuzi kwa toba.” — Shuhuda, Gombo la 7, uk. 33. {TN3: 86.2}

Malimbuko ya wafu (120) likiwa kundi lililohesabiwa, na mavuno ya pili ya wafu (umati wa watu waliokusanywa baada ya Pentekoste) wakiwa kundi lisilohesabiwa, vivyo hivyo lazima iweze kuwa na malimbuko na mavuno ya pili ya walio hai. Hivyo kutiwa muhuri watu 144,000 malimbuko; na hivyo “baada ya hayo,” asema Yohana, “nikaona na tazama, umati mkubwa,

86,

ambao hapana mtu awezaye kuuhesabu, watu wa kila taifa, na kabila, na jamaa, na lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya Mwana-Kondoo, wamevikwa mavazi meupe, wana matawi ya mitende mikononi mwao…. Na malaika wote walikuwa wakisimama pande zote za kile kiti cha enzi, na za hao wazee, na za wale wenye uhai wanne, nao wakaanguka kifulifuli mbele ya kile kiti cha enzi, wakamsujudu Mungu.” Ufu. 7:9, 11. {TN3: 86.3}

Maki kwa makini kwamba kundi hili kubwa lilisimama mbele ya kiti cha enzi, si kwa mwili, bali kwa mfano tu, jinsi linavyotazamwa katika Maandishi ya Awali, uk. 55, na kama linavyoshuhudiwa na ukweli maradufu kwamba (1) malaika “walisimama pande zote za kile kiti cha enzi na kuwazunguka wazee na wale wenye uhai wanne,” kuonyesha kwamba kundi kubwa lilikuwa nje ya mdwara wa malaika; na ya kwamba (2) uwepo wa malaika, wazee, na wanyama wanne karibu na kiti cha enzi huonyesha kwamba hukumu (Ufu. 4:2-6) ilikuwa bado katika kikao, na kwa hivyo, muda wa rehema ulikuwa haujafungwa. {TN3: 87.1}

Mitende mikononi mwa umati mkubwa (Ufu. 7:9, 11), na “mtende wa mshindi” uliowekwa “katika kila mkono” wa “jeshi lisiloweza kuhesabika la waliokombolewa” (Pambano Kuu, uk. 646), huonyesha kimbele matukio mawili tofauti kabisa: maana la mwisho lilipokea vyote “mtende wa mshindi na [kinubi] kinachong’aa,” ilhali la awali halikuwa na vinubi ila mitende tu. “Jeshi lisilohesabika la waliokombolewa” walipokea mitende na vinubi mbinguni, walipokuwa wakipanda katika “gari la mawingu,” na kabla tu kuingia katika mji mtakatifu. Umati mkubwa, hata hivyo,

87

walikuwa na mitende yao duniani, maana, jinsi tumeona, walikuwa nayo wakati wa hukumu ya upelelezi katika hekalu la mbinguni — kabla ya kufungwa kwa muda wa rehema. (Angalia Ufunuo 4 na 5; Fimbo ya Mchungaji, Gombo la 2, uk. 194-197.) {TN3: 87.2}

Dhahiri, basi, wakati mitende na vinubi vya majeshi ya waliokombolewa mbinguni ni tuzo halisi za ushindi, mitende ya umati mkubwa juu ya nchi ni mitende ya ushindi ya mfano. {TN3: 88.1}

Tukiwa hadi hapa tumejifunza mavuno kwa nuru ya Shuhuda za manabii, mifano, na sherehe, sasa tunaongozwa kuyatazama

Katika Nuru ya Tarakimu. {TN3: 88.2}

Ingawa waovu wanafagiliwa sasa katika mkondo ambao hawawezi tena kuepuka kuliko wanavyoweza kuuzuia au kuupinga, lakini hawawezi kuuona wala kuuelewa, kwa maana Neno pekee hivyo huangazia na kuiwezesha nafsi. Amebarikiwa kweli kweli mtu yule anayelifanya Neno kuwa taa ya miguu yake, na mwanga kwa njia yake (Zab. 119:105). Ndugu, Dada, Je, Neno hilo li katika mifano migumu kwako? Jibu lako litakuambia iwapo wewe ni wa wale wanaotembea katika nuru au wa wale wanaojikwaa katika giza, na uhusiano sahihi tu kwa Mungu unaweza kukuhifadhi salama kwa kundi moja na kukuweka nje ya lingine. {TN3: 88.3}

Iwapo unafikiri kwamba Kristo bila ishara alisalia siku 40 baada ya kufufuka, au

88

kwamba Roho Mtakatifu alishuka kwa watu 120 tu kwa sababu ilitukia walikuwa wengi; au kwamba hakika kwa bahati nasibu 12,000 kutoka kati ya kila kabila watatiwa muhuri; basi unaweza pia kufikiria ukweli kwamba 12 mara 12,000 sawa na 144,000 ni ajali ya hisabati! Kile tu unachofikiri kitakupa kipimo cha nuru iliyo ndani yako. {TN3: 88.4}

“Maneno Ninayowaambia,… Ni uzima.” Yoh. 6:63. {TN3: 89.1}

“Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.” Luka 4:4 {TN3: 89.2}

Kwa sababu tarakimu ni mtindo wa asili ya mifanano ya muda, Maandiko mara nyingi kwa hivyo huzitumia ili kufunua urefu wa muda kutoka kwa tukio moja la Biblia hadi kwa lingine. Hivyo, muda kutoka kwa kutikiswa mganda wa malimbuko hadi kwa Pentekoste ni sawa na kuzidisha idadi ya siku (7) zilizogawiwa kwa sherehe ya kwanza ya mavuno, sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu, kwa idadi ya majuma (7) hadi kwa Pentekoste, ambayo ni 7×7, au siku 49. Vile vile, muda kutoka Yubile moja hadi nyingine unapatikana kwa kuzidisha idadi ya miaka inayofanya mwaka wa sabato (7) na 7, miaka ya sabato, kutoa 7×7, au miaka 49. Wazi sana, basi, Maandiko kawaida hutumia mchakato wa kuzidisha katika kuufunua ukweli. {TN3: 89.3}

Bila shaka kwa baadhi, mfanano huu wa tarakimu utaonekana kuwa wa ajabu — ajabu kama wazo la dunia kuzunguka kwa

89

mhimili wake lilivyokuwa kwa ulimwengu wa Zama za Giza! Ni maajabu ya leo, hata hivyo, ambayo yanachukuliwa kama kawaida uhalisi wa kesho. Kwa hivyo, ingawa kwa wakati huu tunajua uchache wa tarakimu nyingi za Biblia na kanuni zake za ukweli zilizofichwa, haitakuwa hivyo daima, maana Mungu ameziweka kwenye njia kuu na ndogo za Ukweli wa Biblia, kama ishara zilizokusudiwa kuonyesha na kuiangaza Barabara ya Kifalme hadi kwa Ufalme. Hivyo kila msafiri kwazo afurahi kwa shukrani ya ndani kwa kila nuru ya ukweli inayoiangaza njia yake. Hebu Bwana akataze kwamba mtu yeyote asichukue nafasi hata ndogo gizani. Na kila mmoja aweze kwa vinywa visivyo na unafiki aililie mbingu: “Niletewe nuru Yako na kweli Zako: ziniongoze; Zinifikishe kwenye Mlima Wako mtakatifu na hata maskani Yako.” (Zab. 43:3) ili Niweze “kujazwa na maarifa ya utukufu wa Bwana” (Hab. 2:14), naam hata kufahamu

Tarakimu ya Mwokozi. {TN3: 89.4}

Ukweli kwamba Kristo baada ya kufufuka alisalia pamoja na wanafunzi Wake siku 40 tu, si zaidi au pungufu, si tukio la bahati nasibu la kupuuzwa. Bila shaka ni sehemu muhimu ya muundo wa juu wa ukweli wote uliofunuliwa, unapaswa uhesabiwe ipasavyo. Na kwa sababu mfumo wake ni wa tarakimu, somo lote linalohusika linapaswa kuchunguzwa kwa tarakimu, na matokeo kulinganishwa katika thamani za tarakimu. {TN3: 90.1}

Bwana akiwa mwakilishi anaye-

90

onekana wa Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, basi tarakimu ya ofisi Yake binafsi (3) na tarakimu ya siku (40) ya usimamizi Wake binafsi katika kuwakusanya watu Wake lazima, kwa usawa sahihi, imfunue Yeye kama Mwokozi wa watu Wake katika kipindi cha Agano la Kale na pia Jipya. {TN3: 90.2}

Kama kuwakusanya (40) kwa njia ya uwepo Wake binafsi (3) kulisababisha kumiminwa kwa Roho Mtakatifu, haya mawili lazima katika uhusiano sahihi yafunue

Idadi ya Watakatifu kwa Pentekoste. {TN3: 91.1}

Zao la Kristo kuwakusanya kwa njia ya uwepo Wake binafsi kuwa ni malimbuko hadi Pentekoste, kisha inafuata kama mlolongo wa busara kwamba zao la tarakimu ya muda wa kukusanya (40) na tarakimu ya nafsi Yake (3), lazima itoe tarakimu halisi ya watakatifu waliokuwapo siku ya Pentekoste. Mlingano, 40×3, kupeana 120, kwa uhalisi ni idadi ya malimbuko ambao wangepokea Roho Mtakatifu wakati huo! {TN3: 91.2}

Hivyo kuwa jinsi walivyokuwa zao la uwezo wa mwenyezi wa utatu wa Uungu (Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu) wakifanya kazi kwa siku 40 kupitia huduma ya binafsi ya mwakilishi wao wa utatu. Kristo, kikundi hiki kidogo cha ajabu hivyo kilihifadhi na kuendeleza safu ya kanisa. {TN3: 91.3}

