fbpx

KARIBU KATIKA GADSDA

Jumuiya ya Wadaudi Waadventista wa Sabato

S.L.P. 23738, Waco, TX 76702

Tupigie Simu: 254-855-9539

Tutumie barua pepe: info@gadsda.com

LENGO LETU

Y

a mpito kwa kuanzishwa na vile vile kwa jina, Jumuiya ya Wadaudi Waadventista wa Sabato ipo tu kukamilisha kazi iliyowekwa na Mungu ndani ya dhehebu la Waadventista wa Sabato, ambamo kwa hivyo huzuilia shughuli zake kikamilifu. Kadiri kazi yake humo ndani inakaribia kufunga, na “watumwa wa Mungu wetu” (Ufu. 7:3) wanatiwa muhuri, jina lake litabadilishwa (Isa. 56:5; 62:2; 65:15) na kusudi lake na kazi yake itakuwa ya kuikumbatia injili yote (Mat. 17:11; Mdo. 3: 21; Isa. 61:4-7). Wakati huo Katiba yake na Sheria ndogo jinsi zilivyoratibishwa hapa ndani zitaanza kufanya kazi kikamilifu.

Lengo la Jumuiya hii ni kuleta miongoni mwa watu wa Mungu yale matengenezo yaliyoitishwa katika Shuhuda kwa Kanisa, Gombo la 9, ukurasa wa 126, kama vuguvugu la lazima la kutangaza “Mwito wa saa Kumi na Moja” (Mat. 20:6, 7) wa “Injili ya milele … kwa kila taifa, na jamaa, na lugha, na watu.” Ufu 14:6. Kupitia mwito huu, Kilio Kikuu cha jumbe za malaika watatu, itawakusanya “watu wa watakatifu wake Aliye Juu” (Dan. 7:27) katika ufalme “ambao hautaangamizwa milele … bali … utavunja vipande vipande na kuziharibu falme … zote.” Dan. 2:44. Hivyo utakaribisha utawala wa Kristo kama Bwana wa mabwana na Mfalme wa wafalme kwa dunia yote milele na milele.

JINA LETU

Jina, Wadaudi, linapatikana kutoka kwa jina la mfalme wa Israeli ya Zamani, lipo kama dai halali la kutekelezwa na Jumuiya hii kwa sababu ya vipengee vyake vifuatavyo: Kwanza, imetiwa wakfu kwa kazi ya kutangaza na kuleta urejesho (jinsi ulivyotabiriwa katika Hosea 1:11; 3:5) wa Ufalme wa Daudi katika uakisi, kwa kiti cha enzi ambacho Kristo, “mwana wa Daudi,” ataketi. Pili, hudai yenyewe kuwa ni ya kwanza ya malimbuko ya walio hai, watangulizi kutoka kwa wazawa wa siku ya leo wa wale Wayahudi waliofanza Kanisa la Kikristo la Kwanza. Katika kujitokeza kwa watangulizi hawa na jeshi lake, malimbuko, ambamo wanachaguliwa 12,000 kutoka kati ya kila moja ya makabila kumi na mawili ya Yakobo, “watu 144,000” (Ufu. 14:1; 7:2-8) ambao watasimama juu ya Mlima Zayuni na Mwana-Kondoo (Ufu. 14:1; 7:2-8), utawala wa Daudi wa uakisi unaanza.

Jina Waadventista wa Sabato, ambalo Jumuiya hii hurithi kutoka kwa dhehebu mzazi, ni la mpito (Isa 62:2) na kwa muda pekee wa kazi yake ndani ya dhehebu mzazi.

11th Hour Trumpeter Logo with Transparent Background
>