Ukipunguzwa kwa maana yake ya msingi,

91

mfululizo huu wa ukweli wa tarakimu huongoza kwa hitimisho kwamba 3, idadi ya Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, kwa hivyo ni mfano wa Utatu, na ya kwamba 120, tarakimu ya Baba, Mwana, Roho Mtakatifu ikizidishwa kwa idadi ya watakatifu, kwa hivyo ki-tarakimu ni mfano wa Pentekoste — jambo la msingi katika usawa wa wokovu, na moja lisiloweza kutenganishwa limelinganishwa kwa uhusiano wa

Kristo na Biblia. {TN3: 91.4}

Ilikuwa kwa Kristo katika maumbo Yake mawili ambayo Yohana aliguzia katika matamshi yake: “Lile lililokuwako tangu mwanzo, tulilolisikia, tuliloliona kwa macho yetu, tulilolitazama, na mikono yetu ikalipapasa, kwa habari ya Neno la uzima.” 1 Yoh. 1:1. “Naye Neno alifanyika mwili,” anasema tena, “akakaa kwetu; nasi tukauona utukufu Wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba; amejaa neema na kweli.” Yoh. 1:14. {TN3: 92.1}

Kristo ni Neno katika mwili; Biblia ni Neno lililoandikwa; au, kulifanya kihususa zaidi, Biblia ni Kristo katika umbo la maneno, na Kristo ni Biblia katika umbo la mwanadamu. Kwa hivyo inafuata kwamba kama Kristo katika mwili ametambuliwa kwa tarakimu, hivyo ni lazima Kristo katika Neno. Na kwa hivyo ijayo kuhakikishwa ni

Tarakimu ya Biblia. {TN3: 92.2}

Mfano wa mwito wa saa ya kumi na moja (Mathayo 20) huonyesha kwamba Biblia inazo

92

jumbe 5 tu za wakati; wa kwanza “mapema asubuhi,” wa pili “saa ya tatu.” Wa tatu kwa “saa yasita na wa nne saa ya tisa,” na wa tano kwa “saa ya kumi na moja”; zote 5. Katika wito huu 5 wa kimfano hupatikana jumbe zote za wakati zinazotajwa katika Biblia tangu wakati ambapo (Nuru ya ulimwengu) ilianza kuchomoza (kuandikwa), mapema asubuhi ya kipindi cha mfano, hadi mwisho wake — saa ya kumi na mbili. Kwa maneno mengine, wakati jumbe hizi 5 zikishatangazwa kwa ulimwengu, Biblia itakuwa kitabu kilichoisha kabisa maadamu hakitakuwa kinatoa lolote kwa ajili ya wokovu. (Kwa ufafanuzi kamili wa Mathayo 20, angalia Fimbo ya Mchungaji, Gombo la 2, uk. 222-238.) {TN3: 92.3}

Zikiwapo, basi, jumbe 5 tu za wokovu katika Biblia, tarakimu ya Biblia inaweza tu kuwa 5, na hatua inayofuata kuwa kupata

Tarakimu ya Wakati wa Kukusanya wa Biblia. {TN3: 93.1}

Kwa sababu tarakimu hii ni kuonyesha wakati wa kuwakusanya watakatifu, kwa hivyo ni lazima tuzidishe tarakimu ya watakatifu kwa Pentekoste (120) na tarakimu ya Biblia (5), ambayo ni 600. Kwa hivyo, 600 ni tarakimu ya wakati wa kukusanya ya Biblia — kipindi ambacho kama sababu katika mlingano wetu inaongoza ufuatano kwa

Tarakimu Ya Miaka Kristo Ni Mwokozi. {TN3: 93.2}

Hebu ukweli uhifadhiwe vyema akilini kwamba sisi

93

sasa tunachunguza tarakimu kwa ukweli kwamba Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu kabla na nyakati za Biblia. Kwa hakika lengo letu ni kupata, si idadi ya watakatifu ambao Kristo ataokoa, ila idadi ya miaka Atakuwa Mwokozi. Kwa hivyo, sisi hapa tunamkumbusha msomaji kwamba wito wa kimfano, au jumbe za Mathayo 20 zinakumbatia tu sehemu ya historia ya kanisa; hasa, sehemu ile tangu wakati Musa alipoanza kuandika Biblia, tangu wakati wa “Kutoka,” hadi kufungwa kwa muda wa rehema. Basi kama Kristo ni Mwokozi wa ulimwengu kabla na baada ya ujio wa Biblia, usawa chini ya majadiliano lazima vile vile ukumbatie muda wote wa rehema tangu siku Adamu alitenda dhambi. Hii inadai kwa hivyo idadi ya muda wa rehema, 600, kizidisho, kizidishwe kwa kizidisho kinachomiliki thamani ya ulimwengu wote, kuonyesha kwamba Kristo ndiye Mwokozi wa pekee katika vizazi vyote. {TN3: 93.3}

Namba 10 ni kwa ukiri wa ulimwengu wote kwamba ni tarakimu ya Kibiblia ya thamani ya ulimwengu wote. Katika sanamu kubwa ya Danieli 2, vidole 10 huashiria dunia wakati wa ujio wa pili wa Kristo. Kisha katika kiitwacho eti mnyama dubwana (Danieli 7), mnyama kama chui (Ufunuo 13:1-10), na mnyama mwekundu sana (Ufunuo 17:1-3), pembe 10 huonyesha falme za ulimwengu katika nyakati tofauti. Ambapo kwa upande mwingine wa picha, wanawali 10 huwakilisha washiriki wote wa kanisa ulimwenguni kote. (Kwa ufafanuzi zaidi wa tunu hizi, angalia

94

Fimbo ya Mchungaji, Gombo la 2, uk. 84-125.) {TN3: 94.1}

Wazi wazi, kwa hivyo, tarakimu ya ulimwengu ambayo tunapaswa kuzidishia namba ya muda wa rehema (600) ni 10, na 600×10 hutoa 6,000. Hapa mwishowe ni uthibitisho mkamilifu wa imani ya Kikristo kwamba miaka ya rehema kwa wanadamu ni 6,000! Hapa, kwa maneno mengine, ni uthibitisho kabisa kwamba wakati malaika wa rehema punde mwishowe anakunja mabawa na kuruka milele kutoka ulimwengu huu wa dhambi, dunia na viumbe vyake chini ya dhambi itakuwa imekuwapo kwa miaka 6,000! Halafu inakuja millenia, miaka 1,000 ambapo Shetani atafungwa na waovu kuhukumiwa (Ufu. 20:3, 12). {TN3: 95.1}

Hivi katika sarakasi ya milele, kuingia kiajabu kwa dhambi na ukombozi itafika kwa miaka 7,000 (ukamilifu kamili), au ama juma moja fupi nje ya umilele, kama ilivyo kwa Bwana, miaka 1000 ni kama siku moja Kwake (2 Pet. 3:8). Kuingia kiajabu hakika! Siri ya Uungu katika uvumilivu wa ajabu kwa siri ya kuasi! Fumbo la mafumbo! Wa ajabu, upendo usioeleweka wa Mungu kwa mwanadamu! {TN3: 95.2}

Ni wa kutisha kama nini huwekeza wonyesho huu mkubwa wa hisabati wa kweli kuu za injili! Zinavyofunua jinsi zinavyofanya kwamba Kristo ndiye Mwokozi pekee wa ulimwengu na kwa vizazi vyote, ukweli wake kwa ukamilifu unainua andiko: “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.”

95

Mdo. 4:12. Na kwa wakati uo huo linatoa onyo kwamba tunaishi katika siku za mwisho za rehema, “wakati wa mwisho,” wakati wa mavuno. {TN3: 95.3}

Baada ya kutuleta hadi wakati wa mavuno ya walio hai, hadi siku za mwisho za miaka 6,000 ya rehema ya wanadamu, mlingano lazima, uwe umekamilika, unajumuisha tarakimu ya

Waliohesabiwa Watakatifu Walio Hai. {TN3: 96.1}

Pentekoste ya mitume, ni lazima ieleweke, haikutimiza kabisa Pentekoste ya unabii wa Yoeli 2:28, 32, unabii maalum wa siku za mwisho, ingawa Petro alirejea kwa maandiko katika mahubiri yake ya Pentekoste (Mdo. 2:14-21). Na uthibitisho wa kweli kuwa unabii bado utatimizwa ni kwamba Pentekoste ya mitume ni ya mfano-pacha wa siku ya mwisho, Pentekoste ya uakisi ambayo haswa i mbele yetu. {TN3: 96.2}

Maadamu kanisa kwa dunia limekuwa na vipindi vitatu, cha Nuhu, cha Abrahamu, na cha Ukristo, na kwa kuwa vyote cha Abrahamu na cha Ukristo vilifunga na Pentekoste, kama ilivyoelezwa awali, ni lazima, basi, vivyo hivyo kuwa kilifunga hivyo kipindi cha Nuhu. Vinginevyo, ujumbe wa Nuhu ungekosa uwezo na nuru kuonyesha Njia ya Uzima kwa hicho “kizazi kiovu na kizinzi,” na kama tokeo Mungu asingalikuwa amewaangamiza kwa haki kwa gharika. {TN3: 96.3}

Petro mwenyewe alielewa kwamba ilikuwapo

96

Pentekoste kabla ya gharika ya Nuhu. Hili analishuhudia dhahiri kwa maneno haya: “Kwa maana Kristo….akiwa ameuawa katika mwili, bali roho yake akahuishwa, ambayo kwa hiyo Yeye aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa.” 1 Pet. 3:18-20. {TN3: 96.4}

Katika taarifa ya Petro, Uvuvio hurekodi kwamba Roho yule Aliyemfufua Kristo, aliwahubiria walioishi kabla ya gharika ya Nuhu wakati walipokuwa gerezani — katika minyororo ya hali ambazo katika uovu wao na kukataa ukweli walighushi kwa upofu na kujifungia wenyewe na ambao hawangaliweza kuokoka isipokuwa kupitia safina ambayo ilikuwa “inatengenezwa.” Na ile safina, hawakuingia. Hivyo waliachwa bila tumaini na bila udhuru. {TN3: 97.1}

Wazi wazi, basi, zipo Pentekoste tatu za kuhesabu katika mlingano wa wokovu: mbili zamani na moja ya siku za baadaye, ya kwanza ikiwa ni mfano, ya pili mfano-pacha, ya tatu ya uakisi. Au, kwa maneno mengine, ya kwanza ilileta juhudi za kuanzishwa kwa kanisa, ya pili msingi wa kanisa (Ufu. 21:14), na ya tatu italeta kukamilika kwalo na utukufu. Ya pili, Pentekoste ya mitume, ikiwa ya msingi, pia ni ya pekee iliyonakiliwa kihistoria, kwa hivyo ni mbeba nuru kwa somo hilo; kuonyesha kwamba ili

97

ulimwengu wa kabla ya gharika ya Nuhu kufaidika kwa ukombozi, Pentekoste ya Nuhu ilikuwa muhimu na lazima iweze kuzingatiwa katika utafiti huu wa tarakimu. {TN3: 97.2}

Tarakimu ya watakatifu kutoka kwa ile iliyonakiliwa ikiwa 120, inafuatia kwamba tarakimu ya mbili mseto lazima iwe 120 jumlisha na 120, au 240, jinsi ilivyoonyeshwa kwenye ukurasa wa 77. {TN3: 98.1}

Kumbuka kwamba tarakimu hizi hazihakiki ni wangapi wanaokolewa katika kila moja, ila ni wangapi wanapokea nguvu za Pentekoste. {TN3: 98.2}

Inasalia sasa lakini kuhakiki idadi ya watakatifu watakaopokea Pentekoste ya tatu na ya mwisho, na kufanya hivyo idadi ya Pentekoste mbili (240) inahitaji tu kuzidishwa kwa tarakimu ya wakati wa kukusanywa wa Biblia (600), kufanya 600×240, ambayo inatoa 144,000, tarakimu haswa iliyotabiriwa! {TN3: 98.3}

Hivyo imegonga katika mwamba wa ukweli milele ni tarakimu ya watakatifu watakaopokea Pentekoste kubwa iliyo mbele yetu, tarakimu ya malimbuko ya wale watakao badilishwa bila kufa, 144,000 wasiokuwa na hila (Ufu. 14: 5), “watumwa wa Mungu wetu.” Ufu. 7:3. Katika uwezo safi na kamili wa Roho, wakitangaza Injili safi na kamili kwa mataifa yote, wao “wanakwenda mbele wakishinda na kushinda” (Manabii na Wafalme, uk. 725), nao “watawaleta ndugu zenu wote kutoka mataifa yote, kuwa sadaka kwa Bwana, juu ya farasi, na katika magari, na katika machela, na juu ya nyumbu, na juu ya wanyama wepesi, mpaka mlima Wangu mtakatifu Yerusalemu,

98

asema Bwana; kama vile wana wa Israeli waletavyo sadaka yao nyumbani kwa Bwana katika chombo safi. “ Isa. 66:20 “hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.” Mat. 24:14. {TN3: 98.4}

Hivyo, kwa njia ya kusisimua imefunuliwa kwa tarakimu, hali tumizi kamili ya ukweli kabisa, ni mlingano wa wokovu, ambao kutoka kwa huo, kwa ufupi kurudia, huibuka Tarakimu ya Kristo kama mwakilishi wa Uungu kwa dunia, 3; tarakimu ya wakati wa kukusanya, 40; tarakimu ya watakatifu katika Pentekoste ya mitume, 120; tarakimu ya mseto wa watakatifu katika Pentekoste ya Nuhu na ya mitume, 240; tarakimu ya Biblia, 5; tarakimu ya wakati wa kukusanywa ya Biblia, 600; tarakimu ya watakaopokea Pentekoste ya mwisho, 144,000; tarakimu ya muda wote wa rehema ya wanadamu, 6,000; na mwisho, tarakimu ya wakati wote wa dhambi na ukombozi, 7,000. Kipawa kilioje cha Munguchenye thamani! Na O ufahamu huu uchochee moyo wa kila msomaji wa bidii, jinsi ulivyoufanya moyo wa Daudi, kutoa sifa na shukrani kwa Mungu kwa upendo Wake usioelezeka kwa mwanadamu: “Ee Bwana,” anaimba nabii, “wewe u Mungu wangu; Nitakutukuza na kulihimidi jina Lako; Kwa kuwa umetenda mambo ya ajabu, Mashauri ya kale, kwa uaminifu na kweli.” Isa. 25:1. {TN3: 99.1}

Hivyo kwa ushuhuda wa manabii, kwa mfano, kwa vivuli vya sherehe, na kwa tarakimu, Mungu ametengeneza muundo imara wa ukweli kwamba (1) hukumu ni mavuno, —

99

utengo wa magugu kutoka kwa ngano — mwisho wa dunia; kwamba (2) hukumu, mavuno, hukumbatia awamu mbili, vipindi viwili; cha awali kwa wafu, cha mwisho kwa walio hai kwamba (3) moja hufanyika kulingana na kumbukumbu vitabuni katika hekalu la mbinguni, ilhali ile nyingine hufanyika sambamba kanisani kwa dunia na katika vitabu mbinguni; na ya kwamba (4) ukweli hasa kwamba somo hili sasa linafunuliwa katika ukamilifu wake unathibitisha kwamba tuko karibu tu ukingoni mwa kupita awamu ya awali na kuingia awamu na kipindi cha mwisho, naya kwamba tunaishi kwa hivyo katika siku za mwisho za historia ya dunia. {TN3: 99.2}

Mtazamo huu mara nne wa hukumu, mavuno, hivyo huinua ukweli wake kama lulu ya thamani kubwa, na hufunua kwamba kina cha Neno la Mungu hakiwezi kupimwa; Hekima Yake haiwezi kukaguliwa na ni ya milele bila mwanzo wala mwisho; Hazina Yake ya maarifa ni chemchemi endelevu ya ukweli; Uwepo Wake hudumu daima; na uzuri Wake usiotamkika! {TN3: 100.1}

Sasa ya kwamba msomaji apate kuimarishwa kushika sana ukweli huu wa msingi na wa umuhimu wote, pamoja na kweli zingine zote, tunamhimiza kufuata njia ya Mungu (Uvuvio) katika kujifunza Maandiko, ili aweze hivyo

Kuepuka Mitego Mingi. {TN3: 100.2}

Labda kwanza kabisa miongoni mwa umati wa watu ambao wamenaswa wakati wanafanya yote wanayoweza

100

kukimbia mbali kutoka kwa ufasiri uliovuviwa wa Maandiko ni wale wenye msimamo mkali, ambao wapo angalau matabaka mawili: moja la mwelekeo wa kufasirimoja kwa moja, lingine la mwelekeo wa kutoa maana ya kiroho. {TN3: 100.3}

Chukua kwa mfano taarifa ya Waufunuo: “…. nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu,…. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi?” Ufu. 6:9, 10. {TN3: 101.1}

Wale wa kufasiri moja kwa moja kwa upande mmoja, wangeweza kuyafasiri maandiko haya kwa maana ya kwamba roho walikuwa na ufahamu na kwa kweli walilia, ingawa Biblia i wazi kabisa kwamba “wafu hawajui neno lolote.” Muh. 9:5. Na pia, laiti nafsi zilizokuwa chini ya madhabahu zingalikuwa zinalia hakika kwa ajili ya kisasi dhidi ya wauaji wao, basi, kuwa yenye upatano, maneno ya Bwana, “Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi” (Mwa. 4:10) , pia taarifa, “Na miti yote ya kondeni itapiga makofi.” (Isa. 55:12), pia inapaswa kufafanuliwa kuwa moja kwa moja licha ya ukweli kwamba haiwezekani hakika kwa ajili ya damu kulia na miti kupiga makofi. {TN3: 101.2}

Ikiwa wote, hata hivyo, wanahitajika kukubali kwamba damu ya Abeli haikulia hakika,

101

na ya kwamba miti inaweza tu kimfano kupiga makofi, basi, tena kuwa thabiti, mtu aliyezoea uhalisi uliokithiri atashikilia kwa wepesi uhalisia kwamba “wafu hawajui neno lolote,” na kwamba “wamelala” — hawana ufahamu. Anapaswa, pia, kwa urahisi kukisia kwamba roho za walioifia imani hulia kwa ajili ya kisasi juu ya waliowaua, na kwamba damu ya Abeli inalia kwa ajili ya kisasi kwa aliyemuua, ni kesi sawa zinazofanana katika hali na jambo. Yote mawili hupata mfano ulio wazi katika usemi wa shairi: “Nasikia sauti ikilia, sauti ya shamba linalonyauka: Ee Bwana, Nihurumie. Acha mvua inyeshe kutoka mbinguni. Uitulize nafsi yangu inayoungua.” {TN3: 101.3}

Kwa nafsi ya mtu kufungwa akiwa na fahamu chini ya kitu kwa mamia ya miaka, bila kufanya chochote ila ikiugua kwa kuteseka ikisubiri asubuhi ya ufufuo, huku ikiendelea kulia kwa ajili ya kisasi kwa wale waliomwaga damu ya mtu, — ni hali gani isiyoweza kuelezeka na kuvumilika kwa nafsi ya mtu kuwa ndani yake! {TN3: 102.1}

Fundisho, hata hivyo, la hali ya wafu kutokuwa na fahamu si tu huweka kwa amani akili yenye hofu ya kibinadamu lakini pia humhesabia Mungu kuwa wa huruma na wa upendo kwa wanadamu wasioweza kujisaidia, hivyo kuwa msimamo wa pekee kwa swala hilo ambao unaweza kumfanya mdhambi kwa busara kumpenda Mungu na kumtegemea Yeye. {TN3: 102.2}

Kwa yule ambaye kwa upande mwingine ana mtazamo wa kinyume, kufanya

102

kiroho, mchinjo, mbingu, dunia mpya, nk., — kwake yeye haya si ya moja-moja wala halisi. Na mintarafu fundisho la mchinjo anaulizwa swali rahisi, Ni aina gani ya mchinjo ingekuwa ya kiroho? Anapata hasara kujibu! {TN3: 102.3}

Kwa wote, lipo katika mwungano huu hitaji moja kuu: Roho wa Kweli, Ambaye ni haki Yake pekee kuyafasiri Maandiko. {TN3: 103.1}

Chanzo cha kawaida sana cha mkanganyiko wa mafundisho miongoni mwa wanafunzi wa Biblia huwa ndani yao mara kwa mara kushindwa kuiangalia mada kwa picha kamili kutoka kwa mtazamo wa mwandishi, — kushindwa ambako husababisha wao kuuona kutoka kwa baadhi ya maoni ya kigeni kupunguza kwa ufinyu mtazamo wao kuwa badala ya kupata wazo la mwandishi kwa mada, wao hupata wazo la uongo kwayo. Na iwapo wazo hilo litakuwa la kuwavutia, wanalitukuza na kwa juhudi kuliendeleza kama ukweli, ilhali iwapo haliwapendezi, wanalipinga kwa dhati, kisha kuweka lawama kwa mwandishi! {TN3: 103.2}

Kuonyesha hivyo kupata wazo kombo la kitu kutoka kwa kukitazama vibaya: mtoto ambaye huambatana pamoja na mamaye kwenye hifadhi ya wanyama, na ambaye hajawahi kumwona tausi, ghafla anamfikia mmoja akiwa ameeneza mkia mzima akienda mbali kutoka kwake, na kufanyiza kwa macho yake yasiyofahamu wazo la upepeo mkubwa unaotembea! {TN3: 103.3}

103

[Picha ya Tausi aliyeeneza Mkia Mzima]

Akiwa na furaha kwa wazo la ajabu mbele yake kwa msisimko anashangaa kuona, ila akiwa na mama yake alimzindua asijihusishe na kifumba macho kwa kumhakikishia kwamba ni tausi tu! Katika hafla nyingine, hata hivyo, wakati akiambatana na baba yake kwenye hifadhi ya wanyama, mtoto huyo anamwona tena tausi, lakini mara hii kwa mtazamo kamili wa mbele akionyesha taswira inayoonekana mpya na tofauti kabisa. Upesi anarudi na maswali ya msisimko kwa baba yake, ambaye anamwambia kwamba ni tausi! {TN3: 104.1}

104

[Picha ya Tausi kwa Mtazamo kamili wa mbele]

Kisha ubishi unaanza, mtoto akiteta kwamba tausi ambaye yeye na mama yake walimwona, hakuonekana kama huyu. Na kwa kutoweza kupatanisha, kama tu sehemu kuu na ndogo za kitu kile kile, ambacho anakiona sasa kutoka mbele, au mtazamo mkuu, na kile alichokiona kutoka nyuma, au mtazamo wa kigeni, akili zake zinapapasa katika kuchanganyikiwa akishangaa iwapo amwamini Baba au Mama. {TN3: 105.1}

105

Ndivyo ilivyo kwa Biblia wakati mtu analiangalia somo kwa mtazamo wa kigeni kutoka kwa ule wa mwandishi. Hupata kasoro katika msimamo unaoshikiliwa na yule anayeliona somo kupitia macho ya mwandishi. Kwa hivyo ili, kudumisha wazo la uongo linalosababishwa na mtazamo wake wa kigeni, anaongozwa kuvitumia vyanzo vya nje: kwa msemaji mmoja au mwingine; kwa toleo hili au kwa lile; kwa ustadi na kuzilinganisha lugha: kwa Kiyunani, kwa Kiebrania, kwa hii, kwa hiyo, au kwa nyingine (lugha, hakuna ambayo yeye mwenyewe inawezekana asome aidha kuandika); au kwa kurejelea hiki au kile kinachoitwa eti miswada halisi (ambayo yamkini hajawahi kuuona). {TN3: 106.1}

Mwishoni mwa barabara hii ndefu inayopinda-pinda, amefanikiwa tu kukuza kutoka kwa kilima cha fuko hadi mlima kifungu kimoja cha maandiko, na kupunguza kutoka kwa mlima hadi kilima cha fuko, au kuweka pembeni kabisa, kifungu kingine cha maandiko, yote kwa sababu Biblia, ambayo Bwana ameweka mikononi mwake, haiungi mkono wazo lake. Taratibu hizi za kujivuna zimekadiriwa kuonyesha mafanikio yake ya usomi kwa tumaini la kulipatia wazo lake la uongo kama umbo la kuonekana lenye mamlaka hivyo kulazimisha kukupokelewa na wote wanaokutana na nadharia yake. {TN3: 106.2}

Kwa uthabiti: Si haki wakati wa kulishughulikia somo la hukumu, kutoa kwanza kabisa upendeleo kwa maandishi yoyote ambayo yanahusika moja kwa moja na somo

106

la wokovu, ilhali kwa hiari tu kurejelea somo la hukumu. Chukua kwa mfano taarifa ya Paulo: {TN3: 106.3}

“Tumaini tulilonalo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, liingialo hata mle mlimo ndani ya pazia, alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki.” Ebr. 6:19, 20. {TN3: 107.1}

Badala ya kutazama maudhui ya mafungu haya katika nuru ya yote yaliyofunuliwa kwa somo hilo, utaratibu ambao utahakikisha aya zinazoakisi wazo la mwandishi, baadhi ya wanafunzi wa Biblia, kwa kukosa kuona lengo la mtazamo wa Paulo, wanakuza nje ya yote uwiano muhimu upasao wa taarifa ya aya hizi, hivyo kuweka kwazo ujenzi ambao, ingawa unaaminika wa kutosha wakati unachukuliwa peke yake ni dhahiri huharibu, hupotosha, na hukanganyana unapotazamwa kwa nuru ya maandiko mengine yote yanahusu hilo somo. Kupotosha kwa jinsi hii, bila shaka, ni ukosefu wa haki kwa mwandishi, hatari kwa yule aliyeathirika, na uhalifu wa anayepotosha. {TN3: 107.2}

Kuonyesha jambo hili zaidi na kwa upana zaidi: Kuizingira meza ni wanafunzi sita wa Biblia na kafiri. Kwa upande mmoja ni Petro Yakobo, na Yohana; kwa upande mwingine, Black Brown, na Green; ilhali upande mmoja ni kafiri. Anawasikiliza kwa makini wale sita wakijadili ukasisi wa Kristo

107

baada ya kupaa Kwake, katika nuru ya Waebrania 6:19 20; 9:12, 26 — {TN3: 107.3}

“Tumaini tulilonalo kama nanga ya roho, yenye salama, yenye nguvu, liingialo hata mle mlimo ndani ya pazia, alimoingia Yesu kwa ajili yetu, mtangulizi wetu, amekuwa kuhani mkuu hata milele kwa mfano wa Melkizedeki.” Ebr. 6:19, 20 {TN3: 108.1}

“Wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu Yake mwenyewe Yeye aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele.” Ebr. 9:12. {TN3: 108.2}

“Kama ni hivyo, Yeye ingalimpasa kuteswa mara nyingi tangu kuwekwa msingi wa ulimwengu: lakini sasa, mara moja tu, katika mwisho wa dunia, amefunuliwa, azitangue dhambi kwa dhabihu ya nafsi Yake.” Ebr. 9:26. {TN3: 108.3}

Petro, Yakobo, na Yohana, wakishiriki mtazamo wa mwandishi, wanakubaliana kabisa kwamba mtu hawezi, kwa maandiko yanayoelezea wokovu, na kwa hiari tu kurejelea ukasisi wa Kristo, kujenga msingi sahihi wa kuelewa ukasisi huo, ila badala yake lazima huyo ayachukue maandiko ya manabii ambayo yanahusika moja kwa moja na hekalu na ukasisi wake, na kisha kuoanisha maandishi ya Paulo kwa ya manabii ‘, si ya manabii’ kwa ya Paulo. {TN3: 108.4}

Hadi hapa Petro, Yakobo, na Yohana wanavyohusika majadiliano yanasababisha

108

kufikia hitimisho kwamba Paulo, ili awe na upatano na yeye mwenyewe na manabii, lazima aeleweke katika Waebrania 6:19 kwamba anazungumza katika wakati wa kinabii uliopita (yaani, baadaye hakika, ingawa kiambishi cha sasa au wakati uliopita) na kwamba kwa hivyo anaonyesha wakati ambao waongofu wake wako, pamoja na Kristo, “mara moja tu, katika mwisho wa dunia” (Ebr. 9:26), kuingia “ndani ya pazia,” “alimoingia Yesu [Kristo] kwa ajili yetu, mtangulizi wetu.” Ebr. 6:20. Lini? — si wakati wa Paulo lakini sasa, “mwishoni mwa dunia,” Yeye akiwa kwanza “aliingia mara moja tu katika Patakatifu.” Ebr. 9:12. {TN3: 108.5}

Black, Brown, na Green, hata hivyo, kutoka kwa mtazamo wao wa kigeni kwa mafungu haya, hawakubaliani hata miongoni mwao wenyewe: Black anasisitiza Waebrania 6:19, 20, ameshawishika kuwa Paulo hufundisha kwamba Kristo aliingia ndani ya Patakatifu Mno mara baada ya kupaa Kwake; Brown, akizingatia Waebrania 9:12, ni hakika kwamba Kristo aliingia, si Patakatifu Mno, ila patakifu; na Green, kwa uzito wa fungu la 26, anasisitiza kwamba Kristo ataingia patakatifu “mara moja katika mwisho wa dunia,” baada ya ujio Wake wa pili. {TN3: 109.1}

Bado akiona kutoka kwa mitazamo yao ya kigeni, Black anahoji zaidi kwamba kwa neno, “patakatifu,” Paulo anamaanisha “Patakatifu mno,” ilhali Brown anateta kwamba iwapo Paulo anatumia kwa ulegevu neno “patakatifu” kumaanisha “Patakatifu mno,” “basi mtu anawezaje kujua kwamba wakati anasema “Patakatifu mno,” hamaanishi “patakatifu”? {TN3: 109.2}

109

Kisha kwa uzito wa maneno ya Musa: “Sema na Haruni ndugu yako, kwamba asiingie wakati wo wote katika mahali patakatifu ndani ya pazia, mbele ya kiti cha rehema, kilicho juu ya sanduku” (Law. 16:2). Black tena anashikilia kwamba Paulo, kwa maneno, “bali kwa damu Yake mwenyewe aliingia…katika patakatifu” (Ebr. 9:12), hurejelea kwa “Patakatifu mno” Ebr. 9:3. Lakini Petro anasisitiza kwamba kuelewa matumizi ya Paulo ya neno “patakatifu” kumaanisha “Patakatifu mno,” yote ni upumbavu na yasio haki, maana hakuna mwandishi wa akili timamu, akizungumza kuvihusu vyumba vyote, atageuza kiholela maneno hayo, na bado atarajie wasomaji wake kwa usahihi kuelewa wazo analolitoa. Black, hata hivyo, anadakia kwamba Musa hutumia neno “mahali patakatifu” (Law. 16:2) anapozungumza kukihusu chumba cha pili. {TN3: 110.1}

Katika kujibu hili, Petro anateta kwamba Musa hufanya hivyo kwa sababu anapoita chumba cha pili “patakatifu ndani ya pazia,” hukiita chumba cha kwanza “hema ya kukutania” (Lawi. 16:16), ilhali Paulo huchagua kukiita chumba cha kwanza “patakatifu,” na chumba cha pili, “Patakatifu mno.” {TN3: 110.2}

Tena: Petro husizitiza kwamba iwapo, katika maandishi ya Paulo, ambapo vyumba vyote vinajadiliwa, mmoja ahalalalishwe kufasiri “patakatifu” kumaanisha “Patakatifu mno,” kisha mwingine, kwa ishara hiyo ya mantiki, ahalalishwe pia kufasiri “Patakatifu mno” kumaanisha “patakatifu.” {TN3: 110.3}

110

Ijapokuwa mantiki ya wazi ya Petro imepunguza kabisa nguvu ya ushindani wa Black, hata hivyo, kwa sababu ya tofauti kubwa ya maoni kati ya kikundi cha waamini wa Kikristo, matokeo ya mwisho ya majadiliano ni kwamba ule uwiano kati ya Petro, Yohana, na Yakobo ulichofanya kumwongoa kafiri kwa Ukristo, kuhitilafiana kwa Black, Brown, na Green, kati yao, pia Black kuhitilafiana na Petro, kukinzana. Mkorogo huu ulimfanya thabiti kafiri katika ukafiri wake, ukimwacha ameshawishika kikamilifu kwamba Ukristo ni bubujiko la kustaajabisha tu; na hapo Shetani, kwa furaha ya ukatili, huwapatia Black, Brown, na Green, “kiti chake, na mamlaka makuu.” Na Jumuia ya Ukristo, tayari imejaa kwa mchafuko wa mafundisho, inaendelea kutia maogofyo na ugomvi wa mafarakano, kuwalea makafiri katika uhasama wao kwa Ukristo, badala ya kuwaongoa! {TN3: 111.1}

Ikiwa Kristo hutangaza ole juu ya wale ambao hukataa kupeana bilauri ya maji baridi kwa wadogo wa wafuasi Wake, itakuwaje hukumu na mwisho wa kama Black, Brown, na Green, ambao, kwa roho yao ya kujikuza nafsi hutawanya kutoka kwa Kristo ilhali hudai kwamba wanakusanya pamoja Naye! {TN3: 111.2}

Kamwe si haki kuyafasiri maandiko yoyote yaliyotengwa kutoka kwa muktadha wake, kwa kufanya hivyo ni moja kwa moja kuivuruga maana yake. {TN3: 111.3}

Kwa mfano, maandiko, “Lakini, wapenzi, msilisahau neno hili,

111

kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja.” (2 Pet. 3:8) yakichukuliwa yalivyo, yamepata ufasiri mbalimbali, kuongeza tu kwa mchafuko na mashaka ambayo tayari yanaenea ulimwengu wa Kikristo. Lakini ufasiri mmoja pekee utaruhusu unapochukuliwa katika muktadha wake: “Mkijua kwanza neno hili ya kwamba katika siku za mwisho watakuja na dhihaka zao watu wenye kudhihaki, wafuatao tamaa zao wenyewe, na kusema, Iko wapi ahadi ile ya kuja Kwake? Kwa maana, tangu hapo babu zetu walipolala, vitu vyote vinakaa hali iyo hiyo, tangu mwanzo wa kuumbwa.” 2 Pet. 3:3, 4. {TN3: 111.4}

Kutoka kwa mpangilio huu wa ki-muktadha, twaona kwamba katika aya husika mtume anajaribu kwa lugha ya mfano kuonyesha kwamba wadhihaki aliowaona wangetokea katika siku zetu, ingawa wanajaribu kupindua imani ya wale wanaoamini katika simulizi la Musa la mafuriko na wanasubiri kurejea kwa Bwana, bila kujua wanaudhihaki upofu wao wenyewe. Kwa maana hawawezi kuona kwamba kile kinachoonekana kwao, kwa geji ya siku zao fupi walizoishi, uwepo wa kukawia daima wa ujio wa pili wa Bwana, kwa Yule wa Milele ila ni nukta inayopita upesi ya kusubiri, na kwamba hekima yao ya kininadamu kwa hivyo ni upumbavu. Na, kinyume chake, kile wanachokiona kama muda mfupi sana na usiokuwa na thamani kwa matumizi ya kweli, Bwana huona kama muda mrefu sana na wa thamani katika maisha yetu mafupi. {TN3: 112.1}

Dhahiri, kwa hivyo, wakati maandiko haya yanafasiriwa kulingana na muktadha wake, geji za

112

wanadamu za wakati zinaonekana kuwa si vipimo vya Mungu, kama tu mawazo ya kibinadamu si mawazo Yake (Isa. 55:7, 8). {TN3: 112.2}

Nuru ya mfano huu inaweka wazi kwamba kama vile valvu ya usalama ni muhimu kushikilia hodhi lisilipuke kwa shinikizo la ziada, hivyo kuangalia tu kwa uaminifu juu ya muktadha wa maandiko kunaweza kumzuia mfasiri wake kulipuka kwa nadharia na mawazo ya kigeni kwa Maandiko. {TN3: 113.1}

Wakati wale wanaopenda ukweli wanajifunza somo lolote la mafundisho, kamwe, katika kujaribu kulinganisha maoni yao binafsi na maandiko husika, huwa hawayaachi maandiko yakiwa yamefasiriwa kukinzana na sehemu zingine za Biblia au nafasi ya mamlaka ya sheria, ila badala yake huyaacha maoni yao. {TN3: 113.2}

Baada ya kuchukua mtazamo usiokuwa sahihi kwa mada ya hukumu, wengine hata hivyo pasipo kujua, walijaribu kwa kweli kubadilisha wakati wake sahihi na ilivyo kikweli badala ya kuidumisha. Jaribio hili la ulaghai limewaongoza kuwa na mitazamo mibaya kwa kweli zingine nyingi za Biblia. Ukweli, hata hivyo, kwamba hili fundisho la kitovu bado limebaki thabiti na imara, ni ushahidi usioweza kupingwa ambao pia yalivyo mafundisho ujukuti yake yote. {TN3: 113.3}

Wale ambao wameyafasiri Maandiko kwa wapendavyo bila Uvuvio, zoezi la kibinafsi ambalo ni

113

kinyume kwa agizo lililotolewa katika 2 Pet. 1:20, 21, na wale ambao wameyapokea maoni hayo, isipokuwa sasa waache makosa yao kwa ajili ya ukweli, siku moja watajikuta kuwa wahanga wa hali hatari ambayo wamejifungia wenyewe, na watafadhaishwa vikali watakaposikia tamko la kutisha: “Mimi sijasema nao, lakini walitabiri.” “ondokeni Kwangu, ninyi mtendao maovu.” Yer. 23:21; Mat. 7:23. {TN3: 113.4}

Waweze, kwa hivyo, ilhali rehema ingalipo na damu ya Kristo ingalipo kufidia dhambi za wote, “kutoa bidii zaidi kutii” tangazo la

Ujumbe wa Malaika wa Kwanza. {TN3: 114.1}

“Mcheni Mungu, na kumtukuza, kwa maana saa ya hukumu Yake imekuja.” Ufu. 14:7. {TN3: 114.2}

Ili kutanzua wakati uliowekwa rasmi kwa ujumbe huu, ni lazima tuzingatie kwamba kutoka sura ya nne hadi ya ishirini na mbili ya Ufunuo, mada yake ni endelevu. Hili linaonekana kutoka kwa kiunganishi “na,” ambacho, kuanzia kila sura, kinaonyesha kwamba mafunuo haya yote yalitolewa kwa Yohana wakati ambapo “Sauti” ilimwambia: “Panda hata huku, Nami nitakuonyesha mambo ambayo hayana budi kuwako upesi.” (Ufu. 4:1) — mambo ambayo yangetukia wakati mwingine baada ya kuwa na maono yake. Na Yohana alikuwa na maono haya karibu 96

114

B.K., ujumbe wa malaika wa kwanza kwa hivyo haingewezekana kuwa ulihubiriwa kabla ya wakati huo, kama wengine wanavyofikiri; maana, kurudia, hakuonyeshwa mambo yaliyopita, ila mambo ya siku za baadaye. {TN3: 114.3}

Tena; ukweli kwamba yeye husema, “Nikaona malaika mwingine [wa kwanza] …mwenye injili ya milele awahubiri,” huonyesha zaidi kwamba ujumbe wa malaika huyu ulikuwa haujahubiriwa kabla ya kuyapokea maono, lakini kwamba ungehubiriwa katika siku za baadaye kutoka wakati huo. {TN3: 115.1}

Hakuna, zaidi ya hayo, maandiko au historia ya kanisa kuonyesha kwamba hukumu ilianza kabla au wakati wa Yohana. Na bado zaidi, kama ujumbe wa malaika wa kwanza haukuwahi kuhubiriwa kabla ya 1844, basi wakati saa ya hukumu ilipokuja, ujumbe wa malaika huyu — ujumbe unaohusu hukumu — ukatangazwa. {TN3: 115.2}

Hukumu ya upelelezi ikiwa katika vipindi viwili (cha kwanza, kimetolewa kwa wafu, cha pili, kwa walio hai), ukweli unaonyesha kwamba ingawa ujumbe wa malaika wa kwanza, wa pili, na wa tatu (Ufu. 14:6-12) unahusika moja kwa moja katika kipindi cha hukumu ya walio hai, lazima pia, hata hivyo isivyo moja kwa moja, unahusika kwa kipindi cha hukumu ya wafu. Katika uhusiano huu tu, isipokuwa kama onyo la matukio yajayo, zimekuwa zikihubiriwa tangu 1844. Basi, wakati hukumu ya walio hai inapoanza na sanamu ya mnyama imetengenezwa, basi jumbe hizi, pamoja

115

na kilio kikuu, zitarudiwa kama ukweli wa sasa kwa walio hai badala ya wafu. {TN3: 115.3}

Hivi, zikiwa zimevutwa katika mtazamo mkali, kweli kuhusu kiti (cha utawala) cha enzi cha milele, kiti (cha upatanisho na hukumu) cha enzi cha muda, na hukumu, mwishowe huthibitisha msimamo uliowekwa na kitabu kilichotumiwa katika kutangazwa kwa jumbe za malaika wa kwanza, wa pili, na wa tatu katika matumizi yake ya kwanza, na ambayo kwa sauti ya mwandishi wake yanasema: {TN3: 116.1}

“Nalimwona Baba akiinuka kutoka kwa kiti cha enzi na katika gari la moto aliingia patakatifu pa patakatifu ndani ya pazia, na akaketi. Kisha Yesu akainuka kutoka kwa kiti cha enzi, na wengi wa wale waliokuwa wamesujudu waliinuka pamoja Naye. Sikuona mshale mmoja wa nuru kutoka kwa Yesu kwa kundi la wasiojali baada ya Yeye kuinuka, na waliachwa katika giza kamilifu. Wale walioinuka Yesu alipoinuka, walikazia macho yao Kwake alipoondoka kwenye kiti cha enzi na kuwaongoza nje kidogo. Kisha akainua mkono Wake wa kulia, na tuliisikia sauti Yake ya kupendeza akisema: “Subiri hapa; naenda kwa Baba Yangu kupokea ufalme; yatunze mavazi bila mawaa, na kitambo kidogo Nitarudi kutoka kwenye harusi na kuwapokea Kwangu. Kisha gari la mawingu, na magurudumu kama miali ya moto, likizungukwa na malaika, likaja alipokuwa Yesu. Aliingia ndani ya gari na akapelekwa hadi patakatifu mno, pale alipoketi Baba. Hapo nalimwona Yesu, Kuhani

116

Mkuu, amesimama mbele ya Baba.” — Maandishi ya Awali, uk. 55. {TN3: 116.2}

Uhamisho huu kutoka kwa kiti cha utawala hadi kwa kiti cha enzi cha upatanisho na hukumu, ukiwa umefanywa kuwapeleleza wageni wa harusi ambao sasa wamelala, unaongoza kwa yafuatayo

Maswali na Majibu. {TN3: 117.1}

1. Je! Kristo alihubiri kwa wafu?

1 Pet. 3:18-20.

“Kwa maana Kristo naye,” anajibu Petro katika maandiko yayo hayo yanayozusha swali hili, “Aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, Mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili Wake akauawa, bali roho Yake akahuishwa, ambayo kwa hiyo Aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka maji.” 1 Pet. 3:18-20. {TN3: 117.2}

Ni dhahiri kabisa, Petro hapa hasemi kwamba Kristo, wakati mwili Wake ulipokuwa umelazwa kaburini, alihubiri kwa roho gerezani, kama wanavyoelewa wengine; ila bali tu kwamba kupitia kwa Roho Ambaye Alimfufua, Aliwahubiria “katika siku za Nuhu, wakati safina ilikuwa inatengenezwa.” Wala haimaanishi kwamba Kristo aliwahubiria wafu, bali

117

“kwa roho zilizo gerezani.” Kwa hivyo, shaka kuhusu iwapo “roho zilizo gerezani” humaanisha wafu au walio hai. Ni swala la ufasiri, na ufasiri kama huu lazima uje kwa mamlaka ya Mungu. {TN3: 117.2}

Inapozungumza kuhusu wafu, Biblia kamwe haiwataji roho. Hufanya hivyo, lakini, kunena kwa walio hai. Huelezea waziwazi, zaidi ya hayo kwamba, “lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote lililofanyika chini ya jua.” Muh. 9:5, 6. {TN3: 118.1}

Bado zaidi, katika mfano wa mtu tajiri na Lazaro, Bwana hufanya wazi kabisa kwamba baada ya kifo mdhambi hana nafasi yoyote kwa ajili ya wokovu; Hapana, hata kwa tone la maji baridi juu ya ulimi wake, jinsi inavyokumbukwa kwa ushuhuda mtu huyo tajiri kukataliwa ombi lake katika kifo: “Mwanangu, kumbuka ya kwamba wewe uliyapokea mambo mema katika maisha yako, na Lazaro vivyo alipata mabaya; na sasa yeye yupo hapa anafarijiwa, na wewe unaumizwa. Na zaidi ya hayo, kati yetu sisi na ninyi kumewekwa shimo kubwa, ili wale watakao kutoka huku kwenda kwenu wasiweze; wala watu wa kwenu wasivuke kuja kwetu.” Luka 16:25, 26. {TN3: 118.2}

Hapa, lisilosahaulika, tunaonyeshwa kwamba njia pekee ya kila mmoja wetu anayoweza kuokolewa kutoka kwa adhabu ya kuzimu ni “kumsikia…Musa na

118

manabii “ tukiwa bado hai, na ya kwamba ikiwa hatutawasikia, basi Bwana hawezi kutusaidia baada ya kifo; pia kwamba iwapo hatuwezi kushawishiwa nao, wala “hawatashawishwa hata mtu akifufuka katika wafu. Luka 16:29-31. Hapo hivyo kwa sababu hawana nafasi yoyote ya wokovu baada ya kifo, basi ikiwa yoyote, wakati anaishi, ameshindwa kumsikia “Musa na Manabii,” kwa nini Kristo awahubirie baada ya kufa? “Mungu si Mungu wa wafu, bali wa walio hai.” Mat. 22:32. {TN3: 118.3}

“Roho gerezani” haziwezi, kwa hivyo, kuwa zingine zozote isipokuwa walioishi kabla ya gharika, ambao Kristo, katika umbo la Roho Wake, Aliyemfufua, alihubiri zamani kupitia Nuhu, na Ambaye onyo la Roho halikukawia, na matokeo ya kutisha kwamba kwa kuukataa kusikia mwito Wake, wakawa kimfano gerezani kwa hali ya mafuriko yaliokuwa yakija, kutoka kwa matokeo hakika ambayo hawangaliweza kuepuka. {TN3: 119.1}

Taarifa, isitoshe, “ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji,” huonyesha zaidi kwamba ilikuwa kwa Roho Wake katika kuhubiri kwa Nuhu kwamba Kristo kabla ya gharika Alizitembelea roho gerezani na kuokoa nafsi nane-Nuhu na familia yake . Hivyo “Roho wa Kristo ambayo ilikuwa ndani ya “manabii,” pia “Katika habari ya wokovu huo manabii walitafuta-tafuta na kuchunguza-chunguza, ambao walitabiri habari za neema itakayowafikia ninyi. Wakatafuta ni wakati upi, na wakati wa namna gani ulioonywa na Roho wa Kristo aliyekuwa ndani yao, Ambaye alitangulia kuyashuhudia mateso yatakayompata Kristo, na utukufu utakaokuwako baada ya hayo.” 1 Pet. 1:10, 11.

119

Lakini kama ni kweli, huuliza mtu, kwamba Kristo hakuhubiri kwa wafu, basi ni vipi kuhusu wale waliokuwa wamekufa

2. Kuachwa Bila Fursa? {TN3: 119.2}

Sheria ya kifo haiwezi kutanguliwa kwa upumbavu wa mtu yeyote kumhusu Mungu. Na zaidi ya hayo, “Nimwambiapo mtu mbaya,” asema BWANA kwa nabii Wake, “Hakika utakufa; wewe usimpe maonyo, wala husemi na huyo mtu mbaya ili kumwonya, kusudi aache njia yake mbaya na kujiokoa roho yake; mtu yule mbaya atakufa katika uovu wake; lakini damu yake Nitaitaka mkononi mwako.” Ezek. 3:18. {TN3: 120.1}

Andiko hili hufundisha wazi kwamba wale ambao wamekufa katika dhambi zao, kwa sababu ya kumpuuza mlinzi, hawawezi kuokolewa, na ya kwamba damu yao itahitajika kwa mkono wa mlinzi aliyehusika kwa hatima yao kuwa hawakuokolewa na kuachwa bila fursa. {TN3: 120.2}

Kuwa thabiti, basi, wale ambao wamekufa katika dhambi zao kwa kupuuza kwao wenyewe, aidha kwa ujinga au kwa kukusudia, walivyofanya walioishi kwa dunia ya kabla ya gharika, badala yake kuliko kuwapuuza walinzi, ungekuwa udhuru kidogo kuliko tabaka la awali, na hata ingalikuwa haki kidogo kuliko wao (ambao hawana haki kabisa) kuhubiriwa baada ya kifo, hata kama ingewezekana. {TN3: 120.3}

Na wale ambao kamwe hawajakuwa na fursa ya kuwasikia manabii, kwa wao “Mbingu

120

zauhubiri utukufu wa Mungu, Na anga laitangaza kazi ya mikono Yake. Mchana husemezana na mchana, Usiku hutolea usiku maarifa. Hakuna lugha wala maneno, Sauti yao haisikilikani.” Zab. 19:1-3. {TN3: 120.4}

Wanadamu wote kwa hivyo watahukumiwa kulingana na geji ya nuru ambayo Mungu ameangaza kwenye njia yao, na kulingana na tumaini lao la kutembea katika nuru. Na wale ambao kwa bahati mbaya wameshindwa kujifunza Kwake na kuujua ukweli halisi, hawatahukumiwa kwa kuwa wameamini kosa wakati walipokuwa gizani, lakini “na hii ndiyo hukumu,” asema Bwana, “ya kuwa nuru imekuja ulimwenguni, na watu wakapenda giza kuliko nuru; kwa maana matendo yao yalikuwa maovu.” Yoh. 3:19. {TN3: 121.1}

Kwa nuru kamili ya ukweli mseto kwenye mada, ni dhahiri sana uhakika kwamba Maandiko hayathibitishi fundisho la fursa ya pili. Lakini kwa jitihada za kuthibitisha kwamba yanathibitisha, wale ambao hutetea fundisho kwa ubishi huleta swali la mtume: “Watafanya nini wanao

3. “Batizwa kwa ajili ya Wafu?” 1 Kor. 15:29 {TN3: 121.2}

Akizungumza kwa Wakorintho, mtume Paulo huweka wazi kwamba kama hakuna ufufuo wa wafu, basi hakuna wokovu katika Kristo: {TN3: 121.3}

121

“Tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure. Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, Ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi, Kristo Naye hakufufuka. Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu. Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea. Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote. Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu. Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo wote watahuishwa. Lakini kila mmoja mahali pake; limbuko ni Kristo; baadaye walio Wake Kristo atakapokuja…. Au je! wenye kubatizwa kwa ajili ya wafu watafanyaje? Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao? “ 1 Kor. 15:14-22, 29. {TN3: 122.1}

Andiko hili halifundishi kwamba walio hai wanapaswa kubatizwa kwa ajili ya wafu: kwa maana Paulo haleti hoja ya athari ya ubatizo itakayokuwa kwa wafu, lakini badala yake athari itakayokuwa kwa walio hai: “Nini,” anauliza, “watafanya [walio hai] wanaobatizwa kwa ajili ya wafu?” Si: watakachofanya wafu, ambao sisi, walio hai, tumebatizwa kwa ajili yao. {TN3: 122.2}

Vivyo hivyo, ile taarifa, “kubatizwa

122

kwa ajili ya wafu,” hufundisha kwamba ubatizo kwa ajili ya wafu ni kwa manufaa ya wale tu ambao wanabatizwa wakati wanaishi. Kwa maneno mengine, wanabatizwa, si kwa tumaini la kuishi hadi Bwana atapokuja kuwapeleka kwenye majumba ya milele juu, ila kwa tumaini la kufufuka kutoka kwa wafu siku ya ufufuo. Kwa hivyo swali: “iwapo wafu hawafufuliwi kamwe. . . kwa nini wao hubatizwa?” {TN3: 122.3}

Kutoka kwa uelezaji huu wa ile mada, watakatifu ambao wamebatizwa kwa ajili ya wafu wanaonekana wazi kuwa wale ambao hupita katika hali ya kifo. Na, kwa kiwango kikubwa, wale watakaobatizwa karibu kwa ujio wa Kristo, kuunda kundi hilo la watakatifu walio hai ambao watakuwa wakisubiri kurudi Kwake kwa ushindi, pamoja na malaika Zake wote, wanaonekana, vile vile na wazi, kubatizwa kwa ajili ya walio hai-kamwe kutopita katika hali ya kifo! {TN3: 123.1}

Na mwisho, iwapo Wakristo wa kwanza walipaswa kubatizwa wenyewe kwa ajili ya wengine waliokuwa wamekufa bila ubatizo, amri kama hiyo ingalikuwa imetolewa katika Maandiko, na huduma kama hizo za ubatizo zingekuwa zimeandikwa: Biblia, hata hivyo, huamuru ubatizo tu kwa ajili ya walio hai , ambao huwaambia: “Tubuni, mkabatizwe.” Mdo. 2:38. {TN3: 123.2}

Kwamba mwanafunzi wa kweli wa Biblia aweze kuujua ukweli wa kuokoa kwa wakati huu; Kwa kuujua, aweze kuufuata popote unapomwongoza; ya kwamba akibatizwa kwa ajili ya wafu, aweze kuwa kati ya watakatifu

123

waliofufuliwa, au iwapo anabatizwa kwa ajili ya walio hai, anaweza kuwa kati ya waliohamishwa pasipo kufa: aidha kwa hali kubadilishwa “kwa dakika moja, kufumba na kufumbua” (1 Kor. 15:52), milele kuwa miongoni mwa waliokombolewa wasioweza kufa, waliokombolewa kutoka kwa maumivu na huzuni, baada ya kuingia katika uzima na furaha ya milele, — hili, msomaji mpendwa, ndilo kusudi la pekee katika kuchapisha na kuwasilisha mikononi mwako trakti hii iliyosheheni ukweli. Iwapo umeazimia kuingia katika utukufu ambao inafunua, utafurahia kutahadhari somo lake linalovuma-wazi

Ruhusu Imani Yako Sasa Iwe Ya Utendaji, Si Ya Nadharia Tu. {TN3: 123.3}

Kama dini inayowaacha wafu bila ufufuo na walio hai bila kubadilishwa pasipo kufa ni nzuri kama si kitu chochote, ndivyo lilivyo fundisho la Biblia likiwa tofauti na matendo. Ingawa “mahubiri ya kinadharia ni muhimu, ili wote waweze kujua namna ya fundisho, na kuona mnyororo wa ukweli, kiungo baada ya kiungo, vikiunganisha kuwa mzima kamili…. hakuna mahubiri yatatolewa kamwe bila kumweka mbele Kristo na Yeye aliyesulubiwa kama matumizi ya utendaji kwa kweli zilizoelezwa, na kuwavutia watu kwa ukweli kwamba fundisho la Kristo si ndio na la, ila ndio na amina katika Kristo Yesu.” — Shuhuda, Gombo la 4. uk. 394, 395. {TN3: 124.1}

“Shetani huwapa wanadamu falme za ulimwengu ikiwa watampa ukuu. Wengi hufanya hivyo, na kujinyima

124

mbingu. Ni bora kufa kuliko kutenda dhambi; bora kuhitaji kuliko kulaghai: bora kuwa njaa kuliko kudanganya. Hebu wote ambao wamejaribiwa, wamkabili Shetani kwa maneno haya: ‘Heri kila mmoja anayemcha Bwana, anayetembea katika njia Zake. Kwa maana utapata mazao ya kazi ya mikono yako; utafurahi, na itakuwa salama nawe. Hapa lipo sharti na ahadi ambayo itatambulika bila shaka. Furaha na mafanikio yatakuwa matokeo ya kumtumikia Bwana.” — Shuhuda, Gombo la 4 uk. 495. {TN3: 124.2}

“Kwa sababu hiyo, tukiacha kuyanena mafundisho ya kwanza ya Kristo, tukaze mwendo ili tuufikilie utimilifu; tusiweke msingi tena wa kuzitubia kazi zisizo na uhai, na wa kuwa na imani kwa Mungu” (Ebr. 6:1), au kusahau kwamba “Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema.” 2 Tim. 3:16, 17. {TN3: 125.1}

(Italiki Zote ni Zetu)

FAHARISI YA MADA

HUKUMU NA MAVUNO ………… ……… JALADA

KUKANGANYIKA KWA KUWA MUHIMU…… 3

Hakuna Ila Wafuasi Wake Wanaweza Kuelewa Kweli Yote ………………………………….. …. 3-4

HUKUMU NA MAVUNO KATIKA SHUHUDA, MIFANO, SHEREHE, NA TARAKIMU …………….. 5

KATIKA NURU YA SHUHUDA ZA MANABII ……………………… 5-54

Sababu ya Vitabu? …………….. 6

Sababu ya Hukumu …………………….. 7- 8

Jinsi Majina Yanavyohifadhiwa Katika Kitabu 8-12

Hitimisho Zisizo Na Msingi ………………… 12-13

Chumba cha Kiti cha Enzi cha Mungu cha Muda …….. 13-17

Chumba cha Kiti cha Enzi cha Mungu cha Milele …………… 17-18

125

FAHARISI YA MADA – (Endelea.)

Kwanza Katika Patakatifu, Kisha Katika Patakatifu Mno… 17

Kuondoa Mchafuko Kuhusu Siku 2300 ……………………………. … 21

Lini Siku 2300 Zinaanzia na Kukoma …… 24

Hukumu Miongoni mwa Walio Hai ………………………………….. 42

Hukumu Miongoni mwa Wafu …………………… 49

Sababu Zaidi kwa Hukumu Zote Mbili ………50

KATIKA NURU YA MIFANO …. 54

Wakati wa Kupanda Mbegu …………….. 55

Wakati wa kuongezeka kwa ngano ………….. 58

Wakati wa Kupanda Magugu… 58

Lipi Ndilo Kanisa la Laodekia? ……………. 62

Utengo Wa Magugu Kutoka Miongoni Mwa Ngano ………….. 63

Wakati wa Mavuno ………….. 64

Ni Nani Wavunaji? ………….. 66

Mtengo katika Sehemu Mbili …………. 67

Uhusiano wa Malimbuko na Mavuno Ya Pili ……….. 68

Kanisa sio Babeli …………. 71

KATIKA NURU YA HUDUMA ZA SHEREHE …………………………………….. ………. 72

Mganda wa Kutikiswa, Mikate ya Kutikiswa, na

Siku kuu ya Vibanda ……………… 75

Malimbuko na Mganda wa Kutikiswa na Mikate ya Kutikiswa ………………………………….. 76

Kristo Akisi wa Mganda wa Kutikiswa …. 79

Mganda wa Kutikiswa wa Walio Hai ……………… 80

Mavuno ya Pili na Siku kuu ya Vibanda …………………………………… …… 80

KATIKA NURU YA TARAKIMU ……………. 88

Tarakimu ya Mwokozi ………………….. 90

Idadi ya Watakatifu kwa Pentekoste …. 91

Kristo na Biblia …………….. 92

Tarakimu ya Biblia ………. 92

Tarakimu ya Wakati wa Kukusanywa Ndani wa Biblia……….. 93

Tarakimu ya Miaka Kristo ni Mwokozi …… ..93

Waliohesabika Watakatifu Walio Hai…………….. 96

EPUKA MITEGO MINGI …………. 100

UJUMBE WA MALAIKA YA KWANZA ….. 114

MASWALI NA MAJIBU ……….. 117

1. Je! Kristo alihubiri kwa wafu? 1 Pet. 3:18-20 ……………………………………… …. 117

2. Kuachwa Bila Fursa? …………………… 120

3. “Kubatizwa Kwa Wafu?.” 1 Kor. 15:29.121

RUHUSU IMANI YAKO SASA IWE YA UTENDAJI. SI YA NADHARIA TU ………………………………….. 124

FAHARISI YA MAANDIKO

MWANZO: 23:16, 17. … … 78

1: 5 …………… .22 23: 27-29 … ….. … 73

4:10 ……… … ..101 23:36 … … … .57,76 KUTOKA: 23: 39,40,42. 76,81

23: 16 ………… … 54 YOSHUA:

31:16. 17 …… .. … 32 7:13, 24, 25 …

32:33 …………… … 7 EZRA:

7: 21-27 …… …… 39

WALAWI: ZABURI:

16: 2 …… .. …… … 110 1: 5 ……… … … 42

16: 16 ………… … 110 19: 1-3 ………

16: 30,33 …… .. … ..73 43: 3 … … … .90

16: 34 ………… .. … 73 69:28 … … 11,73

23: 10,11 ……… ….. 75 87: 6 ……… .. … 6

23: 11,14 … .. …… … 78 119: 105 … ..88

23: 14-17 … .. … .75-76 139: 16 ……… … 6

126

FAHARISI YA MAANDIKO – (Endelea.)

MITHALI:

14:12 …………………………… ……………..

MHUBIRI:

5: 6 ………………………………… .. … .8-9

9: 5 …………………………………… ..101

9: 5,6 ………………………………… … 118

ISAYA:

25: 1 …………………………………… ..99

28: 22 ………………………………… …. 84

55:12 ……………………………………….. … 101

55: 7,8 ……………………………………… ………. 113

62: 2-4,12 ……………………………………. ………. 74

63: 5,6 ……………………………………… ………. 49

65: 11,15 ……………………………………… …… 74

63: 5,6 ……………………………………… ………. 63

66: 16,17 ……………………………………… .68,69

66:19 ……………………………………….. ……… 70

66:20 ……………………………………….. …. 70,99

YEREMIA:

8:20 ……………………………………….. ……….. 70

17:13 ……………………………………….. …….. 7,8

23:21 ……………………………………….. ………. 114

EZEKELI:

1 …………………………………………. …………… 47

1:10 ……………………………………….. ……….. 46

3:18 ……………………………………….. ……… 120

3:20 ……………………………………….. …………….. 11

4: 6 …………………………… …………. 56

9 …………………………………………. ……… 49,86

FAHARISI YA MAANDIKO – (Endelea.)

4:14 ……………………………………….. ………… 74

YOELI:

2:28, 32 ……………………… ……………. 96

HABAKUKI:

2:14 ……………………………………….. ……….. 90

ZEKARIA:

14:20, 21 ……………………………………… …. 74

MALAKI:

3: 1-3 …………………………………….. 43 , 47, 49

3: 2,3 ……………………………………… ………… 46

MATHAYO:

3: 7, 8 ……………………………………… ……….. 59

4:17 ……………………………………….. …………. 6

7:23 ……………………………………….. ……… 114

10:30 ……………………………………….. …………….. 8

13: ………………………………………… ………… 82

13:11 ……………………………………….. ……….. 3

13: 27-30 ……………………………………… …… 64

13:30 …………………………… 42, 49 , 65

13:37 ……………………………………….. ……… 56

13:38 ……………………………………….. … 66, 68

13:39 ……………………………………….. …. 56,66

13:40 ……………………………………….. ……… 66

13: 44-46 ……………………………………… ….. 3,4

13: 47-49 ……………………………………… ..42, 49

13:47, 48 ……………………………………… ….. 67

13:49 ……………………………………….. … 48, 66

127

20 …………………………………………. ………, 92

22:23 ……………………………………….. … 119

24: 1 …………………………… …………. 7

24:14 ……………………………………….. ……… 99

24:15, 16 ……………………………………… ….. 25

24:31 ……………………………………….. ……… 53

25 …………………………………………. ………. 45, 47

25: 1-5 ……………………………………… ………. 60

25: …………………… … 31, 34, 41 … 45-46

MARKO:

4:16, 17 ……………………… ……………… 7

13:34 ……………………………………….. ……… 58

LUKA:

4: 4 …………………………… …………. 89

6:22, 23 ……………………………………… ………. 61

12:10 ……………………………………….. ……… 10

16:25, 26 ……………………………………… … 118

16: 29-31 ……………………………………… …. 119

YOHANA:

1:14 ……………………………………….. ……….. 92

3:19 ……………………………………….. ……… 121

6:63 ……………………………………….. ……….. 89

7:17 ……………………………………….. …………. 3

14: 1-3 ……………………………………… ……… 49

14: 6 …………………………… …………. 4

16:11 ……………………………………….. ……… 10

MATENDO YA MITUME:

1: 3, 9 ……………………………………… ……….. 86

2: 14-21 ……………………………………… ……. 96

2:38 ……………………………………….. ……… 123

4:12 ……………………………………….. ……….. 96

5: 3, 5, 7, 8, 10 ……………… 60

7:56 ……………………………………….. ……………… 17

10:28 ……………………………………….. ……… 40

WARUMI:

14: 5 ………………………………….. ……….. 62

1 WAKORINTHO:

2: 9 …………………………… …………. 13

10:11 ……………………………………….. ………..

10:12 ……………………………………….. ……… 11

15: 14-22, 29 …………………………………… 122

15:29 ……………………………………….. ………. 121

15:52 ……………………………………….. …….

WATHESALONIKE:

4:16 ……………………………………….. ……….. 49

4:16, 17 ……………………………………… ………. 45

2 TIMOTHEO:

2: 3 ……………………………………….. …………… 8

3:16, 17 ……………………………………… ….. 125

WAEBRANIA:

2: 1 …………………………… …………. 54

6: 1 …………………………… ……….. 125

6:19 ……………………………………….. ……… 109

6: …………………… .19, 20..107,108,109

6:20 ……………………………………….. ……… 109

8: 1, 2 ……………………………………… …… 19-20

9: 3 …………………………… ……….. 110

9: 1-9 ……………………………………… ………… 13

9: 12 …………………… … 19, 108, 109, 110

9:24 ……………………………………….. ……………… 20

9: 24-27 ……………………………………… 24, 128

9:26 ……………………………………….. … 21, 108

9:26, 27 ……………………………………… ………. 20

10: 35-37 ……………………………………… …. 19

1 PETERO:

1:10, 11 ……………………………………… …. 119

3: 18-20 …………………………………….. 97 , 117

4:17 ……………………………………….. ………… 8

2 PETRO:

1:12 ……………………………………….. ……….. 10

1: 19-21 ……………………………………… …….. 12

1: 20-21 ……………………………………… ….. 114

3: 3, 4 ……………………………………… ……… 112

3: 8 ……………………………………….. ………… 95

1 YOHANA:

1: 1 ……………………………………….. ………… 92

UFUNUO:

3:17 ……………………………………….. ………. 10

4 …………………………………………. ……………

4: 1 …………………………… ………. 114

4: 5 …………………………… …………. 47

4: 1-6 ……………………………………… ……………… 13

4: 2-6: …………………………………….. ………… 87

4: 6 …………………………… ………….

4: 7 ……………………………………….. ………… 46

5 …………………………

5: 6 …………………………… ………… 15

5: 8, 9 ……………………………………… ………..

5:11 ……………………………………….. …. 15, 46

6: 9, 10 ……………………………………… …….

7: 3 …………………………… ………… 70

7: 3-8 ……………………………………… ……….. 86

7: 9 …………………………… ………… 70

7: 9, 11 ……………………………………… ……… 87

8: 1 …………………………… ………… 47

8: 5 ……………………………………….. ………… 47

10:22 ……………………………………….. ……..

13: 1-10 ……………………………………… ………. 94

13:25 ……………………………………….. ………

14 …………………………………………. …………. 49

14: 4 …………………………… ………. 71

14: 1-5 ……………………………………… ……… 86

14: 5 ………………………………….. ………. 62

14: 6-11 ……………………………………… 62, 67

14: 6-12 ……………………………………… ….. 115

14: 7 ……………………………………….. ..41, 114

14: 14-16 ……………………………………… ….. 48

14: 17-20 ……………………………………… ……

15: 1 …………………………… ………. 48

17: 1-3 ……………………………………… ……… 94

18: 4 ……………………………………….. …. 49, 68

20: 3 ……………………………………….. ………. 95

20: 5 ……………………………………….. ………. 50

20: 6 ……………………………………….. ………. 50

20:11 ……………………………………….. ……..

20:12 ……………………………………….. …. 6, 95

21:14 ……………………………………….. …….. 97

22: 1, 2 ……………………………………… …….. 17

22:13 ……………………………………….. ………

22:19 ……………………………………….. ……………… 7

128

>